Ha ha haa! Mkopo ulikuwa mwaka mmoja ambao ndio umeisha, dogo alisaini bila kusoma kilichoandikwa, aliongeza mmoja hadi 2014. Si umesikia anajitetea kwamba "mimi sikujua"? Kuhusu kipigo ndo hivyo tena, safari hii tutasajili mchanganyiko wa vijana na wazoefu !Kule alienda kwa mkopo mkuu wangu Sinkala, pole kwa kipigo
basi itakuwa haina tofauti na 'ugaidi' wa mpira. Naamini binafsi watu wenye mapenzi mema na mpira (mpira sio timu moja) inabidi walaani hiki kitendo kama kweli kilitokea. Kumbe ndizo fitna za soka la bongo hizi, clearly hatutakaa tukawaona akina Nonda, Malliga, Oliechi, Katongo nk wakitokea hapa kwetu!Ni sahihi mkuu!
Ata baadhi ya vyombo vya habari vimeriport juu ya hili.
Ha ha haa! Mkopo ulikuwa mwaka mmoja ambao ndio umeisha, dogo alisaini bila kusoma kilichoandikwa, aliongeza mmoja hadi 2014. Si umesikia anajitetea kwamba "mimi sikujua"? Kuhusu kipigo ndo hivyo tena, safari hii tutasajili mchanganyiko wa vijana na wazoefu !
Karibu nyumbani Ngassa ulikuwa umepotea
Ahsante sana mkuu kwa mipicha!
Jf ni zaidi ya habari!
Hahahahahahaaaa!IVI Ngassa ina single s au double s????? kama wenyewe Yanga hamjui ata jina sahihi lake iyo inaonesha hamko serious nae....Ila Ngassa nae hamnazo bongo mpk lini wewe mtoto? umri ushaenda huo utu uzimani utakuwa unafanya nn sasa?
Wagumu kukumbuka lakini wepesi kusahau, hivi Umesahau ni miezi michach etu nyuma kuna watu walilia uwanjani kama watoto walionyimwa wali na maharage na mwingine babu wa watu Moro goro alifariki ghafla baada ya kupigwa mkono kwa bila.Kwanza nawapongeza first 11 na wachezaji wote kwa kazi nzuri ya kutuondolea kelele mtani jamaa walilala mapema hata ulinzi ilikuwa rahisi, zaidi nawpongeza viongozi makini wa klabu yetu. Ushauri wangu kwa Simba wafungue mradi wa kuuza maduka mtaa wao kwa biashara uko vizuri, pia wagombee ubunge mpira watuachie!
Maji kupwa maji kujaa, na wale machangudoa wa Sinza atawaachia nani? Chezea Sinza wewe ndiyo maana hata Sudan alikataa kwenda aliona atawamiss.Huyo nae ni mchezaji wa kutegemewa?Mchezaji gani leo ancheza vizuri kesho anacheza vibaya mara anabweteka amini hicho mmepata kimeo, muda si mrefu utakumbuka ninayokuambia leo.Kwa uhakika zaidi hebu Tazama alivyokuwa anacheza AZAM, anavyocheza Simba na anavyocheza Taifa Stars, hicho ni kimeo.
Ngasa sio mtoto kama mnavyodhani,yule ni kibabu wa kichina!Waulize watu wa Mwanza hususan Magu watakwambia ameanza kucheza lini tena akiwa na familia yake mama na watoto kadhaa!Nitawashangaa Simba wakifanya uhuni wa kumsainisha kama wazungu walivyomfanya Sultani Mangungo wa Msovero!Mimi nawashauri viongozi wa Simba waachane na Ngasa hata kama kweli alisaini mwaka mmoja zaidi, wahangaike kutafuta wachezaji wengine tu kama ni kutoka timu zingine sawa, kama ni kutoka nje ya nchi sawa, kama ni kupandisha wengine kutoka timu B sawa, lakini hawatakiwi kuanza kumgombea huyu mtoto, wamwache aende kula roho yake inapenda na mimi namtakia kila la heri katika maisha yake ya soka.