Chama Kipya cha Siasa (AFTP) Chaanzishwa

Status
Not open for further replies.

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,447
39,855
Chama kipya cha kisiasa cha AFTP kimepata usajili wa muda leo mbele ya Msajili wa Vyama vya Kisiasa. Chama hicho ambacho lengo lake ni kuwavutia wakulima kinajulikana kama Alliance Farmers Party ambacho sasa hivi Mwenyekiti wake wa Muda ni Said Sudi Said. Bw. Said akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupata usajili huo wa muda alisema kuwa "tunawaendea wakulima kwa sababu wamesahauliwa na vyama vingi vilivyopo". Kwa mujibu wa sheria za vyama vya kisiasa, chama hicho kipya kinatakiwa kizunguke ndani ya angalau mikoa kumi na kupata wanachama angalau 200 ili kiweze kupata usajili wa kudumu.
 
Nadhani kama unawaunga mkono utakuwa unakaribishwa... as a matter of fact nadhani hiki chama ni kinyume na sheria.. Kwa sababu Katiba inakataza kuunda chama kwa misingi ya kuhudumia watu wa kundi fulani..
 
mhhhhhhhhhh kazi kweli kweli,baada ya kumiliki GAZETI LA RAIA MWEMA sasa wanakuja wanaanzisha CHAMA,duh wa-tz tumechoka na mavyama kibao.tunataka vyama vicheche vyenye sera ZA KUMKOMALIA NYANI GILADI bilaya kumtizama machoni.
 
Tanzania labor party basi nacho kipo kinyume cha sheria kwa m isingi hiyo

Labour Party, sidhani ni cha msingi wa "labour" kama unavyotaka iaminike. Na chenyewe kama ni kwa msingi wa watu wa kundi fulani chaweza kuwa na makosa!
 
Hakuna mtu anayeweza kusema ana escape "labor" in one form or another.Ukitaka kusema labor ina discriminate basi mpaka Chama cha Mapinduzi kina discriminate maana kuna watu hawaamini katika Mapinduzi.

Labor is OK kwa sababu haija specify a segment of the population,granting one is of age and sane, sasa kama wewe sio mfanyakazi na huna interest na mambo ya kazi (kazi being ukulima, professional, semi profession na non professional workers na hata ufanyabiashara) wewe utakuwa unafanya nini?
 
mhhhhhhhhhh kazi kweli kweli,baada ya kumiliki GAZETI LA RAIA MWEMA sasa wanakuja wanaanzisha CHAMA,duh wa-tz tumechoka na mavyama kibao.tunataka vyama vicheche vyenye sera ZA KUMKOMALIA NYANI GILADI bilaya kumtizama machoni.

Mkuu engineer!!..Hapa unamaana gani haswa...? Yaani Raia mwema wana mkono kwenye chama kipya?
 
Huu utitiri wa vyama mpaka lini? :confused:
Tayari tuna vyama vingi vya kisiasa Tanzania, hivi wamekosa chama ambacho sera za chama hicho zinashabihiana na chama chao mpaka waunde chama kingine!?

Sasa hivi mkakati uwe ni kuunganisha vyama ili kupata chama kimoja chenye nguvu na wanachama kila kona ya Tanzania ili kuiondoa CCM madarakani hapo 2010, badala ya kuongeza utitiri wa vyama ambao hautasaidii chochote Watanzania.
 
Na vije tu katika "soko la mawazo" tutaona vyama makini ni vipi na dhaifu ni vipi.Tunachotaka ni kujenga upinzani makini kwa kutumia haki za kikatiba, kukataza, kutokubali au kuchukia mtu kuanzisha chama wakati hujajua mchango wake utakuwaje ni sawa na kumkataa mtoto mchanga.

Labda kuna nafasi ya kuongeza vitu vinavyokosekana katika upinzani.

But you also have a justified right to be cynical based on past experience.
 
jamaa mwenyewe Said alikuwa anazungumza tu "demokrasia haina kikomo, mkiona kuna jamii ya watanzania ambao maslahi yao hayajatiliwa maanani na chama chochote basi anzisheni chama"...
 
Sioni kama ni tatizo. Kwana wana JF walivyosema CCM ni cha wanamapinduzi, au cha wakulima na wafanyakazi kama kinavyojiita, inagwa sasa hivi inaonekana kimewatosa wakulima na wafanyakazi na kuwaleta Karamagis. Naona kinaweza kukubaliwa.
Lakini wanaJF naona ingekuwa ni jambo la maana kama tungejadili ili kuona kama kweli Tanzania tuna haja na utitili wa vyama, are we using democarcy or abusing it?
 
