New York: Uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour Tanzania - Starring Samia Suluhu Hassan, President of The United Republic of Tanzania

Point hivi wa chini maslai duni wanateseka wanakusanya kwa uzalendo Ili nchi iwe na pesa tuwe na maendeleo kwa jumla.Lakini wa juu wanazitafuna haswaa tena bila hata huruma, mabilioni na mabilioni na awachukuliwi hatua.Ripot ya CAG isiyofanyiwa Kazi ni SAwa na wimbo wa KILA jumapili kanisani,kama mamlaka hazichukui hatua kuwawajibisha wezi nini umuhimu wa CAG sasa,si SAwa na muimba kwaya tu kanisa.
Point nyingine watu wengi walikuwa wazalendo Sana wamefanya Kazi kwa uaminifu mkubwa leo hii walishastaafu ni masikini mbwa wanajutia uaminifu wao ikiwemo kuchekwa na jamii, serikali imewatupa na uaminifu wao.
Key points serikali kutochukua hatua za upigaji wa wachache ni kuwavunja moyo walipa kodi.
Ina maana wao pekee ndo wenye shida ya pesa,kuliko hawa wa chini wafanyao Kazi kama watumwa kwa maslai mbuzi,huku wanazikusanya kwa kupigwa jua, mvua,kazini masaa 12 tena bila overtime,posho , hardship allowence,na stahiki zote?
Au na wewe umo kwenye mfumo wa upigaji, maana nchi hii imelaaniwa kwa upigaji na majizi ya awamu ya nne yamerudi kazini.
Mkuu 'Kalunya', sasa nimekuelewa unachosema, lakini sikubaliani na msimamo wako.

Kwa hiyo, kwa maoni yako, kwa vile wakubwa 'wanapiga' na hawa wengine wote pamoja na uzalendo wao unataka na wao wageuke wawe wapigaji?
Mantiki ya namna hii uliiona wapi?

Unahimiza kila mtumishi aliye na nafasi, asitekeleze majukumu yake kwa uaminifu, kwa vile wakubwa wanapiga?
Unataka kila mwenye nafasi inayomwezesha kupiga, afanye hivyo, kwa sababu asipofanya hivyo, atastaafu akiwa maskini, na watu kama wewe mtakuwa mkimcheka kwa vile hakutumia nafasi yake kwa manufaa yake mwenyewe?

Haya ni mawazo ya kipuuzi kabisa.

Kama uovu unaofanywa na hawa viongozi juu ya nchi hii unakuumiza kama waTanzania wengine wote, huwezi kuja hapa na kushangilia maovu hayo hata kama ni kwa aina ya kukata tamaa kama unavyoonyesha wewe hapa.

Haya mambo ya uandishi wa kuzungukazunguka, ukionekana kushangilia uovu, kumbe nia yako ni kuumia kwa uovu huo, ni uandishi mbovu.

Sema wazi unachotaka kusema, usizunguke kama kusifu kumbe una maana ya kulaani.

Sasa unamulaumu nini huyo bosi hapo juu ambaye hata baiskeli hana, lakini analinda heshima yake na heshima ya nchi yake.

Wewe ni mmoja wa wapuuzi, na nimekuweka kwenye orodha hiyo hapa JF.

"KALUNYA", ni mpuuzi.
Bure kabisa.
 
Mkuu 'Kalunya', sasa nimekuelewa unachosema, lakini sikubaliani na msimamo wako.

Kwa hiyo, kwa maoni yako, kwa vile wakubwa 'wanapiga' na hawa wengine wote pamoja na uzalendo wao unataka na wao wageuke wawe wapigaji?
Mantiki ya namna hii uliiona wapi?

Unahimiza kila mtumishi aliye na nafasi, asitekeleze majukumu yake kwa uaminifu, kwa vile wakubwa wanapiga?
Unataka kila mwenye nafasi inayomwezesha kupiga, afanye hivyo, kwa sababu asipofanya hivyo, atastaafu akiwa maskini, na watu kama wewe mtakuwa mkimcheka kwa vile hakutumia nafasi yake kwa manufaa yake mwenyewe?

