News alert:Mgombea urais NCCR- Mageuzi Azomewa

TandaleOne

JF-Expert Member
Sep 4, 2010
1,644
709
Send to a friend Friday, 15 October 2010 07:40 0diggsdigg

Patricia Kimelemeta, Kigoma
MGOMBEA urais kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi, Hashimu Rungwe jana alipata wakati mgumu baada ya wananchi wa kijiji cha Nguruka kilichopo nje kidogo wa Mji wa Kigoma kumwambia wazi kuwa hawamhitaji, bali wanamtaka David Kafulila kuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini.

Hatua hiyo imekuja baada ya mshereheshaji wa kampeni hiyo kumpa nafasi ya kuzungumza na wananchi kwenye kiwanja cha shule ya msingi Nguruka, mara baada ya Rungwe kuinuka, wananchi hao walianza kuondoka huku wakisema wao wamekuja kumsikiliza Kafulila na si mgombea mwingine wa chama chochote.

"Haaa, huyu, hapana, hatuwezi kumpa, bora angekuwa Mbatia, lakini sio huyu, hapana," zilisikika sauti za wananchi hao huku mmoja aliyezungumza na waandishi wa habari na kujitambulisha kwa jina la Faraj(37) alisema kuwa, mgombea huyo hajawahi kufika kwenye vijiji hivyo, jambo ambalo limewafanya wananchi hao kuguna.

"Hatuwezi kumpa kura zetu huyu, bora angekuwa James Mbatia lakini sio huyu, hatujawahi kumuona hata siku moja, kama ni hivyo bora tumpe mgombea mwingine wa urais lakini sio huyu, hatumjui ila za ubunge tutampa Kafulila," alisema Faraji.

Kwa mujibu wa Faraji, walidhani anayewania nafasi hiyo ni mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia badala yake amekuja mtu mwingine asiyejua matatizo yao.

Naye mwananchi mwingine wa kijiji hicho, Ramadhan Rajab (54), alisema kuwa nafasi ya urais inamtaka mtu ‘smati’ ambaye anaweza kuzungumza na wadau mbalimbali katika kutetea maslahi ya wananchi, hivyo basi kitendo cha kumpa Rungwe nafasi hiyo wakati anafuga ndevu kinaweza kuwafundisha tabia mbaya.

"Huku kwetu usafi ni kitu muhimu, hatuwezi kuruhusu mtu kufuga ndevu ndefu kiasi hiki na anashindwa kuzitunza, huu ni uchafu, hatuwezi kumpa,"alifafanua.

Hata hivyo, Rungwe alijaribu kuwasihi wananchi hao wamsikilize huku akisema kuwa, serikali iliyopo madarakani inapaswa kupumzishwa.

"Naomba mnisikilize ndugu zangu, tulieni kwanza niwaambie kitu nataka tuwapumzishe hawa manyang'au, hawafai,"alisema Rungwe.

Alisema, serikali ya awamu ya nne ya chama tawala kimeshindwa kusikiza kero za wananchi, badala yake wamekaa madarakani kwa ajili ya maslahi yao binafsi.

Alisema, kutokana na hali hiyo wananchi wana haki ya kuwanyima kura kwenye kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Wakati huo huo Rungwe amepata wakati mgumu kufanya kampeni kwenye maeneo mengine ya Jimbo la Kigoma baada ya kukosa usafiri na kulazimika wakati fulani kutumia daladala.

Rungwe ambaye alifika mkoani Kigoma Oktoba saba mwaka huu, baada ya kuachwa na ndege zaidi ya siku mbili, alikodi gari ndogo ya kubeba abiria aina ya teksi ambayo aliitumia maeneo ya mjini Kigoma huku akishindwa kwenda vijiji vilivyo nje ya mkoa.

Tatizo hilo la usafiri kwa mgombea huyo lilingia katika hatua nyingine pale alipochukua gari la mgombea ubunge na kulazimisha gari hilo kulitumia kwenye mikutano yake na kuwatelekeza waandishi wa habari waliokuwa wakitumia gari hiyo kwenye msafara huo.
Chanzo:Mwananchi
 
Send to a friend Friday, 15 October 2010 07:40 0diggsdigg

Patricia Kimelemeta, Kigoma
MGOMBEA urais kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi, Hashimu Rungwe jana alipata wakati mgumu baada ya wananchi wa kijiji cha Nguruka kilichopo nje kidogo wa Mji wa Kigoma kumwambia wazi kuwa hawamhitaji, bali wanamtaka David Kafulila kuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini.

Hatua hiyo imekuja baada ya mshereheshaji wa kampeni hiyo kumpa nafasi ya kuzungumza na wananchi kwenye kiwanja cha shule ya msingi Nguruka, mara baada ya Rungwe kuinuka, wananchi hao walianza kuondoka huku wakisema wao wamekuja kumsikiliza Kafulila na si mgombea mwingine wa chama chochote.

