Boniphace Kichonge
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 1,606
- 1,956
NOVEMBA 6 , 2019
Serikali imesema matumizi ya dawa za kulevya aina ya bangi bado ni tatizo nchini, huku yakishika kasi katika mikoa ya Mara, Tanga, Morogoro, Arusha, Kagera na Ruvuma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, akitoa taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka jana, alisema katika kipindi hicho vyombo vya dola kwa kushirikiana na wananchi walikamata tani 24.3 za bangi na watuhumiwa 10,061.
“Dawa za kulevya aina ya mirungi nayo imeendelea kutumiwa na watu wa rika mbalimbali hapa nchini, kwamba kwa mwaka 2018 vyombo vya dola vilifanikiwa kukamata tani 8.97 za mirungi zikiwahusisha watuhumiwa 1,186,” alisema.
Alisema katika kipindi cha mwaka jana, kesi 7,592 zikiwa na watuhumiwa 10,979 zilifunguliwa katika mahakama mbalimbali nchini, huku kesi 7,174 zilizowahusisha watuhumiwa 11,045 ziliendelea kusikilizwa.
Serikali imesema matumizi ya dawa za kulevya aina ya bangi bado ni tatizo nchini, huku yakishika kasi katika mikoa ya Mara, Tanga, Morogoro, Arusha, Kagera na Ruvuma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, akitoa taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka jana, alisema katika kipindi hicho vyombo vya dola kwa kushirikiana na wananchi walikamata tani 24.3 za bangi na watuhumiwa 10,061.
“Dawa za kulevya aina ya mirungi nayo imeendelea kutumiwa na watu wa rika mbalimbali hapa nchini, kwamba kwa mwaka 2018 vyombo vya dola vilifanikiwa kukamata tani 8.97 za mirungi zikiwahusisha watuhumiwa 1,186,” alisema.
Alisema katika kipindi cha mwaka jana, kesi 7,592 zikiwa na watuhumiwa 10,979 zilifunguliwa katika mahakama mbalimbali nchini, huku kesi 7,174 zilizowahusisha watuhumiwa 11,045 ziliendelea kusikilizwa.