Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Ngawaiya atangaza kumvaa Ndesamburo
Daniel Mjema, Moshi
BAADA ya kukaa nje kwa kipindi kimoja, mbunge wa zamani wa Moshi Vijijini, Thomas Ngawaiya sasa anataka kurudi tena bungeni, lakini amechagua njia ambayo itambidi afanye kazi ya ziada; kumngâoa Philemon Ndesamburo jimbo la Moshi Mjini.
Ngawaiya, ambaye alikuwa mbunge wa Moshi Vijijini kwa tiketi ya TLP kwa kipindi kimoja (2000 hadi 2005), atavaana na Ndesamburo wa Chadema kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu iwapo atapitishwa na chama chake kipya cha CCM.
Akitangaza nia yake ya kurudi bungeni, Ngawaiya alisema kuwa ameamua kugombea ubunge wa Moshi Mjini kwa sababu ana hoja za msingi ambazo hazijafanyiwa kazi kwa miaka 15 ambayo jimbo hilo limekuwa chini ya upinzani.
Awali Ngawaiya ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM alikuwa ameonyesha nia ya kuwania Jimbo la Moshi Vijijini linaloshikiliwa na Dk Cyrill Chami, lakini sasa amebadili msimamo huo na kujikita Moshi Mjini.
Hatua hiyo ya Ngawaiya imekuja miezi michache tangu mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM, Anne Kilango Malecela atangaze uamuzi wa kupiga kambi katika jimbo hilo ili kuhakikisha CCM inamng'oa Ndesamburo.
Ngawaiya alitangaza msimamo huo mbele ya wajumbe wa kamati ya siasa ya CCM wilayani Moshi Mjini katika kikao chake kilichofanyika juzi.
"Nina hoja ya msingi hapa kwamba katika kipindi chote Ndesamburo hajaweza kutatua tatizo la ajira kwa vijana na wala hawajui wafanye nini; viwanda vimekufa na hakuna anayepigania vifufuliwe," alisema Ngawaiya alipoongea na waandishi wa n habari baadaye jana.
Aliongeza kuwa jimbo la Moshi Mjini halina mwakilishi bali ni mfadhili na kuongeza kuwa anachokifanya Ndesamburo kinaweza kufanywa na mfadhili yoyote, hasa ikizingatiwa kuwa anapata Sh12 milioni za jimbo kwa mwaka.
Ngawaiya alisema japokuwa yeye si mbunge, tayari ameshafanya mazungumzo na Waziri wa Fedha ili kuwashawishi wawekezaji kuanzisha viwanda vipya na kuwanyangâanya wale walioshindwa kuviendeleza.
Mwanasiasa huyo ambaye alikuwa amefuatana na katibu wa Jumuiya ya Wazazi mkoani Kilimanjaro, Godliver Kamala alisema ajira ya wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama machinga, hailipi na imekuwa ni adha kubwa.
"Lakini mimi nitasimamia kuanzishwa kwa viwanda vya kusaga kahawa hapa hapa Moshi ili tuuze kahawa yenu ikiwa imeongezwa thamani kwa sababu kuanzishwa kwa viwanda hivyo kutapanua wigo wa ajira," alisema.
Alipoulizwa ni kwanini ameamua kumkimbia Dk Chami Moshi Vijijini, Ngawaiya alisema lingekuwa ni jambo la ajabu kwenda kupambana na mbunge ambaye yeye alimpigania ashike wadhifa huo mwaka 2005.
Ngawaiya alisema Dk Chami amefanya mambo makubwa ya kimaendeleo katika jimbo hilo hivyo haoni sababu ya msingi ya kumuondoa kwa sasa kwani anakubalika kwa wananchi kutokana na maendeleo aliyosimamia. Hatua hiyo ya Ngawaiya inafanya idadi ya wanachama wa CCM waliojitokeza kuchuana na Ndesamburo kufikia wawili baada ya aliyekuwa mhasibu wa ofisi ya mkuu wa mkoa Kilimanjaro, Gibson Lyamuya kutangaza nia hiyo.