"Haaa, huyu, hapana, hatuwezi kumpa, bora angekuwa Mbatia, lakini sio huyu, hapana," zilisikika sauti za wananchi hao huku mmoja aliyezungumza na waandishi wa habari na kujitambulisha kwa jina la Faraj(37) alisema kuwa, mgombea huyo hajawahi kufika kwenye vijiji hivyo, jambo ambalo limewafanya wananchi hao kuguna.

"Hatuwezi kumpa kura zetu huyu, bora angekuwa James Mbatia lakini sio huyu, hatujawahi kumuona hata siku moja, kama ni hivyo bora tumpe mgombea mwingine wa urais lakini sio huyu, hatumjui ila za ubunge tutampa Kafulila," alisema Faraji.

Kwa mujibu wa Faraji, walidhani anayewania nafasi hiyo ni mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia badala yake amekuja mtu mwingine asiyejua matatizo yao.

Naye mwananchi mwingine wa kijiji hicho, Ramadhan Rajab (54), alisema kuwa nafasi ya urais inamtaka mtu ‘smati' ambaye anaweza kuzungumza na wadau mbalimbali katika kutetea maslahi ya wananchi, hivyo basi kitendo cha kumpa Rungwe nafasi hiyo wakati anafuga ndevu kinaweza kuwafundisha tabia mbaya.

"Huku kwetu usafi ni kitu muhimu, hatuwezi kuruhusu mtu kufuga ndevu ndefu kiasi hiki na anashindwa kuzitunza, huu ni uchafu, hatuwezi kumpa,"alifafanua.

Hata hivyo, Rungwe alijaribu kuwasihi wananchi hao wamsikilize huku akisema kuwa, serikali iliyopo madarakani inapaswa kupumzishwa.

"Naomba mnisikilize ndugu zangu, tulieni kwanza niwaambie kitu nataka tuwapumzishe hawa manyang'au, hawafai,"alisema Rungwe.

Alisema, serikali ya awamu ya nne ya chama tawala kimeshindwa kusikiza kero za wananchi, badala yake wamekaa madarakani kwa ajili ya maslahi yao binafsi.

Alisema, kutokana na hali hiyo wananchi wana haki ya kuwanyima kura kwenye kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Wakati huo huo Rungwe amepata wakati mgumu kufanya kampeni kwenye maeneo mengine ya Jimbo la Kigoma baada ya kukosa usafiri na kulazimika wakati fulani kutumia daladala.

Rungwe ambaye alifika mkoani Kigoma Oktoba saba mwaka huu, baada ya kuachwa na ndege zaidi ya siku mbili, alikodi gari ndogo ya kubeba abiria aina ya teksi ambayo aliitumia maeneo ya mjini Kigoma huku akishindwa kwenda vijiji vilivyo nje ya mkoa.

Tatizo hilo la usafiri kwa mgombea huyo lilingia katika hatua nyingine pale alipochukua gari la mgombea ubunge na kulazimisha gari hilo kulitumia kwenye mikutano yake na kuwatelekeza waandishi wa habari waliokuwa wakitumia gari hiyo kwenye msafara huo.
Chanzo:Mwananchi


Funny boy! haha!
 
Naye mwananchi mwingine wa kijiji hicho, Ramadhan Rajab (54), alisema kuwa nafasi ya urais inamtaka mtu ‘smati' ambaye anaweza kuzungumza na wadau mbalimbali katika kutetea maslahi ya wananchi, hivyo basi kitendo cha kumpa Rungwe nafasi hiyo wakati anafuga ndevu kinaweza kuwafundisha tabia mbaya.

"Huku kwetu usafi ni kitu muhimu, hatuwezi kuruhusu mtu kufuga ndevu ndefu kiasi hiki na anashindwa kuzitunza, huu ni uchafu, hatuwezi kumpa,"alifafanua.
Kheeee heeee heeee... Duniani kuna mambo!
 
Send to a friend Friday, 15 October 2010 07:40 0diggsdigg


Naye mwananchi mwingine wa kijiji hicho, Ramadhan Rajab (54), alisema kuwa nafasi ya urais inamtaka mtu ‘smati’ ambaye anaweza kuzungumza na wadau mbalimbali katika kutetea maslahi ya wananchi, hivyo basi kitendo cha kumpa Rungwe nafasi hiyo wakati anafuga ndevu kinaweza kuwafundisha tabia mbaya.

"Huku kwetu usafi ni kitu muhimu, hatuwezi kuruhusu mtu kufuga ndevu ndefu kiasi hiki na anashindwa kuzitunza, huu ni uchafu, hatuwezi kumpa,"alifafanua.

Chanzo:Mwananchi

He! Hii kali. Kufuga ndevu ni tabia mbaya!!!!!??????

Au Bado kuna watu wanatafuta akina baba warembo?
 
Ingekuwa busara sana kama NCCR wangeamua kutosimamisha mgombea na badala yake wamuunge mkono Dk Slaa... Fundisho kwa mapandikizi wote...
 
Back
Top Bottom