News Alert: Mbeba Vibuyu wa Rais afariki?

Enzi zangu nafanya kazi kwenye shirika moja la umma lilokuwa maarufu sana, meneja akihamishwa ofisi anahama na kiti chake kuogopa kuzidiwa kete.
Akishindwa kuhama na kiti chake basi ni lazima akiharibu ili mwingine akija ashindwe kikalia.

Huko aendako akikikuta kingine atatoa udhuru wa nguvu mpaka kinunuliwe kingine.

We fikiria zile kuta na sakafu za majumba ya sementi kali pale bongo watu wanazichimba ili wazike Hirizi zao humo, Wakishindwa wanatoboa mbao za milango kwa usiri mkubwa na kuweka hirizi zao humo.

Usione wako bussy kutengeneza viambaza vya maofisi lengo ni kufukua hirizi za wenzao ili waziweke zao na mara zote kazi zilikuwa zikifanywa na washika vibuyu wao.

Nchi ilo jaa Vingunge waabuduo Giza itajaenenda nuruni na kupata maendeleo ya kweli?
 
Yule bwana aliyemdondosha pale jukwaani MZA, ilikuwa ni vibuyu vilivyogongana; kibuyu kilichoshindwa kikadondoka chini.

Sijui yule bwana aliishia wapi; bado yumo lupango ama aliachiwa?
Wao wangekubali tu, kuwa kibuyu chake kilikuwa zaidi ya hicho chao wakubwa.

Yule wa Mza nilipata tetesi baada ya tukio kutoka kwa watu wanaodai wana utaalamu kiasi kuhusu hayo masuala. Wanadai alikuwa amejifunga hirizi ya kumfanya asionekane, kwa hiyo angepita tu kama hewa na kumpiga mweleka JK, kwa hiyo watu wangeshangaa tu kuona JK amedondoka chini. Lakini inadaiwa asingemdhuru, ati ni "mtani" wake. Sijui wakwere wana utani na kabila gani huko Mwanza? Lakini kwa bahati ya mwungwana, Kamati yake ya Ufundi ilikuwa "njema", kwa hiyo hirizi ya jamaa ikawa haifanyi kazi (ingawa yeye alipanda jukwaani kwa kujiamini kwamba haonekani), ndipo akaishia kupata kile "kisago" mlichoona kwenye TV siku ile.

Hatima ya kesi yake nakumbuka alihukumiwa kifungo fulani kifupi, kama kuna anayeweza ku-retrieve magazeti ya kipindi hicho atuwekee, maana iliandikwa.

Kali ilikuwa ile ya siku ya mwisho ya kampeni pale Jangwani, ule "mzinga" wataalamu wanadai ulikuwa "bab kubwa". Wanadai mizinga ya namna hiyo inakamilishwa kwa mkusudiwa kuomba maji, akiyanywa tu ndio kwa heri. Na walinipa reference za marehemu Kolimba na Ipy Malecela, ambao wote kitu cha mwisho walichofanya katika uhai wao baada ya kukumbwa na hilo "zinga" ni kuwa walikunywa maji, na wakafariki muda mchache baadae. Hapo tena ndipo Kamati ya Ufundi ya Mwungwana ilipocheza smart, kwani mwungwana hakuyaonja yale maji pale Jangwani jioni ile. Angeyaonja tu ingekuwa habari ingine, ndivyo wanavyodai.

Kaaz kwelkwel!
 
Zile safari za MZA za mwanzo mwanzo zilizoendeana na habari za mapanki inasemekana ilikuwa ni mipango ya kwenda kusuruhisha 'kamati za ufundi' za pande zote mbili. Baada ya hapo mambo yakawa waaa.
 
Back
Top Bottom