Daniel Mjema, Moshi
BAADA ya kukaa nje kwa kipindi kimoja, mbunge wa zamani wa Moshi Vijijini, Thomas Ngawaiya sasa anataka kurudi tena bungeni, lakini amechagua njia ambayo itambidi afanye kazi ya ziada; kumngâoa Philemon Ndesamburo jimbo la Moshi Mjini.
Ngawaiya, ambaye alikuwa mbunge wa Moshi Vijijini kwa tiketi ya TLP kwa kipindi kimoja (2000 hadi 2005), atavaana na Ndesamburo wa Chadema kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu iwapo atapitishwa na chama chake kipya cha CCM.
Akitangaza nia yake ya kurudi bungeni, Ngawaiya alisema kuwa ameamua kugombea ubunge wa Moshi Mjini kwa sababu ana hoja za msingi ambazo hazijafanyiwa kazi kwa miaka 15 ambayo jimbo hilo limekuwa chini ya upinzani.
Awali Ngawaiya ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM alikuwa ameonyesha nia ya kuwania Jimbo la Moshi Vijijini linaloshikiliwa na Dk Cyrill Chami, lakini sasa amebadili msimamo huo na kujikita Moshi Mjini.
Hatua hiyo ya Ngawaiya imekuja miezi michache tangu mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM, Anne Kilango Malecela atangaze uamuzi wa kupiga kambi katika jimbo hilo ili kuhakikisha CCM inamng'oa Ndesamburo.
Ngawaiya alitangaza msimamo huo mbele ya wajumbe wa kamati ya siasa ya CCM wilayani Moshi Mjini katika kikao chake kilichofanyika juzi.
"Nina hoja ya msingi hapa kwamba katika kipindi chote Ndesamburo hajaweza kutatua tatizo la ajira kwa vijana na wala hawajui wafanye nini; viwanda vimekufa na hakuna anayepigania vifufuliwe," alisema Ngawaiya alipoongea na waandishi wa n habari baadaye jana.
Aliongeza kuwa jimbo la Moshi Mjini halina mwakilishi bali ni mfadhili na kuongeza kuwa anachokifanya Ndesamburo kinaweza kufanywa na mfadhili yoyote, hasa ikizingatiwa kuwa anapata Sh12 milioni za jimbo kwa mwaka.
Ngawaiya alisema japokuwa yeye si mbunge, tayari ameshafanya mazungumzo na Waziri wa Fedha ili kuwashawishi wawekezaji kuanzisha viwanda vipya na kuwanyangâanya wale walioshindwa kuviendeleza.
Mwanasiasa huyo ambaye alikuwa amefuatana na katibu wa Jumuiya ya Wazazi mkoani Kilimanjaro, Godliver Kamala alisema ajira ya wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama machinga, hailipi na imekuwa ni adha kubwa.
"Lakini mimi nitasimamia kuanzishwa kwa viwanda vya kusaga kahawa hapa hapa Moshi ili tuuze kahawa yenu ikiwa imeongezwa thamani kwa sababu kuanzishwa kwa viwanda hivyo kutapanua wigo wa ajira," alisema.
Alipoulizwa ni kwanini ameamua kumkimbia Dk Chami Moshi Vijijini, Ngawaiya alisema lingekuwa ni jambo la ajabu kwenda kupambana na mbunge ambaye yeye alimpigania ashike wadhifa huo mwaka 2005.
Ngawaiya alisema Dk Chami amefanya mambo makubwa ya kimaendeleo katika jimbo hilo hivyo haoni sababu ya msingi ya kumuondoa kwa sasa kwani anakubalika kwa wananchi kutokana na maendeleo aliyosimamia. Hatua hiyo ya Ngawaiya inafanya idadi ya wanachama wa CCM waliojitokeza kuchuana na Ndesamburo kufikia wawili baada ya aliyekuwa mhasibu wa ofisi ya mkuu wa mkoa Kilimanjaro, Gibson Lyamuya kutangaza nia hiyo.