Haya ni mawazo ya kipuuzi kabisa.

Kama uovu unaofanywa na hawa viongozi juu ya nchi hii unakuumiza kama waTanzania wengine wote, huwezi kuja hapa na kushangilia maovu hayo hata kama ni kwa aina ya kukata tamaa kama unavyoonyesha wewe hapa.

Haya mambo ya uandishi wa kuzungukazunguka, ukionekana kushangilia uovu, kumbe nia yako ni kuumia kwa uovu huo, ni uandishi mbovu.

Sema wazi unachotaka kusema, usizunguke kama kusifu kumbe una maana ya kulaani.

Sasa unamulaumu nini huyo bosi hapo juu ambaye hata baiskeli hana, lakini analinda heshima yake na heshima ya nchi yake.

Wewe ni mmoja wa wapuuzi, na nimekuweka kwenye orodha hiyo hapa JF.

"KALUNYA", ni mpuuzi.
Bure kabisa.
Bwashee nalaani wizi kama upigaji wapige wote,kama ni mkanda wafunge wote.
Sio wachache wafunge mkanda juu washindane kulegeza,then fainali uzeeni nani atachekwa.
 
Wanabodi,

Niko Standby kuwaletea link ya uzinduzi huu.

====

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo ashiriki kwenye uzinduzi wa makala maalumu iitwayo ‘Royal Tour’ jijini New York nchini Marekani.

Makala hayo maalumu ambayo mchakato wake umefanyika kwa takribani mwaka mzima umemshirikisha moja kwa moja Rais Samia akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii nchini Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.

Uzinduzi huo wa aina yake unahudhuriwa na takribani watu 400 unafanyika kwenye Jumba Mashuhuri la Makumbusho liitwalo Guggenheim kuanzia saa moja na nusu za usiku za Marekani, sawa na saa nane na nusu usiku kwa Afrika Mashariki.

Miongoni mwa washiriki ni pamoja na wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, viongozi wa kisiasa, mashirika ya kimataifa, waandishi wa habari na Watanzania waishio Marekani.

Pia wafadhili na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za uhifadhi kama TANAPA, NCAA, TTB, TAWA, TFS na makundi ya wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Tanzania wakiwakilishwa na CTI, TBA, TPSF, TATO na CEOrt wahudhuria.

Shughuli hiyo inaoneshwa mubashara kupitia televisheni za Marekani kwenye mfumo wa utangazaji wa umma (PBS) kupitia kituo cha televisheni cha WTTS yenye watazamaji takribani milioni 3.5 na baadaye makala hayo itaoneshwa kwenye zaidi ya chaneli 300 zinazowafikia takribani asilimia 86 ya Wamarekani.

Makala hayo yatazinduliwa pia jijini Los Angeles, Aprili 21, mwaka huu na baada ya matukio hayo mawili, filamu hiyo pia itarushwa kwenye mtandao wa kidijitali wa Amazon na Apple TV.

Kwa Tanzania, filamu hiyo itazinduliwa kwanza jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili na baadaye visiwani Zanzibar tarehe 7 Mei.



Taarifa zaidi soma;

Uzinduzi wafanyika New York
Uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour umefanyika usiku wa kuamkia leo Aprili 19, 2022 Jijini New York Nchini Marekani na kuhudhuriwa na watu wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan.

Filamu hiyo maalumu ilitengenezwa kwa mwaka mzima ikimshirikisha Rais Samia kama mhusika mkuu akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii #Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na zaidi ya watu 400 katika Jumba la Makumbusho la Guggenheim, baadhi ya waliohudhuria ni wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, wanasiasa, mashirika ya kimataifa.

View attachment 2192524View attachment 2192525View attachment 2192528

View attachment 2192538
Paskali
DSM
Tanzania

Mbuga zipo Tanzania au Marekani? mambo ya hovyo kabisa
 
No sio kuhamasika bali hili ni tukio muhimu sana kwa taifa Letu. Kama huwa tunaletewa live za matukio less important, why not this very important?.
P
Lina umuhimu gani hili tukio? Unataka kuniambia mpaka karne hii hakuna juhudi zozote zilizofanywa kutangaza utalii wetu? Kama vivutio vyetu havijulikani Marekani mpaka karne hii! Hili ni la kushangaza.

