Ngasongwa: Inatia hofu mawaziri kushtakiwa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Date::1/19/2009
Ngasongwa: Inatia hofu mawaziri kushtakiwa
Exuper Kachenje
Mwananchi​

WAZIRI wa zamani wa Mipango, Uchumi na Uwekezaji katika utawala wa awamu ya tatu, Dk Juma Ngasongwa amesema hatua ya serikali kuwafikisha mahakamani viongozi waandamizi wa serikali, wakiwemo mawaziri kwa makosa waliyofanya wakiwa madarakani, inatia hofu.

Ngasongwa alitoa kauli hiyo alipozungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili nyumbani kwake jijini Dar es Salam jana.

Dk Ngasongwa alisema: "Ukimshtaki mtu kwa maamuzi aliyoyafanya akiwa madarakani, ukweli inatia mashaka. Inatakiwa kuwa makini kidogo katika kulitazama suala hilo. Pale serikalini kuna mambo mtu anaweza kuamua si kwa sababu alifikiria kufanya ufisadi. "

Alifafanua kuwa kwa watendaji wa serikali, inawezekana mtu alifanya maamuzi kwa sababu alilazimika kufanya hivyo kwa sababu zilizopo wakati huo na si kwa kufikiria kufanya ufisadi.

Aliongeza kuwa, kama binadamu baadaye anaweza kugundua maamuzi yake hayo ya awali kuwa hayakuwa sahihi na kuhitaji kusahihisha, lakini hushindikana kwa kuwa tayari anakuwa nje ya nafasi hizo.

"Pengine angepata nafasi, angesahihisha," alisema waziri huyo wa zamani. Dk Ngasongwa, ambaye ni mbunge wa Ulanga Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisisitiza kuwa ni muhimu suala hilo likaangaliwa vizuri na kwa umakini zaidi. Hata hivyo, alisema kuwa watu ambao wanatuhumiwa kwa ufisadi wote wafikishwe mahakamani, washtakiwe na mahakama iamue kuwahukumu kwa ushahidi na iwapo hawataridhika wakate rufaa.

"Kama mtu kweli alifanya ufisadi, basi hilo sawa. Watu ambao walifanya ufisadi kama ule wa EPA hilo ni dhahiri, wanastahili washtakiwe na mahakama siku zote tunaiheshimu, iamue lazima mmoja atusaidie, kama hataridhika atakata rufaa. "Lakini wale watu wa EPA nadhani ni muhimu wakashtakiwa. Washtakiwe kweli, kusiwe na danganya toto. Washtakiwe na utaratibu uende kwa makini... watakaonekana wana hatia, wahukumiwe kwa mujibu wa sheria."

Vita ya ufisadi hadi sasa imechukua sura tatu kuu; watu wanaotuhumiwa kuiba jumla ya Sh133 bilioni katika Akaunti ya Malipo ya Malimbikizo ya Madeni ya Nje (EPA), mawaziri wanaotuhumiwa kutumia vibaya ofisi zao na kutumia uongo ili kupata tenda ya serikali ya ufuaji umeme wa dharura.

Watu 21 wameshafikishwa mbele ya sheria kujibu tuhuma za wizi, kula njama za kuiba fedha za EPA, wakati mawaziri wawili wa zamani, Basil Mramba na Daniel Yona, pamoja na katibu mkuu wa wizara, Gray Mgonja wakifikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia vibaya ofisi na kuisababishia serikali hasara.

Mtu mmoja ameshtakiwa kwa tuhuma za kughushi nyaraka ili aifanikishe Kampuni ya Richmond kupata zabuni ya kufua umeme wa dharura.
 
Hata yeye anakaufisadi ndani yake. Si ndiyo mmoja kati ya mawaziri waliojiuzulu mwanzoni wakati wa mkapa kwa ajili ya ufisadi. Labda anaogopa faili lake lisije likafunguliwa.
 
Huyu alifanya ufisadi mkubwa sana alipokuwa waziri wa maliasili, aliuza mbuga kwa waarabu wakamhonga pamoja na vitu vingine saa ya mkononi!! Hao hao masheikh wakiarabu ndio walimuombea akarudishwa kwenye CABINET; hii ndio athari ya kuongoza nchi masikini, hata mawaziri wako wanapendekezwa na wale unaowatembezea bakuli!! Ngasongwa anaogopa kuwa nae pengine madhambi yake yatafufuliwa.
 
Huyo ni mtu smart maradufu, kujiuzuru kwake 96 muulizeni warioba na kurudi kwake barazani muulizeni mkapa na jk.
Tabia yake hiyo ndiyo inayomponza na kuundiwa fitina tele kwa wakuu wa nchi, chama chake.

Wengi wenu hamumfahamu- na zaidi siri ya maliasili waulizeni wenyewe maliasili- he was the first to stand aginst anti-porching na kuiwezesha hiyo unit kwa mwaka wake wa kwanza akiwa waziri.

Tafuteni data zake vizuri lakini muwaangalie na hao wanaomsakama wana nini juu yake?

Maoni yake yako very genuine na yenye kuasa kuhusu mustakabali wa nchi yetu.
 
Bwana Ngasongwa ,Waziri wa Zamani wa Mipango hapa hana hoja ya msingi.Kuna viongozi wanaofanya hujuma ya dhahiri, hujuma ambayo haina mwongozo kiserekali, kiitikadi au kitaalamu.
Hebu fikiria mtu anakuketea mvua ya kutengeneza kwa ajili ya kilimo na kutengeneza umeme-hiii ni kutukana kisomo na intelligence ya watanzania.
Mambo haya yapo, na kwa walio yafanya madudu haya mahali pa kufikishwa si pengine ila mahakamani tu ili mtu atetee uamuzi wake na kuona umuhimu wake katika maslahi ya ki-inchi
 
bwana ngasongwa ,waziri wa zamani wa mipango hapa hana hoja ya msingi.kuna viongozi wanaofanya hujuma ya dhahiri, hujuma ambayo haina mwongozo kiserekali, kiitikadi au kitaalamu.
Hebu fikiria mtu anakuketea mvua ya kutengeneza kwa ajili ya kilimo na kutengeneza umeme-hiii ni kutukana kisomo na intelligence ya watanzania.
Mambo haya yapo, na kwa walio yafanya madudu haya mahali pa kufikishwa si pengine ila mahakamani tu ili mtu atetee uamuzi wake na kuona umuhimu wake katika maslahi ya ki-inchi

kama umemsoma hapingani na pale ambapo kuna uzembe uliokusudiwa
 
Bwana Ngasongwa ,Waziri wa Zamani wa Mipango hapa hana hoja ya msingi.Kuna viongozi wanaofanya hujuma ya dhahiri, hujuma ambayo haina mwongozo kiserekali, kiitikadi au kitaalamu.
Hebu fikiria mtu anakuketea mvua ya kutengeneza kwa ajili ya kilimo na kutengeneza umeme-hiii ni kutukana kisomo na intelligence ya watanzania.
Mambo haya yapo, na kwa walio yafanya madudu haya mahali pa kufikishwa si pengine ila mahakamani tu ili mtu atetee uamuzi wake na kuona umuhimu wake katika maslahi ya ki-inchi

At least watu sasa wanaona kuwa Mvua za Lowassa zilikuwa ni ujinga tu, ni kitu ambacho hakihitajiki Tanzania. Na hata politiki za Mh Ngasongwa nazo hazihitajiki. Kama mtu ni safi na anafanya kazi kwa manufaa ya nchi hawezi kufukishwa mahakamani. Wanaofikishwa mahakamani ni mafisadi (so far ni wadogo wadogo) na wanatumia vibaya madaraka yao. Lakini siuo wanaofanya maamuzi kwa manufaa y nchi.
Ngasongwa anafahamu vizuri kuwa kuna loop holes nyingi za kutoa kisingizio cha kufanya kazi kwa manufaa ya nchi, lakini ukweli ni kwa manufaa ya watu fulani ndani ya serikali. Hilo sasa hivi limeanza kuwekwa wazi na yale mafaili ya wezi ambayo zamani yalikuwa yanafichwa sasa yameanza kusomwa na wezi wameanza kufahamika. Walio wezi ndio wanaostahili kutishika, sio walio safi.
 
Kumtetea Ngasongwa kunahitaji sana moyo kwa sababu zifuatazo;

1. Akiwa waziri wakati wa Mkapa waliuza kiwanda cha SPM -Mgololo kwa shilingi milioni moja ya kitaqnzania kwa mwekezaji anayejulikana kama Angel Hurts Industries ltd ambaye na yeye ni share holder akishirikiana na vigogo wengine wawili ambao ni Mkapa na Sumaye.
2. Alimwandikia barua waziri wa kazi ajira na vijana wa wakati huo Prof. Kapuya kuwa wafanyakazi na wananchi waliokuwa wanalalamika kuuzwa kwa kiwanda wasisikilizwe kwani yeye ameshamalizana nao .
3.Alimwandikia barua IGP mahita na kuomba polisi wa kwenda kulinda kiwanda cha SPM kwa muda wa miezi sita ili kuwahamimsha wananchi.

kwa wale mnaokumbuka hotuba ya Dr.Slaa bunge la bajeti waziri mkuu Pinda aliomba wapewe muda kujibu hoja hiyo sasa huenda ameshanusa kuwa mambo yanaanza kuwa magumu juu yake , fuatilieni hotuba bya Slaa japo haikumtaja mtu mojo kwa moja na mjue kinachoendelea.

Nimewamegea vya kutosha.
 
Kumtetea Ngasongwa kunahitaji sana moyo kwa sababu zifuatazo;

1. Akiwa waziri wakati wa Mkapa waliuza kiwanda cha SPM -Mgololo kwa shilingi milioni moja ya kitaqnzania kwa mwekezaji anayejulikana kama Angel Hurts Industries ltd ambaye na yeye ni share holder akishirikiana na vigogo wengine wawili ambao ni Mkapa na Sumaye.
2. Alimwandikia barua waziri wa kazi ajira na vijana wa wakati huo Prof. Kapuya kuwa wafanyakazi na wananchi waliokuwa wanalalamika kuuzwa kwa kiwanda wasisikilizwe kwani yeye ameshamalizana nao .
3.Alimwandikia barua IGP mahita na kuomba polisi wa kwenda kulinda kiwanda cha SPM kwa muda wa miezi sita ili kuwahamimsha wananchi.

kwa wale mnaokumbuka hotuba ya Dr.Slaa bunge la bajeti waziri mkuu Pinda aliomba wapewe muda kujibu hoja hiyo sasa huenda ameshanusa kuwa mambo yanaanza kuwa magumu juu yake , fuatilieni hotuba bya Slaa japo haikumtaja mtu mojo kwa moja na mjue kinachoendelea.

Nimewamegea vya kutosha.

Mzee si utuwekee hiyo hotuba ya Slaa hapa!!!!
 
"Pengine angepata nafasi, angesahihisha," alisema waziri huyo wa zamani. Dk Ngasongwa, ambaye ni mbunge wa Ulanga Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisisitiza kuwa ni muhimu suala hilo likaangaliwa vizuri na kwa umakini zaidi.

- Ngasongwa asidanganye hapa, we are smarter than this nonesense zake, hakuna asiyejua kua ni innocent until proven guilty, hatuwezi kuacha ku-excute sheria zetu za jamhuri kwa visingizio uchwara kama hivi vyake,

- If that is the case then tuwape break wafunwga wote, maana huenda walipitiwa na wanaweza au wangeweza kujisahihisha bila kufika kwenye sheria, ni aibu hata kuamini haya yanasemwa na former minister wa jamhuri no wonder taifa hili lipo hapa, wewe kiongozi wa zamani hukuiba sasa tatizo lako lipo wapi? Sisi tunatafuta wezi tu! na wanafahamika tayari.
 
