Ngeleja: Uzembe wa usimamizi wa sheria ndio umelifikisha taifa hapa, sheria nzuri ila hazisimamiwi

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,261
99a41c01fbf8dbf96fdf4401568ad22e.jpg
Mbunge wa Sengerema kwa Chama cha Mapinduzi (CCM), William Ngeleja amesema kuwa hawezi kuzungumzia agizo la Rais Magufuli la kuhojiwa na vyombo vya usalama kutokana na kuhusika kwake katika mikataba ya madini.

Hata hivyo alitaja uzembe wa usimamizi wa sheria kuwa ndiyo uliolifikisha Taifa hapo kwa kuwa sheria zilizopo ni mzuri, lakini hazisimamiwi ipasavyo.

"Kuhusu kuhojiwa au kuwajibika sina neno la kusema lakini nampongeza sana kwa moyo wa dhati Muheshimiwa Rais maana amezungumza kwa hisia na uzalendo kabisa kuhusu tunachostahiki kupata badala ya tunachopata ", alisema Ngeleja ambaye pia ni mbunge wa Sengerema.

Hata hivyo alikiri mikataba mingi iliyopitishwa siyo mizuri kwa kuwa inawanyonya Watanzania ambao wameshindwa kupitia sheria mpya (ya madini ya mwaka 2010)
kuifanyia kazi.

" Kifungu cha 11 pia kinachosema mikataba yote ipelekwe bungeni baada ya miaka ya mitano na kifungu cha 10 kinasema Serikali ishiriki kimkakati kwenye migodi, lakini usimamizi wake ni shida", alisema Ngeleja

Kuhusu mchanga kusafilishwa nje ya nchi, alisema walishaliona jambo hilo mapema lakini wakabainisha kuwa mashine za kufanya kazi hiyo zina gharama kubwa duniani zaidi hivyo kuhitaji ubia katika ujenzi baina ya Serikali na sekta binafsi.


Chanzo: Mwananchi
 
huyu jamaa escrow alipewa hela ndogo sana lakini ikamtesa vibaya mno.. bora wenzake kina chenge walilipwa mabilioni
 
99a41c01fbf8dbf96fdf4401568ad22e.jpg
Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja amesema kuwa hawezi kuzungumzia agizo la Rais Magufuli la kuhojiwa na vyombo vya usalama kutokana na kuhusika kwake katika mikataba ya madini.

Hata hivyo alitaja uzembe wa usimamizi wa sheria kuwa ndiyo uliolifikisha Taifa hapo kwa kuwa sheria zilizopo ni mzuri, lakini hazisimamiwi ipasavyo.

"Kuhusu kuhojiwa au kuwajibika sina neno la kusema lakini nampongeza sana kwa moyo wa dhati Muheshimiwa Rais maana amezungumza kwa hisia na uzalendo kabisa kuhusu tunachostahiki kupata badala ya tunachopata ", alisema Ngeleja ambaye pia ni mbunge wa Sengerema.

Hata hivyo alikiri mikataba mingi iliyopitishwa siyo mizuri kwa kuwa inawanyonya Watanzania ambao wameshindwa kupitia sheria mpya (ya madini ya mwaka 2010)
kuifanyia kazi.


" Kifungu cha 11 pia kinachosema mikataba yote ipelekwe bungeni baada ya miaka ya mitano na kifungu cha 10 kinasema Serikali ishiriki kimkakati kwenye migodi, lakini usimamizi wake ni shida", alisema Ngeleja

Kuhusu mchanga kusafilishwa nje ya nchi, alisema walishaliona jambo hilo mapema lakini wakabainisha kuwa mashine za kufanya kazi hiyo zina gharama kubwa duniani zaidi hivyo kuhitaji ubia katika ujenzi baina ya Serikali na sekta binafsi.


Chanzo: Mwananchi
kwenye red sijamuelewa, inamaana anapingana na mwenyekiti wake? Jana mh rais alisema sheria zikapitiwe tena, yeyeanasema sheria ni nzuri. Pia anakiri mikataba inawanyonya watanzania, inamaana mikataba ipo nje ya sheria anazoziita nzuri? kwahiyo sheria nzuri zilipitisha mikataba hovyo, inaiingia akilini?
 
Kamanda Sirro! Huyu jamaa mbona bado yupo kitaa!? Kamata, weka ndani atuambie kama alikula mlungura.
 
kwenye red sijamuelewa, inamaana anapingana na mwenyekiti wake? Jana mh rais alisema sheria zikapitiwe tena, yeyeanasema sheria ni nzuri. Pia anakiri mikataba inawanyonya watanzania, inamaana mikataba ipo nje ya sheria anazoziita nzuri? kwahiyo sheria nzuri zilipitisha mikataba hovyo, inaiingia akilini?
Angesema mchawi ni Sheria mbovu bila shaka angeeleweka sana.
 
Ndo mlokula 10 percent nyie, yaani mwanasheria unaona leo mikataba ilikuwa mibovu ? Au ulimuogopa Boss mkwere ?
 
Hata hivyo alitaja uzembe wa usimamizi wa sheria kuwa ndiyo uliolifikisha Taifa hapo kwa kuwa sheria zilizopo ni mzuri, lakini hazisimamiwi ipasavyo....

Eti sheria ni nzuri ? Sheria ya kuwapa wawekezaji asilimia 96 na kutachia sisi wenye mali asilimia 4 ina uzuri gani?

Na huo uzembe wa kusimamia sheria mbona yeye hakuuondoa wakati akiwa waziri?


 
Kwa hiyo anapingana na Magufuli aliesema sheria zote mbovu zirudi bungeni zikarekebishwe upya
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom