Ney wa Mitego atoboa na hit song yake kwenye wakati mgumu wa kiki za kisiasa (Free Nation)

KESI YA UCHOCHEZI YA NEY WA MITEGO NA WIMBO WAKE MPYA WAPO

NA
,Mdude nyagali

WAKILI; unasema wewe ni afisa wa polisi ney wa mitego alifanya uchochezi kwenye nyimbo yake na baadhi ya maneno yaliyopo kwenye hati ya mashtaka yameandikwa kichaa kapewa rungu hebu iambie mahakama kichaa aliyemsema ney ni yupi?

SHAHIDI PC;;kichaa aliyemsema ney ni mtukufu

WAKILI;;ifafanulie vizuri mahakama wewe ulijuaje kama kichaa aliyeimbwa na ney ni mtukufu?

SHAHIDI PC.;mimi nilihisi kuwa atakuwa mtukufu kwa kuwa ney ni timu ukawa;

WAKILI;;shahidi hivi unafahamu kuwa ushahidi wa kuhisi na kupiga ramli mahakamani haupo kwa kuwa sio kwa mganga wa kienyeji na haupo kwenye sheria yoyote?

SHAHIDI PC;;ndiyo

WAKILI;;Sasa ebu iambie mahakama bila kuhisi huyu kichaa kapewa rungu aliyemuimba ney ulijuaje ni mtukufu?

SHAHIDI PC;;kimya

WAKILI;kuna maneno mengine unayakumbuka ambayo ni ya kichochezi na yapo kwenye wimbo wa ney?

SHAHIDI PC;ndiyo
WAKILI;;unaweza kuyataja?
SHAHIDI PC;;1,kuna watu hawana malinda,,2.daudi bashite kavoji vyeti,,,3.hutaki ushauri unajifanya ndugu yake yesu

WAKILI;kwa hiyo watu kutokuwa na malinda ni uchochezi?
SHAHIDI PC;ndiyo
WAKILI;ebu iambie mahakama nini maana ya kutokuwa na malinda?

SHAHIDI PC;;kimya

WAKILI ;;jibu mheshimiwa HAKIMU anasubili a note jibu lako

SHAHIDI;;sijui ila nilisikia bungeni mbunge wa mbeya mjini mheshimiwa mbilinyi akiongea kuwa gavana akaguliwe malinda.

WAKILI ;je wewe una hiyo malinda?
SHAHIDI PC;sina na siijui

WAKILI;;Kwa upelezi wako kama afisa wa polisi ulijua ney wa mitego anamsema nani ambaye hana malinda?

SHAHIDI PC;katika kufanya upelelezi tukishilikiana na ofisi ya OCCID na ofisi ya RCO tuligundua ney alikuwa anamsema gavana wa mkoa wetu kuwa ndiye hana malinda

WAKILI;wewe ulijuaje kama ney anamsema gavana huenda alikuwa anakusema wewe na wewe si umesema hapa na mahakama ime note kuwa huna malinda?

SHAHIDI PC;hapana sio mimi ni gavana

WAKILI;;;Kwani kuna mstari wowote wa huo wimbo gavana ametajwa?

SHAHIDI PC;;hapana ila ametajwa kwa jina la daudi bashite;

WAKILI;;;kwani gavana alishawahi kusibitisha popote au kanisani ama kiapo cha mahakama kuwa jina la daudi bashite ni lake?

SHAHIDI PC;;sijui ila naona kwenye mitandao watu wanamuita hivyo.

WAKILI;;huko kwenye mitandao ni akina nani wanamuita hivyo?

SHAHIDI PC;akina Mdude Chadema Nyagali, Malisa GJ, Daniel Ezekiel Daniel Kumbusho Dawson Kagine Michael Mwaikenda Boniface Mwabukusi Yericko Nyerere Bob Chacha Wangwe Boniface Jacob Julius S. Mtatiro mange kimambi Tanzagiza Hilda Newton Chadema Karama Kaila na wengine wengi

WAKILI;;je unaweza kumleta gavana ili aje aisibitishie mahakama kuwa yeye ndiye bashite halafu ndio tuendelee na tafsiri ya neno malinda?

