Ngokolo, Shinyanga: Mume ajinyonga kwa mtandio baada ya kugombana na mkewe

Kwanini mke akope? Jibu ni moja tu; alikuwa haachiwi Pesa za kutosha mahitaji ya familia ya watu watano. Kwa maana nyingine yeye marehemu ndio sababu ya yote japo ameyakimbia majukumu kiana na kumwachia mkewe. Tutegemee idadi ya watoto wa mitaani kuongezeka.
 
Kujinyonga siyo suluhisho. Nahisi huo ni msongo wa mawazo umesababisha yote hayo. Haswa kwa mtu uliyekuwa unampenda sana hukutegemea akufanyie yote hayo.

Nawashauri watu wakiwa kwenye lindi kubwa la mawazo watafute vitu vya kuwasaidia kama kuwashirikisha marafiki, kusali sana na hata kuchukua muda mwingi kuongea na wanao kama mke/ mume amekuudhi watakuwa faraja yako

Unaweza ukakimbiwa na mume/mke lakini watoto watakuwa karibu yako. Kuongea nao tu hata kama ni wadogo ni faraja kubwa sana kwako na kuona kuwa bado kuna uhitaji mkubwa wa kuishi na kuwasaidia wanao waweze kuwa na maisha mazuri na kujivunia kuwa angalau yupo.mzazi mmoja anayewajali.

Kuongea na marafiki hukusaidia kushare experience katika ndoa. Nakuhakikishia Unaweza fikiri kuwa unapitia mambo magumu lakini ukiongea na wenzako utajiona cha mtoto. Kumbe wapo wanaopita mambo makubwa kuliko hayo. Na hii ikakusaidia kufahamu kuwa ni mapito tu mambo yatakuwa vyema.

Kusali sana, hili litakusaidia kuepuka kufanya mabaya kama kujiua au kumwua mwenzako. Maana ukiwa na hofu ya Mungu huwezi kufanya yote hayo. Katika kusali utajikuta hata kama mwandani wako anakuudhi unamuombea ili kama kuna roho chafu zimemuingia zitoke. Na utakavyozidi kumfanyia vyema ndivyo atakavyobadilika na kuwa mtu mwema.

Jamani mke/mume hatukuzaliwa nao. Tumewakuta ukubwani isiwe sababu ya kutuondolea uhai kabisa. Maisha yetu ni ya muhimu sana. Mtu akikuacha mwacha aende na hamsini zake.
Good idea
 
watu bdo wanajiua kuhusu mapenzi kwa Marne ya Leo?? Kumbe wasukuma nanyi bdo mpo nyuma sana
 
Kwanini mke akope? Jibu ni moja tu; alikuwa haachiwi Pesa za kutosha mahitaji ya familia ya watu watano. Kwa maana nyingine yeye marehemu ndio sababu ya yote japo ameyakimbia majukumu kiana na kumwachia mkewe. Tutegemee idadi ya watoto wa mitaani kuongezeka.

Hapana, kuna ugonjwa wa kina mama wa kutaka kuwa na kila kitu, hivyo kuishia kujiunga na vikoba na kukopa kila kona... hilo ni tatizo nadhani kikubwa ni tamaa...
 
Khaa! Hiyo nyumba ya marehemu mbona haiendani na hizo pavements? Au wamezipata kwa deal? :eek::eek::eek: Maana pavements kama hizo tumezoea kuziona mitaa ya Masaki!
 
Huyu marehemu alijiua bure kutesa watoto, ujinga wa mwanamke yeye anajinyonga. Labda siku zake zilishatimia.
Usahihi wa jambo angeagana naye tu.. Kwaheri kila mmoja ashike lake
 
Inaonekana qumq za kanda ya ziwa taaamu sana mpaka haya ma kina ngosha yanajiua na kuua kisa lipochi manyoya
 
wengi wanaishi lakini nafsini mwao wana matatizo makubwa zaidi.....

kujiua sio suluhisho, inatakiwa ni kupambana na changamoto.....
 
Inasikitisha sana...

Inatia sana haisra...

Ila hata iweje kwa nini ujiue, si mnaachana tu...
Msiba ukitulia huyo mwanamke sasa auze vyote mpaka naniliii yake...


cc: mahondaw
 
Back
Top Bottom