News Alert: Waziri wa Awamu ya Nne Tapeli!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Waziri Maua Daftari atiwa hatiani kwa utapeli

na Irene Mark, Dodoma (tanzania daima)


MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, imemtia hatiani Naibu Waziri wa Miundombinu, Dk. Maua Daftari kwa kosa la utapeli na kumwamuru kulipa sh milioni 100.7.

Uamuzi huo ulitolewa jana na aliyekuwa Jaji wa mahakama hiyo, ambaye sasa ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Laurean Kalegeya na kumtaka Naibu Waziri huyo kumlipa fedha hizo, Fatma Salmin ambaye alikuwa mlalamikaji katika kesi hiyo ya madai.

Naibu Waziri huyo alifikishwa mahakamani hapo mwaka 1999 kwa kesi ya madai ya kujipatia fedha kwa nja ya udanganyifu kutoka kwa Fatma.

Katika madai hayo, ilielezwa kuwa Naibu Waziri huyo alishindwa kulipa sh milioni 39.5 kwa ajili ya malipo ya shamba lenye thamani ya sh milioni 40 alilouziwa eneo la Kibaha, mkoani Pwani.

Aidha, mlalamikaji huyo alidai kumuuzia Dk. Daftari mtambo wa kusindika matunda wenye thamani ya sh milioni 100.

Hata hivyo, madai ya mlalamikaji ni kulipwa sh milioni 400 alizotapeliwa na Naibu Waziri huyo aliyedai kuwa rafiki yake waliokuwa wakishirikiana katika biashara mbalimbali.

Akizungumzia hukumu hiyo, Naibu Waziri, alisema hakubaliani na uamuzi huo, hivyo amemwagiza wakili wake, Peter Swai kukata rufaa haraka.

Alisema hana imani na mazingira ya usomwaji wa hukumu hiyo kutokana na ukweli kuwa wakili wake hakupelekewa taarifa mapema.

“Sina imani na mazingira ya hukumu hiyo na sina imani nayo hata kidogo kwa sababu wakili wangu amepewa taarifa za hukumu muda mfupi kabla ya kusomwa, tena kwa njia ya ujumbe kwenye simu yake ya mkononi na karani wa mahakama.

“Baada ya hukumu hiyo ilinayonitaka mimi kumlipa Fatma sh milioni 100 nimemwamuru wakili wangu kukata rufaa mara moja... naamini huko haki itapatikana, lakini sikubaliani na hukumu hiyo kabisa,” alisema Dk. Daftari.

Aidha, alisisitiza kuwa hajawahi kumkopa wala kufanya biashara na mdai, hivyo haoni sababu ya mahakama kumtia hatiani. Hivyo anapigania haki yake na atafanya hivyo hadi atakapokata kauli.

“Nilisema mahakamani kuwa sijawahi kumkopa mdai hata siku moja, nimekata rufaa kuhakikisha napigania haki yangu hadi nitakapokata kauli... sidaiwi wala sijawahi kumkopa yule mama,” alisisitiza.
 
Waziri Maua Daftari atiwa hatiani kwa utapeli

na Irene Mark, Dodoma (tanzania daima)


MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, imemtia hatiani Naibu Waziri wa Miundombinu, Dk. Maua Daftari kwa kosa la utapeli na kumwamuru kulipa sh milioni 100.7.

Uamuzi huo ulitolewa jana na aliyekuwa Jaji wa mahakama hiyo, ambaye sasa ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Laurean Kalegeya na kumtaka Naibu Waziri huyo kumlipa fedha hizo, Fatma Salmin ambaye alikuwa mlalamikaji katika kesi hiyo ya madai.

Naibu Waziri huyo alifikishwa mahakamani hapo mwaka 1999 kwa kesi ya madai ya kujipatia fedha kwa nja ya udanganyifu kutoka kwa Fatma.

Katika madai hayo, ilielezwa kuwa Naibu Waziri huyo alishindwa kulipa sh milioni 39.5 kwa ajili ya malipo ya shamba lenye thamani ya sh milioni 40 alilouziwa eneo la Kibaha, mkoani Pwani.