SHAHIDI PC.;itakuwa ngumu mheshimiwa kumleta gavana.

WAKILI;;unafahabu kwa mujibu wa sheria usipo mleta gavana kuthibitisha kuwa yeye ndiye daudi bashite ushahidi wako kuhusiana na malinda unakosa uhalali mbele ya mahakama tukufu?

SHAHIDI PC;kimyaaa

WAKILI;unafahamu kuwa kwa mujibu wa katiba serikali yetu haina dini ila wananchi wake ndio wana dini?

SHAHIDI PC;;ndiyo

WAKILI;;unakubaliana na mimi kuwa kwa mwongozo huo wa katiba ili uwe na undugu na yesu ni lazima uwe myahudi au muisrael?

SHAHIDI;;Ndiyo

WAKILI ;;sasa haya maneno unayosema ni ya uchochezi kwenye wimbo wake kuwa hashauliki ana undugu na yesu ulijua ney anamsema ni nani?

SHAHIDI;;ney alikuwa anamsema ni mtukufu kwa kuwa wapinzani hulalamika kuwa mtukufu hashauriki.

WAKILI;;kwani mtukufu ni muyahudi?au ana vitambulisho vyovyote vinavyoonyesha ni muisrael ama viashilia vinavyoonyesha ana undugu na yesu?

SHAHIDI;;kimyaaa

NINGEKUWA WAKILI MIMI MDUDE HAKIKA KESI YA NEY NINGEJITOLEA KUISIMAMIA BURE.

Mdude nyagali
sumu ya nyigu
 
Verse 1:
Unachokipanda leo ndicho
utachovuna kesho.
Imeandikwa Mwanaume kula kwa
jasho.
Najiuliza hivi ni nani kaiona
kesho.
Chapa mwendo na ukilala hauna
chako.
Hivi uhuru wa kuongea kwenye hii
nchi bado upo?.
Usije kuongea vitu kesho ukajikuta
sentro.
Chorus:
Kuna viongozi wavuta bangi?
"wapo "
Maana wana maamuzi ya kise....
"wapo"
Kuna walio mmiss Jakaya? "wapo"
Walio choka kuisoma namba?
"wapo"
Kuna walio poteza malinda?
"wapo"
Kuna wasanii mateja? "wapo"
Kuna mademu wanasagana?
"wapo"
Kuna vidume wanalelewa? "wapo"
Kuna wasanii wanarogana? "wapo"
Verse 2
Kuna Radio na Tv, naona
zimeshapoteza CV.
Hakuna uhuru wa habari, wala
taarifa ya habari.
Wanapindisha pindisha tu
kuiogopa serikali.
Siamini nchi inaendeshwa na kiki.
Siasa inafunika mziki.
Viongozi wanashindana kukiki.
Wanagombea front page, wauze
kwenye gazeti.
Nasikia kuna viongozi wamefoji
vyeti.
Verse 3
Kiongozi mwenye busara
anapokea ushauri.
Anapokea mawazo,haweki mbele
kiburi.
Hey! Samahani mheshimiwa, hivi
unamjua BASHITE?.
hili ni jipu jipya toka koromije.
Limesha iva na usaa,
limeshatunga.
Na kukabidhi sindano ya
kulidunga.
Daktari haogopi ukubwa wa
kidonda.
We_si Dr wa majipu, tumbua
hakuna kuvunga.
Kuvamia ofisi za watu kumbe nayo
ni kazi.
Hakuna noma wanangu pigeni
kazi.
Boda boda kazi, bajaji Kazi.
Eti! Vipi? Kukaba nayo kazi?.
Refa ni wao piga manati.
Vita ya Masai na mmang'ati.
Biashara ya ngono na Super
shafti.
Pumzi imekata nashika shati...
Hahahahahaha! Wewe mtu gani
sasa......
Hutaki kushauriwa, hutaki
kukosolewa......
Umerongwa wewe,........
unajiona ndugu yake na Yesu
ee....
Oya! Wanangu eeeh! Round hii
mtanyooka haki ya Mungu.
Naona kichaa kapewa Rungu..
MWISHO:
 
Kisheria hapana kesi hapo,umekaa kimaadili zaidi sio kisheria...serkali ingeacha tu BASATA WATOE TAMKO BASI.
 
Style alotumia Mkuu Wa nchi ime workout,niliwahi kusema serikali kuna mambo Mengi huwa ni hofu tu,kukataza jambo kwa nguvu kubwa ni kuliongezea umaarufu kwa nguvu kubwa,mfano mzuri ile habari yetu ya hapa Dar ilio trend karibu miezi miwili sasa kama ingechukuliwa easy ingekua easy hivyohivyo na yangeisha mapema
Hongera Mh Rais watu wachape kazi tuendelee mbele.
 
Unachokipanda leo ndicho utachovuna kesho.

Imeandikwa Mwanaume kula kwa jasho.

Najiuliza hivi ni nani kaiona kesho.

Chapa mwendo na ukilala hauna chako.

Hivi uhuru wa kuongea kwenye hii nchi bado upo?.

Usije kuongea vitu kesho ukajikuta sentro.



Kuna viongozi wavuta bangi? "wapo "

Maana wana maamuzi ya kise.... "wapo"

Kuna walio mmiss Jakaya? "wapo"

Walio choka kuisoma namba? "wapo"

Kuna walio poteza malinda? "wapo"

Kuna wasanii mateja? "wapo"

Kuna mademu wanasagana? "wapo"

Kuna vidume wanalelewa? "wapo"

Kuna wasanii wanarogana? "wapo"




Kuna Radio na Tv, naona zimeshapoteza CV.

Hakuna uhuru wa habari, wala taarifa ya habari.

Wanapindisha pindisha tu kuiogopa serikali.

Siamini nchi inaendeshwa na kiki.

Siasa inafunika mziki.

Viongozi wanashindana kukiki.

Wanagombea front page, wauze kwenye gazeti.

Nasikia kuna viongozi wamefoji vyeti.




Kuna viongozi wavuta bangi? "wapo "

Maana wana maamuzi ya kise.... "wapo"

Kuna walio mmiss Jakaya? "wapo"

Walio choka kuisoma namba? "wapo"

Kuna walio poteza malinda? "wapo"

Kuna wasanii mateja? "wapo"

Kuna mademu wanasagana? "wapo"

Kuna vidume wanalelewa? "wapo"

Kuna wasanii wanarogana? "wapo"


Kiongozi mwenye busara anapokea ushauri.

Anapokea mawazo,haweki mbele kiburi.

Hey! Samahani mheshimiwa, hivi unamjua BASHITE?.

hili ni jipu jipya toka koromije.

Limesha iva na usaa, limeshatunga.

Na kukabidhi sindano ya kulidunga.

Daktari haogopi ukubwa wa kidonda.

We_si Dr wa majipu, tumbua hakuna kuvunga.

Kuvamia ofisi za watu kumbe nayo ni kazi.

Hakuna noma wanangu pigeni kazi.

Boda boda kazi, bajaji Kazi.

Eti! Vipi? Kukaba nayo kazi?.

Refa ni wao piga manati.

Vita ya Masai na mmang'ati.

Biashara ya ngono na Super shafti.

Pumzi imekata nashika shati...


Hahahahahaha! Wewe mtu gani sasa......

Hutaki kushauriwa, hutaki kukosolewa......

Umerongwa wewe,........

unajiona ndugu yake na Yesu ee....

Oya! Wanangu eeeh! Round hii mtanyooka haki ya Mungu.

Naona kichaa kapewa rungu!
 
Back
Top Bottom