Chama kinaweza kuwa cha wakulima lakini si kwa ajili ya kundi la wakulima tu. Na chama cha wakulima kinaweza kisiwe na hata mkulima mmoja kwenye ngazi za uongozi. Kinaweza kisiwe na wakulima hata kwenye safu ya wanachama. Jina la chama linaashiria nia ya chama. Makosa yatakuwepo kama wasio wakulima hawaruhusiwi kujiunga na kushiriki uongozi.

Chama cha wakulima kinaweza kikawa tu ni chama ambacho mojawapo ya malengo yake makuu ni kutetea wakulima. Huhitaji kuwa mkulima ili kutetea wakulima.

Kwetu sisi, wakulima ni 85% ya watu wote. Chama cha wakulima si chama cha kundi moja la watu. Chama ambacho sii cha wakulima kitakuwa ni cha kikundi hicho cha 15% ya watu waliobaki, na hiyo ni hitilafu.

Sina uhakika kuhusu nia ya waanzilishi wa chama kipya. Inaweza kuwa ni kupata ruzuku. Inaweza kuwa ni kuugawanya upinzani zaidi. Kinaweza kuwa kimeanzishwa kwa siri, na CCM. Yetu macho. Time will tell.
 
AM nakubaliana nawe kabisa kuwa inawezekana kukawa na mkono wa CCM katika uanzishaji wa hiki chama kipya cha 'Wakulima'.
Hawa jamaa wanauhakika kuwa kuanzishwa kwa chama hicho kutachota na kugawa nguvu ya baadhi ya vyama vya upinzani na kuvidhoofisha hasa kwa wakati huu ambao dalili za umoja miongoni mwa vyama vikuu vya upinzani zinaonekana kutokana na vuguvugu la mageuzi ya kifikra kuenea miongoni mwa WaTz.
Nimemsikiliza mwenyekiti wa muda hoja zake, lakini mmh! napata mashaka na dhamira yao.
 
mhhhhhhhhhh kazi kweli kweli,baada ya kumiliki GAZETI LA RAIA MWEMA sasa wanakuja wanaanzisha CHAMA,duh wa-tz tumechoka na mavyama kibao.tunataka vyama vicheche vyenye sera ZA KUMKOMALIA NYANI GILADI bilaya kumtizama machoni.

Engineer Mohamed, hebu fafanua hapa, una maana Said Soud Said ni mmimiliki wa gazeti la RAIA MWEMA? Au Jenerali Ulimwengu anahusika na kuanzisha chama hicho? Au una maana gani, hebu weka wazi ama kama vidole vimeteleza pia tufafanulie
 
jina la chama sio dili, hata ujerumani kuna chama cha mazingira, chama cha kijani na kadhaa wa kadhaa. na wala haina maana kuwa wengine haviwahusu.


ila cha kujiuliza na kutaka kujua nn malengo yao ya kuanzisha chama jee kinaweza kuongeza fikra mbadala au ndio yale yale.


wanao uhuru kisheria kuanzisha chama na tusivize demokrasia.
 
Mzee mwanakijiji,
Tafadhali naomba kufahamishwa ktk hili.
Huyu bwna Said kaanzisha CHAMA kama JUMUIYA au CHAMA cha SIASA?.... maana kuna tofauti kubwa kimlengo kati ya vyama hivi, tena nadhani itakuwa kiswahili kizuri zaidi ikiwa tutakuwa tukitumia neno Jumuiya moja kwa moja badala ya kutanguliza neno CHAMA tunapoanzisha hizi jumuiya. Mathalan Jumuiya ya wakulima au Jumuiya ya wafanyakazi badala ya chama cha wakulima au wafanyakazi. Neno chama litumike tu pale linapohusina na siasa zaidi...
haya ni mawazo yangu binafsi....
 
Nadhani kama unawaunga mkono utakuwa unakaribishwa... as a matter of fact nadhani hiki chama ni kinyume na sheria.. Kwa sababu Katiba inakataza kuunda chama kwa misingi ya kuhudumia watu wa kundi fulani..

Kama hivyo ndiyo, hata CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi. Bendera ya CCM inaliweka hili wazi.

Ccmtanzania.gif
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom