News Alert: CCM kumuenzi Nyerere

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Maamuzi ya kwanza kabisa yaliyotolewa kwenye kikao cha NEC Butiama ni hatua mahususi za kumuenzi Baba wa Taifa. Bado napitia nyaraka fulani kwani nilikosa kusikiliza vizuri sehemu ya kwanza (matatizo ya kiufundi) lakini naamini mambo makubwa mawili yaliamuriwa.

a. Kuchapisha maandishi, hotuba, na kazi za Mwalimu katika mkusanyiko maalum ili watu wengi waweza kuzipata (??)
b. Kuiagiza serikali ya Jamhuri ya Muungano kuhakikisha kuwa Butiama inakuwa makao makuu ya wilaya Mpya wakati wilaya ya Bunda itakapogawanywa.

Maamuzi mengine ni pamoja na kuanzisha vyuo vya itikadi ya chama ili wanachama wa CCM wajue chama chao vizuri na pamoja na kuimarisha jumuiya za Chama (Vijana, Wanawake, na Wazazi)

Maamuzi hayo ya kumuenzi Nyerere yanaenda kinyume na madai ya Makamba na Kingunge kuwa NEC imeenda Butiama kama kikao cha kawaida na badala yake kimefanya maamuzi ya kumuenzi Nyerere ikiwa ni ishara ya Chama hicho kufufua mawazo na fikra za Mwalimu ambazo watu wengi wameona kuwa kimezisahau.
 
SAD IN DEED. UNADHANI MWALIMU ANGEPENDA KUENZIWA KWA NJIA HIYO???
mwalimu angependa kuenziwa kwa kupambana na ufisadi, kutoa elimu ya maana, huduma za afya za maana etc etc, labda na kumwadhibu vikali Lowassa.
 
Maamuzi ya kwanza kabisa yaliyotolewa kwenye kikao cha NEC Butiama ni hatua mahususi za kumuenzi Baba wa Taifa. Bado napitia nyaraka fulani kwani nilikosa kusikiliza vizuri sehemu ya kwanza (matatizo ya kiufundi) lakini naamini mambo makubwa mawili yaliamuriwa.

a. Kuchapisha maandishi, hotuba, na kazi za Mwalimu katika mkusanyiko maalum ili watu wengi waweza kuzipata (??)
b. Kuiagiza serikali ya Jamhuri ya Muungano kuhakikisha kuwa Butiama inakuwa makao makuu ya wilaya Mpya wakati wilaya ya Bunda itakapogawanywa.

Maamuzi mengine ni pamoja na kuanzisha vyuo vya itikadi ya chama ili wanachama wa CCM wajue chama chao vizuri na pamoja na kuimarisha jumuiya za Chama (Vijana, Wanawake, na Wazazi)

Maamuzi hayo ya kumuenzi Nyerere yanaenda kinyume na madai ya Makamba na Kingunge kuwa NEC imeenda Butiama kama kikao cha kawaida na badala yake kimefanya maamuzi ya kumuenzi Nyerere ikiwa ni ishara ya Chama hicho kufufua mawazo na fikra za Mwalimu ambazo watu wengi wameona kuwa kimezisahau.

Watuondolee upuuzi wao! Kama kweli wanataka kumuenzi Mwalimu kwanza wawataje na kuwatia ndani na kuwafilisi mara moja wahusika wa ufisadi wa BoT, Richmonduli, ununuzi wa Rada na ufisadi mwingine. Vinginevyo tumechoshwa na usanii wao kila kukicha.
 
CCM wanashindwa kufanya maamuzi makubwa yanayohusu maisha ya Watanzania wengi badala yake wanakimbilia kwenye PR kwa kutumia jina la Nyerere.

Nyerere alisimamia haki za msingi za wanyonge na sio kutukuzwa. Haki itatoka wapi wakati vijana wanahangaika mitaani bila kujua watafanya nini?
 
CCM wanashindwa kufanya maamuzi makubwa yanayohusu maisha ya Watanzania wengi badala yake wanakimbilia kwenye PR kwa kutumia jina la Nyerere.