- Ngasongwa asidanganye hapa, we are smarter than this nonesense zake, hakuna asiyejua kua ni innocent until proven guilty, hatuwezi kuacha ku-excute sheria zetu za jamhuri kwa visingizio uchwara kama hivi vyake,

- If that is the case then tuwape break wafunwga wote, maana huenda walipitiwa na wanaweza au wangeweza kujisahihisha bila kufika kwenye sheria, ni aibu hata kuamini haya yanasemwa na former minister wa jamhuri no wonder taifa hili lipo hapa, wewe kiongozi wa zamani hukuiba sasa tatizo lako lipo wapi? Sisi tunatafuta wezi tu! na wanafahamika tayari.


Mkuu hawa wazee wengine wanadhani ule ujinga wa kutoa statement za uongo kwa umma kupitia kwenye vyombo va habari, bila kuwa questioned bado unaendelea. Anataka mtu afanye wizi wizara ya Utalii halafu apelekwe akajisahihishe wizara ya Madini. Nadhani anatupa mfano wa Mh Mramba, amefanya ujanja wizara ya fedha halafu amepewa nafasi ajirekebishe wizara ya madini, matokeo yake tunayaona. Sijui bado anadhani sisi watanzania bado ni wajinga kama siku zile??? Mzee Kingunge aliitisha press conference na kusema kina Slaa waongo, akidhani kuwa uongo aliokuwa akiusema huko nyuma utakubalika na leo, matokeo yake amekumbwa a aibu ajabu. Ngasongwa anaelekea huko huko, anataka kutafuta cheap excuse ya kuwalinda mafisadi. This time around it will not work, lazima waanikwe tu.
 
- Mkuu Bongolander, ninasema hivi hawa viongozi wetu wamekua na kasumba ya kuamini kuwa wako juu ya sheria kwa sababu haingii akilini kabisa viongozi wetu wanakuja juu na maneno mengi ya wasi wasi na sheria kuchukua mkondo wake.

- Huyu Ngasongwa, anashangaa kuona mawaziri wa zamani wanaenda kwenye mkono wa sheria, maana amezoea kuona sheria inashika wanyonge tu na masikini walalahoi, lakini sio viongozi kama yeye, na anasema wazi bila hata ya aibu na waandishi nao hakuna mwenye ubavu wa kumuuliza.

- Ndio maana taifa letu tumekwama, wenzetu huko US mpaka rais Nixon amewahi kulazimishwa kujiuzulu kukimbia sheria, Clinton naye el-manusura lakini hata hivyo akalipa faini na kunyang'anywa leseni ya sheria, sisi ndio kwanza waziri anashangaa kuona sheria sasa inagusa viongozi tena mawaziri tu bado hatujafika kwa wa juu zaidi!

Kwa kweli hili taifa tuna safari ndefu sana mbele yetu!, ingawa tutafika tu!
 
Date::1/19/2009
Ngasongwa: Inatia hofu mawaziri kushtakiwa
Exuper Kachenje
Mwananchi​

WAZIRI wa zamani wa Mipango, Uchumi na Uwekezaji katika utawala wa awamu ya tatu, Dk Juma Ngasongwa amesema hatua ya serikali kuwafikisha mahakamani viongozi waandamizi wa serikali, wakiwemo mawaziri kwa makosa waliyofanya wakiwa madarakani, inatia hofu. ................Dk Ngasongwa alisema: "Ukimshtaki mtu kwa maamuzi aliyoyafanya akiwa madarakani, ukweli inatia mashaka. Inatakiwa kuwa makini kidogo katika kulitazama suala hilo. Pale serikalini kuna mambo mtu anaweza kuamua si kwa sababu alifikiria kufanya ufisadi. " ............................
"Pengine angepata nafasi, angesahihisha," alisema waziri huyo wa zamani. .................

Ngasongwa.......what you are saying is......BULL SHIT!!
 
Back
Top Bottom