News Alert: Dr. Maua na wazalendo wafanya kweli tena!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Chama cha Msalaba Mwekundu nchini kimeendelea kupokea misaada ya kukipa uwezo wa kukabiliana na majanga yanayotokana na mafuriko ambayo yamesababisha maelfu ya watu kukosa makazi, chakula bora, na kuweka hatari maisha ya wananchi wengi wao wakiwa ni wazee, kina mama na watoto.

Awamu ya Pili ya michango inayochangwa kwa kuhamasishwa na mitandao ya JamiiForums.com, mwanakijiji.com, Issamichuzi.blogspot.com na kuratibiwa na kusimamiwa na Mtandao wa Wanataaluma Tanzania TPN imekabidhiwa kwa chama hicho siku ya Jumamosi mchana na kupokelewa na Mkurugenzi wa Maafa wa Chama hicho Bw. Joseph Kimaryo.

Akikabidhi michango hiyo Dr. Maua alifafanua kwa wananchi kuwa Chama cha Msalaba Mwekundu hakiendeshi kampeni ya Red Alert inayoendeshwa na Vodacom Foundation na hivyo kuondoa mchanganyiko ambao umetokea. Alisisitiza kuwa juhudi za kuwachangia waathirika ni za kila Mtanzania pasipo ulazima wa kutumia kwa makusudi kauli za kuwachanganya watu.

Misaada iiliyowasilishwa siku ya Jumamosi inafanya kiasi cha misaada ambayo imeshapatikana hadi hivi sasa kufikia thamani ya Shilingi milioni saba.

Zifuatazo ni baadhi ya picha za tukio hilo. Harambee hii inaendelea hadi tarehe 11 mwezi wa Pili ambapo tunatarajia michango zaidi itakuwa imepatikana. Mtu yeyote anaweza kuchangia kwa kupitia mitandao yote mikubwa ya simu nchini kwa kutuma neno "TPN" kwenda namba "15522" ambapo mtu atakatwa shs 250 kujiandikisha (mara moja tu) na kukatwa Shs 150 kwa siku thelathini bila ulazima wa kujisajiri tena bali atapokea uthibitisho wa kukatwa kiasi hicho kila siku.

mzee-mwanakijiji-albums-news-worthy-picture872-dr-maua-daftari-akikabidhi-awamu-ya-pili-ya-misaada-ya-wadau-wa-kuchangia-chama-cha-msalaba-mwekundu-cha-tanzania-kulia-ni-mkurugenzi-wa-maafa-wa-red-cross-bw-joseph-kimaryo.jpg
Dr. Maua Daftari akikabidhi awamu ya pili ya misaada ya wadau wa kuchangia Chama Cha Msalaba Mwekundu cha Tanzania. Kulia ni Mkurugenzi wa Maafa wa Red Cross Bw. Joseph Kimaryo

mzee-mwanakijiji-albums-news-worthy-picture875-bw-mtsimbe-anaelezea-kuwa-michango-ya-awamu-ya-pili-imefikia-gharama-ya-shs-milioni-5-ikiwa-ni-vitu-mbalimbali-kama-vinavyoonekana.jpg
Bw. Mtsimbe anaelezea kuwa michango ya awamu ya pili imefikia gharama ya Shs milioni 5 ikiwa ni vitu mbalimbali kama vinavyoonekana.

a kipindupindu. Madawa hayo yana dhamani ya Zaidi ya TZS Millioni 1.3."> Mkurugenzi Mtendaji wa CAPS Limited na Mdau wa TPN Mzalendo Peter Marealle akikabidhi madawa ya choo kwa Mlezi wa TPN kwa ajili ya matumizi ya vyo vya Wahanga wa Mafuriko. Dawa hizi zinaua wadudu wote na harufu mbaya na hivyo kuzuia uwezekano wa magonjwa ya Kuhara na kipindupindu. Madawa hayo yana dhamani ya Zaidi ya TZS 1.3 milioni.


mzee-mwanakijiji-albums-news-worthy-picture873-dr-maua-daftari-akikabidhi-awamu-ya-pili-ya-misaada-ya-wadau-wa-kuchangia-chama-cha-msalaba-mwekundu-cha-tanzania-kulia-ni-mkurugenzi-wa-maafa-wa-red-cross-bw-joseph-kimaryo-na-kushoto-ni-rais-wa-tpn-bw-sanctus-mtsimbe.jpg
Dr. Maua Daftari akikabidhi awamu ya pili ya misaada ya wadau wa kuchangia Chama Cha Msalaba Mwekundu cha Tanzania. Kulia ni Mkurugenzi wa Maafa wa Red Cross Bw. Joseph Kimaryo na kushoto ni Rais wa TPN Bw. Sanctus Mtsimbe
icon_out.png
 
Hafla ya Kukabidhi Misaada ya Wahanga Wa Mafuriko iliyokusanywa na TPN; Jamiiforums na Michuzi Blog kwa Chama Cha Msalaba Mwekundu Tanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Tarehe 30-01-2010 katika ofisi za Chama Cha Msalaba Mwekundu; Masaki jijini Dar Es Salaam.