Mara kadhaa mbuga ya Serengeti imeongoza kwa kuwa Mbuga bora ikishindanishwa na Mbuga nyingine, hili halikuvutia Watalii? kuna Channel kadhaa za Kimataifa zinaonesha Mbuga zetu tangu miaka mingi nyuma, haikusaidia? Au ushiriki wa Rais kwenye filamu hiyo ndiyo itawavuta Watalii?

Tumeambiwa fedha zilizotumika kuandaa si za Tanzania, je huyu aliyetoa hizo pesa katoa kwa Manufaa ya Tanzania? Anafaidika vipi? Kuna tathmini yoyote imefanyika ili kujiridhisha kama pesa zilizotumika kusafirisha kundi kubwa la Watu kwenda kwenye uzinduzi zitapatikana kupitia filamu hii?

Katika kufanya kitu kama hicho usitarajie sana kufanikiwa, endapo onesho hilo halitafanikiwa, gharama zitafidiwa vipi? Maana Watu wanaweza kuangalia na wasione jipya la kuwavutia kwenda Tanzania.

Tanzania ipo katika kipindi kigumu cha mfumuko wa bei, fedha zilizotumika kusafirisha Watu kwenda Marekani na kukaa kwa siku kadhaa zingeweza kutumika kama ruzuku kwenye baadhi ya bidhaa ili kupunguza mfumuko wa bei.
 
Mkuu Kambi ya Fisi , kila zama na zama zake, JPM sio tuu hakusafiri, bali pia alizuia wengine wasisafiri kwa lengo la kubana matumizi. Inawezekana kwake na kwako kusafiri ni kuzurura ovyo hivi Mama anavyo piga ma trips mnamuona kama ni kama anazurura ovyo!. No!. Kwanza kusafiri sio kuzurura, kuzurura ni kufanya safari zisizo na malengo, JPM alikuwa ni Inward person, hapendi kusafiri na kujichanganya na wenzake. Anapenda kujifungia ndani tuu.

Samia ni Outward person, outgoing kama JK, ni mtu wa kujichanganya na wenzake kubadilishana mawazo, uzoefu na kupata exposure.

Matokeo ya JPM kujifungia ndani, aliifunga na nchi, hakuwa na exposure hivyo kuna mambo alifanya kishamba. Sasa Samia anafungua nchi. Matokeo utayaona.
P
Samia kafungua nchi tayari, wapigaji wameshika hatamu, yaani wale wezi wa mali za umma na wahujumu uchumi wanakomba kwa raha zao. Mama anaendeleza yale ya Jakaya,ama kweli hizi ni zama zao
 
Bwashee nalaani wizi kama upigaji wapige wote,kama ni mkanda wafunge wote.
Sio wachache wafunge mkanda juu washindane kulegeza,then fainali uzeeni nani atachekwa.
Ulishaona wapi kitu kama hicho kinafanyika!

Typical 'Pascal Mayala' approach; popo si mnyama wala si ndege!

Watu wa aina yenu hamfai kwa lolote.
 
Pascal Leo ulichofanya nimekumbuka enzi za drive inn cinema,au pale empress cinema walivyoanzisha sinema za mpaka asubuhi kilichotokea no kwamba wale vipofu waliokuwa wanaombaomba madukani mchana ikifiKa usiku wanaeñda empress cinema ikawa ndio nyumbani kwao kulala,Sasa Mayalla mtu kama shaka anamsifu mama Toka Lumumba Huku cinema yenyewe yeye na hata wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM sio wateja walengwa wa hiyo makala.
 
Ulishaona wapi kitu kama hicho kinafanyika!

Typical 'Pascal Mayala' approach; popo si mnyama wala si ndege!