Nyerere alisimamia haki za msingi za wanyonge na sio kutukuzwa. Haki itatoka wapi wakati vijana wanahangaika mitaani bila kujua watafanya nini?

Kazi kwenu wenye imani na Kikwete kabla na sasa .Mimi nilisha hana nia na Nchi wala nini ila utajiri wa Nchi na CCM yake.
 
Mimi swali langu lilikuwa haya ya kumuenzi Nyerere yalitokea wapi wakati walisema ni kikao cha "kawaida"... ?
 
Ama kweli sisiem sasa wameamua kujichimbia kaburi refu ili tuwafukie mapema.
Mwisho wao mbona umeshafika,Kumuenzi mwl kwa lipi?astaghafulullah!Nani ana ujasiri leo wa kukemea hadharani wanaofanya biashara kwa jina la chama cha sisiem kama RA,Nchi imeuzwa kwa wakoloni(wawekezaji??),Madini aliyosema mwl yabaki hapa wameruhusu walowezi wanachukua yote bila hata faida kwa kigezo kuwa hatuna vitendea kazi??
Tena wasitupandishe mzuka kabisa.Nani anafuata kwa dhati maadili
ya uongozi ya mwl??
 
Masikini Mwafrika wa KIke na matumaini alokuwa nayo kwa JK.

Wewe acha tu,

Nimetumia advil za kutosha for the last 16 hours ili kutuliza maumivu ya kichwa niliyoyapata hapa. These guys hata hawana aibu wala chembe ya utaifa hata kidogo. Dissapointment kubwa hapa ni kwa Kikwete ambaye alikuwa na nafasi nzuri tu ya kugeuza mambo lakini ameshindwa.

Taifa zima lingekuwa nyuma yake, wananchi wote wangekuwa agents wa usalama wa taifa na kumlinda Kikwete dhidi ya mafisadi wa ccm. Huyo Mkono mwenyewe hata huko musoma kwenyewe hapendwi pamoja na kujenga shule (bila kuleta walimu) kwa kutumia kasehemu tu ka mabilioni aliyolipwa na benki kuu.

Kikwete angeonesha bollz kwa kuanza na huyo Mkono mwenyewe na wengine wote kina Rostam na Chenge wangezima fegi zao. Haya mengine sasa ni historia.

Mapambano yameanza sasa kumzuia Kikwete asiuze zaidi ya nusu ya Tanzania by the time anatoka ofisini!
 
Wewe acha tu,

Nimetumia advil za kutosha for the last 16 hours ili kutuliza maumivu ya kichwa niliyoyapata hapa. These guys hata hawana aibu wala chembe ya utaifa hata kidogo. Dissapointment kubwa hapa ni kwa Kikwete ambaye alikuwa na nafasi nzuri tu ya kugeuza mambo lakini ameshindwa.

Taifa zima lingekuwa nyuma yake, wananchi wote wangekuwa agents wa usalama wa taifa na kumlinda Kikwete dhidi ya mafisadi wa ccm. Huyo Mkono mwenyewe hata huko musoma kwenyewe hapendwi pamoja na kujenga shule (bila kuleta walimu) kwa kutumia kasehemu tu ka mabilioni aliyolipwa na benki kuu.

Kikwete angeonesha bollz kwa kuanza na huyo Mkono mwenyewe na wengine wote kina Rostam na Chenge wangezima fegi zao. Haya mengine sasa ni historia.

Mapambano yameanza sasa kumzuia Kikwete asiuze zaidi ya nusu ya Tanzania by the time anatoka ofisini!

Pole sana ndugu yangu - tukusanye nguvu tuzidishe mapambano iko siku ndoto ya kuiona TZ yenye neema na kila MTZ kufaidi rasilimali ya nchi yake itafika japo kama hatukuyaona sisi mabadiliko hayo lakini itakuwa ni kati ya waloanzisha mizizi ya ukombozi.
 
Mzee Mwanakijiji heshma mkuu,
Kuhusu kauli za Makamba achana nazo kwani, unamjua vizuri kabla hajaingia jeshini alikuwa anafanya kazi ya vichekesho kama Kingwendu, bado ucommedy haujamtoka.