attachment.php


Rais wa Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (TPN); Mzalendo Sanctus Mtsimbe; akitoa maelezo ya misaada iliyokusanywa katika awamu ya pili ya Kampeni kwa ajili ya kuwasaidia Wahanga wa Mafuriko. Pichani ni misaada mbalimbali ambayo ilikusanywa na Wadau mbalimbali.



attachment.php



Mlezi wa TPN Mzalendo Maua Dfatari (kati); Mkurugenzi wa Maafa wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Bw. Joseph Kimaryo na Rais wa TPN Mzalendo Sanctus Mtsimbe wakiteta jambo kabla ya hafla ya kukabidhi misaada katika Makao Makuu ya Chama Chama Msalaba Mwekundu; Masaki; Dar Es Salaam




attachment.php



Mlezi wa TPN Mzalendo Dr. Maua Dfatari (kati) akitoa maelezo kuhusiana na kampeni kwa; Mkurugenzi wa Maafa wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Bw. Joseph Kimaryo (Kulia) katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Chama Chama Msalaba Mwekundu; Masaki; Dar Es Salaam. Mzalendo Daftari aliweka wazi kuwa Kampeni yetu ni ya Kukisaidia na Kukiwezesha Chama cha Msalaba Mwekundu Red Cross na haina uhusiano wowote na kampeni ya Red Alert inayoendeshwa na Vodacom ambayo hata hivyo wameiga kutoka TPN na Wadau wake baada ya wao kudokezwa kuwa tutaendesha kampeni ya jinsi hiyo. Alisema TPN imefurahi kuwa imetoa changamoto na sasa wadau mbalimbali wanasaidia na kuendesha kampeni kuwasaidia wahanga ingawa ilikuwa ni jambo jema kuunganisha nguvu kwani wote lengo letu ni moja. Aliasa kuwa Muhimu kuliko vyote ni kuhakikisha kuwa misaada inafika kwa walengwa. Kampeni yetu inaendelea kwa kutuma SMS yenye neon TPN kwenda namba 15522.



attachment.php

Rais wa Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (TPN); Mzalendo Sanctus Mtsimbe; akitoa maelezo ya misaada iliyokusanywa katika awamu ya pili ya Kampeni kwa ajili ya kuwasaidia Wahanga wa Mafuriko. Pichani ni misaada mbalimbali ambayo ilikusanywa na Wadau mbalimbali. Mz. Mtsimbe alisema hadi sasa zaidi ya watu 1880 wanachangia katika kampeni ya SMS. Vitu vilivyokabidhiwa ni pamoja na ndoo; magodoro; miswaki na dawa za miswaki; sabuni; vyandarua; mablanketi; maji ya kunywa; Nguo mbalimabli za kike, kiume,watoto, Mataulo, mashati, Suruali; Viatu na Madawa ya vyooni vyote vikiwa na dhamani ya TZS Million 5.






attachment.php


Mkurugenzi Mtendaji wa CAPS Limited na Mdau wa TPN Mzalendo Peter Marealle akikabidhi madawa ya choo kwa Mlezi wa TPN kwa ajili ya matumizi ya vyo vya Wahanga wa Mafuriko. Dawa hizi zinaua wadudu wote na harufu mbaya na hivyo kuzuia uwezekano wa magonjwa ya Kuhara na kipindupindu. Madawa hayo yana dhamani ya Zaidi ya TZS Millioni 1.3.
 

Attachments

  • DSC05561.jpg
    DSC05561.jpg
    77.4 KB · Views: 590
  • DSC05559.jpg
    DSC05559.jpg
    63 KB · Views: 571
  • DSC05594.jpg
    DSC05594.jpg
    74 KB · Views: 571
  • DSC05616.jpg
    DSC05616.jpg
    82.2 KB · Views: 571
  • DSC05569.jpg
    DSC05569.jpg
    64.9 KB · Views: 559
Asanteni kwa kazi nzuri, tuko nyuma yenu.
Jana asubuhi nilibahatika kumuona na kumsikiliza Mzalendo Sanctus Mtsimbe akitoa taarifa ya maendeleo ya michango.

So far so good.

Pia ni kumkumbusha Mzalendo kila anapopata nafasi kwenye local media, atie msisitizo kuwa michango hiyo ni juhudi za pamoja za mitandao ya JamiiForums.com, mwanakijiji.com, Issamichuzi.blogspot.com na kuratibiwa na kusimamiwa na Mtandao wa Wanataaluma Tanzania TPN. Alipozungumza jana, alitaja TPN pekee, kwa mtazamaji mpya na msikilizaji hawezi elewa.

Together we can.
 
Asanteni kwa kazi nzuri, tuko nyuma yenu.
Jana asubuhi nilibahatika kukuona na kukusikiliza Mzalendo Sanctus Mtsimbe ukitoa taarifa ya maendeleo ya michango.

So far so good.