Watu wa aina yenu hamfai kwa lolote.
So wafaao ni wapigaji,au kwa sababu Hakuna sheria iwezayo mfunga fisadi, maana tunajua jela ni kwa ajili ya watu masikini walioiba kuku sababu hawana ya kumuhonga hakimu.
Ndugu Mimi binafsi sijapata Neema hio tu ya kuzikwapua, maana huu ni upumbavu unakusanya vipi Ili zikaliwe na wajanja juu,KILA mtu ale kwa urefu wa kamba.
Kama taifa limeamua kuwa la wapigaji ifahamike hivyo KILA mtu na apige kulingana na fimbo yake.
 
So wafaao ni wapigaji,au kwa sababu Hakuna sheria iwezayo mfunga fisadi, maana tunajua jela ni kwa ajili ya watu masikini walioiba kuku sababu hawana ya kumuhonga hakimu.
Ndugu Mimi binafsi sijapata Neema hio tu ya kuzikwapua, maana huu ni upumbavu unakusanya vipi Ili zikaliwe na wajanja juu,KILA mtu ale kwa urefu wa kamba.
Kama taifa limeamua kuwa la wapigaji ifahamike hivyo KILA mtu na apige kulingana na fimbo yake.
Naona tunazungushana bure 'mkuu wangu 'Kalunya'.

Nionavyo mimi, ni kama na wewe inakuumiza sana kuona hali mbovu iliyopo, lakini badala ya kuilaani moja kwa moja, inakuwa kama umekata tamaa, au ungependa na wewe uwe upande wa pili ili ufaidi?

Hayo mapapa yanayotunyonga hayastahiri hata kwa sekunde moja kusifiwa hapa, au kuonekana kuwa sisi tusiokuwa na nafasi hizo tutamani kuwa kama wao. Hawa ni watu wa kulaani, na katika kitabu changu ningependa kabisa pawepo na sheria ya kuyanyonga/kuyapiga risasi hadharani.
Sina chochote cha kutamani kutokana na vitendo vya wahujumu hawa wa taifa letu; na kamwe, siwezi kumlaumu mtu kama "lile li bosi linalopanda daladala" kwa kutotumia nafasi yake ili na yeye aendeshe gari zuri.
Hapa ndipo ninapoachana nawe kabisa.

Sasa angalia: Ni taifa lipi "limeamua kuwa la wapigaji"?
 
Naona tunazungushana bure 'mkuu wangu 'Kalunya'.

Nionavyo mimi, ni kama na wewe inakuumiza sana kuona hali mbovu iliyopo, lakini badala ya kuilaani moja kwa moja, inakuwa kama umekata tamaa, au ungependa na wewe uwe upande wa pili ili ufaidi?

Hayo mapapa yanayotunyonga hayastahiri hata kwa sekunde moja kusifiwa hapa, au kuonekana kuwa sisi tusiokuwa na nafasi hizo tutamani kuwa kama wao. Hawa ni watu wa kulaani, na katika kitabu changu ningependa kabisa pawepo na sheria ya kuyanyonga/kuyapiga risasi hadharani.
Sina chochote cha kutamani kutokana na vitendo vya wahujumu hawa wa taifa letu; na kamwe, siwezi kumlaumu mtu kama "lile li bosi linalopanda daladala" kwa kutotumia nafasi yake ili na yeye aendeshe gari zuri.
Hapa ndipo ninapoachana nawe kabisa.
Yeye kama atumii nafasi yake vizuri bahati haiji mara mbili wala Hakuna ujira au kuja kuzikwa na tuzo ya uadilifu wa uzalendo ajiandae tu na fedheha siku mfumo utakapo mtupa jongoo na uadilifu wake.
Kama toka juu wanaiba,wanalamba mikopo na misaada kisha wanamega zao wanaficha bank za Ulaya kwa faida zao binafsi.Sisi wadogo huo mwako wa kulipa kodi tutoe wapi. Sasa kama wanatoboa mtumbwi Ili kupata ubao wa kujisitiri wakati wa dhoruba hali tunazama wote kwann na sisi tusitoboe ubao, maana fainali uzeeni.
 
Back
Top Bottom