Aidha, mlalamikaji huyo alidai kumuuzia Dk. Daftari mtambo wa kusindika matunda wenye thamani ya sh milioni 100.

Hata hivyo, madai ya mlalamikaji ni kulipwa sh milioni 400 alizotapeliwa na Naibu Waziri huyo aliyedai kuwa rafiki yake waliokuwa wakishirikiana katika biashara mbalimbali.

Akizungumzia hukumu hiyo, Naibu Waziri, alisema hakubaliani na uamuzi huo, hivyo amemwagiza wakili wake, Peter Swai kukata rufaa haraka.

Alisema hana imani na mazingira ya usomwaji wa hukumu hiyo kutokana na ukweli kuwa wakili wake hakupelekewa taarifa mapema.

“Sina imani na mazingira ya hukumu hiyo na sina imani nayo hata kidogo kwa sababu wakili wangu amepewa taarifa za hukumu muda mfupi kabla ya kusomwa, tena kwa njia ya ujumbe kwenye simu yake ya mkononi na karani wa mahakama.

“Baada ya hukumu hiyo ilinayonitaka mimi kumlipa Fatma sh milioni 100 nimemwamuru wakili wangu kukata rufaa mara moja... naamini huko haki itapatikana, lakini sikubaliani na hukumu hiyo kabisa,” alisema Dk. Daftari.

Aidha, alisisitiza kuwa hajawahi kumkopa wala kufanya biashara na mdai, hivyo haoni sababu ya mahakama kumtia hatiani. Hivyo anapigania haki yake na atafanya hivyo hadi atakapokata kauli.

“Nilisema mahakamani kuwa sijawahi kumkopa mdai hata siku moja, nimekata rufaa kuhakikisha napigania haki yangu hadi nitakapokata kauli... sidaiwi wala sijawahi kumkopa yule mama,” alisisitiza.

hii iwe fundisho kwa vigogo wote dhulumati, kwa muonekano inadhihirisha kuwa yeye na wakili wake likuwa wanapuuzia wito wa mahakama ndiyo maana hukumu imetolewa kwa upande mmoja. Kuna daawa ningi mahakamani ambazo vigogo wamehusika kuwapora raia mali zao na hasa huko zenjibar.

Na huyo wakili anayepokea amri awe amepitia jeshini basi maana huwezi kumuamuru raia tena anayejua haki zake..... kwikwikwi
 
Mahakama zetu kama zitakuwa zinatoa hukumu bila kuogopa cheo na jina la mtu zitajiongezea heshima na kuaminika mbele ya jamii, na hili ni jambo jema.
Tunaamini mahakama huru ikisema "wewe mwizi" basi ndio hivyo tena,mwizi. Mhe.Maua kaambiwa katapeli (Tapeli) ndio hivyo tena kawa tapeli. Sidhani kama anastahili kuendelea kuongoza chombo cha Umma ikiwa tayari haaminiki kwa Utapelialiohukumiwa nao.
 
Ila bkesi ya tangu 1999 hadi 2007 du, ndo maana sipendi mambo ya mahakama mie.
 
Ati hana imani na mazingira ya hukumu hiyo na hana imani nayo hata kidogo.

Leo hii ndio amegundua kwamba mahakama za nchi hii zinaendeshwa vibaya au alifikiri kwa vile yeye ni mmoja wa wenye nchi hii asingepatikana na makosa tena bila ya kuhudhuria mahakamani.

These people should style up, hawa wana nafasi kubwa sana kuweza kubadilisha mfumo wa mahakama nchi hii if only they did thier work nothing else.

And I will not be surprised kabisa kama huyu mwanamama alitapeli kweli na labda hata kujigamba atafanywa nini, matumizi mabavu ya madaraka.
 
Labda utapeli...
Mimi nafikiri huyo Waziri kazidiwa kete na huyo mama Salmin, kwani kwa jinsi mama huyo alivyomchota taratibu na vijizawadi vya hereni na vibangiri vya dhahabu na baada ya kumuona kuwa waziri ana tammaa ndipo akamutengenezea zigo analohangaika nalo, nakumbuka enzi zao Bi Maua alikuwa halali Dar bali Mlandizi kwa mama yule na watu tulitegemea mtego utanasa tu, sasa TAYARI KAISHA. ila tumhurumie jamani kwani kwa mama yule kama humjui hata sie tungeumia tu,
 
Mimi nafikiri huyo Waziri kazidiwa kete na huyo mama Salmin, kwani kwa jinsi mama huyo alivyomchota taratibu na vijizawadi vya hereni na vibangiri vya dhahabu na baada ya kumuona kuwa waziri ana tammaa ndipo akamutengenezea zigo analohangaika nalo, nakumbuka enzi zao Bi Maua alikuwa halali Dar bali Mlandizi kwa mama yule na watu tulitegemea mtego utanasa tu, sasa TAYARI KAISHA. ila tumhurumie jamani kwani kwa mama yule kama humjui hata sie tungeumia tu,

Kite,
Siye kweli hatujui ebu mwaga ze dataz tujue undani wake!
 
hapo hata riba hakuna,1999 dola moja ilikuwa sawa na shiling mia tano,leo hii baada ya hukumu dola moja ni sawa na tshs 1200.mahakama haikumtendea haki mlalamikaji
 
Yawezekana Waziri walionyesha mkono wa Birika kwa Hakimu- au hakimu alikataa kupotea chochote!

Hii ni hukumu- inatufundisha kuwa haki inawezekana tu tz kama tuna nia njema!
 
Huko CCM kuna nini ? Maua ni mwana mtandao huyu Jaji asije jikuta akiwa na hali ngumu maana CCM bwana !!!!
 
Aidha, alisisitiza kuwa hajawahi kumkopa wala kufanya biashara na mdai, hivyo haoni sababu ya mahakama kumtia hatiani. Hivyo anapigania haki yake na atafanya hivyo hadi atakapokata kauli.

Mashitaka hayakuwa ya kukopa au kufanya biashara bali kununua shamba. Haya ndiyo majibu ya naibu waziri, hivi kweli alisoma hayo mashitaka na judgement iliyotolewa? Ama kweli kazi ipo.

BTW hivi kutokana na judgement hii kazi bado anayo?
 
Kwa mujibu wa mahakama, Dr Maua ndie mkosa, kwa hiyo ameamuriwa kumlipa mlalamikaji hela yake. Naye Dr Maua anadai atakata rufaa, yaani ataka kutushawishi kwamba yeye si mkosa. Kama akikata rufaa kweli, tutaendelea kudhani mkosa hajulikani hadi hapo rufaa itakapoamuliwa. Lakini kuna uhakika kuwa kati ya wawili hao mkosa yupo, ama kwa kutapeli au kwa kusingizia mwenzie utapeli. Lakini jamani kama kesi ya 1999 inaamuliwa 2007 (baada ya miaka 8), na bado sijui hiyo rufaa itachukua muda gani, kuna haki kweli hapa? Mbona ni masikhara tu? Nani atayefidia hasara ya yule asiye mkosa? Sasa kama mambo ni haya, tunashangaa nini watu wanapochukua sheria mikononi na kuamua sijui kulogana au chochote wanachojua? Inauma sana!
 
She need to shut-up, and pay the money... I wanna see if they will go after her house, and auction everything she have. I said once, the power of suing is amazing.
 
hivi kimaadili huyu waziri kweli anatakiwa kuwepo kwenye nafasi aliyonayo sasa,au ndio bongo kila kitu kwetu ni sawa tu hata kuongozwa na watu wasio waaminifu.
 
Katibu Tarafa, najaribu kuona kama ni kosa la Madai (civil suit) sidhani inamuondoa madarakani; kama ni conviction ya kosa la jinai angejiondoa mara moja.
 
Back
Top Bottom