Kuhusu kumuenzi baba wa Taifa mimi naunga mkono katika yafuatayo:-
(a) kuifanya Butiama makao makuu ya wilaya mpya, endapo wananchi wa wilaya hiyo watashawishika kulikubali hilo.
(b) Kuchapisha maandishi, hotuba, na kazi za Mwalimu katika mkusanyiko maalum ili watu wengi waweza kuzipata. Baada ya kuchapisha zisambazwe maktaba mbalimbaliili watu wasome WAINGIWE NA DHANA YA UJAMAA NA KUJITEGEMEA. Ila CCM itakuwa ktk hati hati

Napinga kwa nguvu zote, kuanzishwa kwa vyuo vya itikadi ya chama, Chama gani? hii ovyo, Mwl. mwenyewe alitanguliza utaifa siyo uchama. Wajenge vyuo vya kilimo, sayansi, sanaa etc.
 
Kuiagiza serikali ya Jamhuri ya Muungano kuhakikisha kuwa Butiama inakuwa makao makuu ya wilaya Mpya wakati wilaya ya Bunda itakapogawanywa.

Hivi hizi gharama za kuanzisha hayo makao makuu tunazijua kweli? Kuna sababu gani ya maana ya huu utitiri wa wilaya mpya? Mimi naona ni yale yale ya polisi posti. Badala ya askari kuwajibika kutembelea maeneo yao sasa wanakaa kwenye post hizo wakitegemea wahalifu wataletewa!
 
Witness the development of a "cult of personality". Sad thing is Nyerere is not there to defend himself against this barrage of the highest degree of pretentiousness, give me a break.

The man who appointed Lowassa PM is now professing to lead a party that is holding Nyerere so dearly, give me a break.

The man who can't even discipline corrupt elements within his own party is all of a sudden so pro Nyerere he cant wait to implement some cosmetic initiatives, such as a new district and some such appeasing gestures, what about adopting the no nonsense Nyerere anti-corruption doctrine? Give me a break.

I believe Mwalimu must be rolling in his grave,I am with the publication thing but some of these extravagances such as new districts I don't think the man himself, modest as he was, would stand that nonsense.

But why am I surprised? Nyerere himself taught them ufisadi and how to steal elections (Zanzibar 1995, remember?)
 
Chief Pundit,

When Mwalimu finishes his rolling, a political death must happen (my personal preference is for all mafisadi like EL, RA and even NM who gave away Tsh. 50m to CCM or rather to silence JK). This is totally waste of taxpayers' money, government's resources and does not do justice to wadanganyika.

I, too, like the publication of Mwalimu's speeches, notes, etc. However, all this work belonged to Mwalimu and not CCM and therefore, I do not think it's CCM's place to do this. I think The Mwalimu Nyerere Foundation (together with his family) should be responsible for the fundraising for the project, copyright and the control of everything with Mwalimu's name on it. I will personally donate to such entity and not CCM.

I would also like to agree with other waheshimiwa saana...to remember Mwalimu by building schools,dispensaries, roads etc. Or, to simplify, how about maintaining every building, road, school etc that has Mwalimu's name? I don't believe Nyerere Roads around the country are paved to the standard of the bearer of the name...not to mention the international airport, schools or hospitals.
 
Kuchapisha, maandishi ya Mwalimu, ambayo wao wenyewe hawawezi kuyafuata, ambayo hata Mwalimu mwenyewe yalimshinda akaishia kutuachia matatizo Visiwani na a fragile political system, ambayo ni a big joke! I mean unaanzishaje siasa za vyama vingi na sheria za chama kimoja?

Hivi sisi wa-Tanzania tumekula nini? Exactly what is wrong with us? Inaonekana wengi wetu tunahitaji a brain surgery, I mean what kind of nonesense is this? Kuhamisha makao makuu ya wilaya kuwa Butiama, ili iweje? Wanafunzi hawana hela huko nje ya nchi makao makuu Dodoma yamewashinda, sasa wanaongelea makao ya Butiama, ili iwe nini?