Pia ni nakukumbusha Mzalendo kila anapopata nafasi kwenye local media, atie msisitizo kuwa michango hiyo ni juhudi za pamoja za mitandao ya JamiiForums.com, mwanakijiji.com, Issamichuzi.blogspot.com na kuratibiwa na kusimamiwa na Mtandao wa Wanataaluma Tanzania TPN. Ulipozungumza jana, ulitaja TPN pekee, kwa mtazamaji mpya na msikilizaji wapya hawezi elewa hizi ni juhudi za pamoja.

Together we can.
 
Umoja ni nguvu,utengano ni udhaifu. Khila la heri wakuu na Mwenyezi Mungu awazidishie,nina imani kila kitu kitatumika kama mlivyopanga na kitamfikia kila muhitaji.
 
Asanteni kwa kazi nzuri, tuko nyuma yenu.
Jana asubuhi nilibahatika kumuona na kumsikiliza Mzalendo Sanctus Mtsimbe akitoa taarifa ya maendeleo ya michango.

So far so good.

Pia ni kumkumbusha Mzalendo kila anapopata nafasi kwenye local media, atie msisitizo kuwa michango hiyo ni juhudi za pamoja za mitandao ya JamiiForums.com, mwanakijiji.com, Issamichuzi.blogspot.com na kuratibiwa na kusimamiwa na Mtandao wa Wanataaluma Tanzania TPN. Alipozungumza jana, alitaja TPN pekee, kwa mtazamaji mpya na msikilizaji hawezi elewa.

Together we can.

Mzalendo; mimi sikupata nafasi ya kusikia. Unajua katika media nimejifunza kitu kimoja, si kila kitu kinatolewa. Nadhani wanarusha maximum 20 seconds. Sasa sijui ni kipande gani kinachotolewa.

Huwa najitahidi kila ninapoweza kuwataja wadau wote. Bahati mbaya sana katika hili wadau wengine hawakuwepo tofauti la lasti time. Nadhani majukumu yalikuwa mengi.
 
Asanteni kwa kazi nzuri, tuko nyuma yenu.
Jana asubuhi nilibahatika kukuona na kukusikiliza Mzalendo Sanctus Mtsimbe ukitoa taarifa ya maendeleo ya michango.

So far so good.

Pia ni nakukumbusha Mzalendo kila anapopata nafasi kwenye local media, atie msisitizo kuwa michango hiyo ni juhudi za pamoja za mitandao ya JamiiForums.com, mwanakijiji.com, Issamichuzi.blogspot.com na kuratibiwa na kusimamiwa na Mtandao wa Wanataaluma Tanzania TPN. Ulipozungumza jana, ulitaja TPN pekee, kwa mtazamaji mpya na msikilizaji wapya hawezi elewa hizi ni juhudi za pamoja.

Together we can.

Mzalendo; mimi sikupata nafasi ya kusikia. Unajua katika media nimejifunza kitu kimoja, si kila kitu kinatolewa. Nadhani wanarusha maximum 20 seconds. Sasa sijui ni kipande gani kinachotolewa.

Huwa najitahidi kila ninapoweza kuwataja wadau wote. Bahati mbaya sana katika hili wadau wengine hawakuwepo tofauti la lasti time. Nadhani majukumu yalikuwa mengi.
 
Mzalendo; mimi sikupata nafasi ya kusikia. Unajua katika media nimejifunza kitu kimoja, si kila kitu kinatolewa. Nadhani wanarusha maximum 20 seconds. Sasa sijui ni kipande gani kinachotolewa.

Huwa najitahidi kila ninapoweza kuwataja wadau wote. Bahati mbaya sana katika hili wadau wengine hawakuwepo tofauti la lasti time. Nadhani majukumu yalikuwa mengi.
.

Hawakukata kitu, nadhani ni live recording na flow was ok.
Tumekuelewa.

Tuko pamoja Mzalendo.

Together we can.
 
Aliyefanya kweli Dk. Maua au wananchi waliochangia?

Mtsimbe hana makuu ya kifisadi, ndiyo maana anapeta na viatu vya Marco Polo vilivyopitia "The Silk Road". Viatu vimeona mengi hivyo na vina zali lake.

Mi naiangalia hiyo mi kasri ya kifisadi tu pembeni hapo kwenye picha, utafikiri Uswizi kumbe bongo.
 
Wivu wa Kike kama alivyosema Nkapa!


Haaa haaa, kama alivyosema Mzee Msekwa Mkuu; TAMWA na TNGP wakamjia juu.

Anachofanya mzalendo Maua ni jukumu lake la kikatiba kama Mlezi. It is more ceremonial ingawa anayo sehemu yake kama mshauri pia.

Tunayefanya naye kazi anatutia sana moyo. Maana haagalii saa wala nini ni mzigo tu. Ukichelewa kumpa update anakupigia kwanza wewe. Ana ku-update kazi ulizompa amefikia wapi kisha na yeye andemand umefikia wapi. Sometime ni vigumu kwenda na speed yake lakini tunaenda vizuri mpaka sasa.

Sasa kama kuna wivu basi ngoja tuwasikie . . .
 
Back
Top Bottom