Hivi ni lini wa-Tanzania tutaachana na maandishi na maneno ya Mwalimu? Hivi ni wapi Mwalimu alisema alipokuwa akitoa hela za mikutano isiyokwisha ya CCM? Mwalimu ni baba wa taifa, tunamshukuru kwa mengi mazuri aliyotufanyia, FULL STOP!

Mimi nilitegemea huko tutaambiwa kuwa sasa CCM imeamua kufuata utawala wa sheria, kwamba sasa itakuwa respect kwa rule of law, kwamba viongozi waliopatikana na tuhuma za ufisadi watafikishwa mahakamani, au CCM itawatenga mpaka watakapo safishwa na sheria, badala yake wanakuja na this joke, eti kuyaenzi maandishi ya Mwalimu, baada ya vurugu zote walizozifanya kwenye uchaguzi wa rais uliopita mpaka Mkapa kukataa katiba za CCM leo wataenzi maaandishi ya asiyekuwepo? Katiba hiii iliyopo ya CCM wameishindwa kuienzi lakini wataenzi maneno ya asiyekuwepo? Kuhamisha wilaya kuwa Butiama, Who cares? what that has to do na baadhi ya viongozi mafisadi ndani ya CCM?

Kwenye haya mawili ya kuhamisha makao ya Butiama na kuyaenzi maandishi ya Mwalimu, ni waste of time, unless kuna mengine muhimu yaliyoamuliwa huko, I am down na kura ya maoni kwa visiwani, ingawa kwa shingo upande lakini angalau,

Lakini this two, Mkuu MMJ tafadhali warudishie wenyewe, wa-Tanzania tufike mahali kwamba sasa ya Mwalimu, yametosha this is our time, kama watu hawawezi uongozi wawaaachie wengine wapo wengi wanaoweza, lakini enough na kutuchezea wa-Tanzania na maneno ya Mwalimu, I hope kuna mengine zaidi yaliyoongelewa huko zaidi ya haya matatu so far!
 
Mkuu ES, naona wamekuuzi sana lakini jamani si tulisema kabla ya kikao issue itakuwa ni muafaka tu!!! Ajabu ya Mussa mkuu wa kaya hata hiyo ameshindwa kuipitisha. what a joke!!!

Kuna siri moja kubwa imejificha kwenye tamko la NEC, nayo ni ule mpango uliokuwa umepigiwa kelele kutenganisha siasa na biashara, wakuu wa kazi kina Rostam wamehijack na mkuu wa kaya ameshindwa kuelewa bao walilopiga wenzake.

Ebu wataalamu humu ndani watueleze::

Serikali mbili zimeambiwa zitengeneze sheria ili watu wa kwenye vyombo vya dola wasiwe na biashara!! Sio CCM itunge sheria za viongozi wake wa kisiasa serikalini but wafanya kazi wote wa serikali wataguswa.

Are u kidding me?? Yaani wataalam ambao sio wanasiasa serikalini nao watakumbumbwa na huu upuuzi?? What is this??

Bao lenyewe ni since kina Rostam, Chenge, Mkono, Mo Dewji, Mkapa, Kigoda, Lowassa, Sumaye nk wao hawako kwenye vyombo vya dola bali wako kwenye CC, NEC hawatakumbwa na utenganishi wa siasa na biashara. (nimemweka chenge hapa sababu uwaziri wake uko numbered in months)

Mkuu wa kaya kweli wamempata!!!
 
Nyerere hakutaka Butiama iwe makao makuu

Na Beldina Nyakeke, Musoma

CHIFU wa Kabila la Wazanaki, Japhet Wanzagi amesema azma ya Rais Jakaya Kikwete kukifanya kijiji cha Butiama kuwa makao makuu ya Wilaya ya Musoma Vijijini, inapingana na mpango wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.

Wanzagi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Ukoo wa Burito Nyerere, amesema mpango wa Mwalimu Nyerere ulikuwa ni kuifanya Butiama kuwa kijiji cha historia, kinyume na azma hiyo ya Rais Kikwete.

Chifu huyo alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu kauli ya Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Halmashauri Kuu ya chama hicho kijijini Butiama hivi karibuni.

Wanzagi alisema kimsingi hapingani na azma ya Rais Kikwete ya kutaka kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa kufanya mambo mbalimbali, ikiwamo kukifanya kijiji cha Butiama kuwa makao makuu ya wilaya, lakini akasisitiza kuwa anao ushahidi ingawa si wa maandishi ambao kabla ya kifo chake, Mwalimu Nyerere aliwahi kumweleza nia na madhumuni ya kukifanya kijiji hicho kuwa cha kihistoria.

Alisema katika nia hiyo, Mwalimu Nyerere alipendekeza kijiji cha Kiabakari kilicho jirani na Butiama ndio pawe makao makuu ya wilaya.

Wanzagi alisema endapo serikali itaamua kukifanya kijiji hicho kuwa makao makuu ya wilaya, upo uwezekano wa kuchanganya mila na desturi za makabila mbalimbali kijijini hapo kutokana na muingiliano wa watu watakaohamia katika mji huo hali ambayo Mwalimu Nyerere hakupenda iwepo.

"Ninao ushahidi japo si wa maandishi. Na sijui hata kama Mama (Mama Maria) anajua kuwa mzee hakupeda kijiji cha Butiama kuwa mji. Maana aliniambia kuwa Butiama itakapokuwa mji, basi kutakuwepo na muingiliano wa watu wa makabila mbalimbali na kupoteza uasilia wa kijiji chetu ambapo alitolea mfano jiji la Dar es Salaam, ambalo kutokana na muingiliano wa watu, wenyeji wa pale, yaani wazaramo, wamehama na kusogea nje kabisa ya jiji," alisema.

Katika hotuba yake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa NEC, Rais Kikwete alisema ili kumuenzi Mwalimu Nyerere, serikali itakapofikia uamuzi wa kuigawa wilaya ya Musoma Vijijini, Butiama lazima kiwe makao makuu ya wlilaya na kuungwa mkono na mkutano huo na kuiagiza serrikali kufanya haraka kutekeleza pendekezo hilo.

Katika hatua nyingine, Chifu Wanzagi, aliitaka serikali kuwawezesha wakulima kwa kuwapa mahitaji muhimu ikiwa ni pamoja na pembejeo ili kuboresha kilimo.

Source: Mwananchi

Swali: Butiama ni kijiji ya Ukoo wa Chifu Burito?
 
Nakumbuka kuna wakati nyumba yake ya Magomeni ilikuwa iende na maji. Mbona hawa wanaotaka kumuenzi leo wote walikuwa MIA?

Na kweli tunaweza kusema tunapafanya mahali kuwa makao makuu ya wilaya kwa sababu ya kumuenzi fulani? Hatuangalii masuala mengine kama location, huduma zilizopo na kadhalika? Tutafika kweli?
 
I really dont know what to say!

...But what a shame!

Hicho kinachofikirisha na kuzungusha FIKRA ya wana CCM waliokaa na Kuja na dhana ya Kumuenzi JKnyerere Nini?

Ni ninikinaingilia mfumo wa fikra wa watu wazima na kuja na fikra zisizo na Mantiki yeyote?

Ni nini hicho kinacho weza kuingia na kuteka fikra za mwanadamu timamu na kujilinganisha na eti kumuenzi Jk nyerere kwa fikra zilizokufa na zisizo na uhai wowote?

Its realy sad!

kinachowafkirisha hawa watu chenyewe hakina UTU...!Hakina uhusiano na umbresha mwanaadamu kwa namana yeyote!

Fikra za hawaviumbe zikoupside down!Si zakutegemewa hata kidogo.

Fikra zao haziko kwnye wakati kabisa!!

But let me send a very srong worning to this people...!

TANZANIA SIO MALI YAO!!!Hili lazima liwe wazi kabisa!!

TUNA HAKI YA KUFIKIRI KATIKA NJIA NYOOFU "WHAT IS RIGHT FOR OUR COUNTRY!!!" NA HILO LITAFANYIKA!!Wale walioko madarakani hawataweza kutuzuia kufnya tunachofikiri ni sahihi dhidi yao, na fikra zao mfu!

Vinginevyo?

WAAMKE NA KUFIKIRI KIKAMILFU au ....!!!
 
Back
Top Bottom