Iceberg9
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 24,565
- 47,011
Nimecheka pole sanaa, kipindi hicho maisha club ndiyo club pendwa watu wengi walikua wanapapenda sana, kulikua na swimming pool penmbeni pale basi kinyamwezi sana, umenikumbusha mbali sana,Aiseeee.. ni hatari sana. Hatari mno. Ila maisha club jamani. Ndo maana sipendagi outing za sehen kama hizo.
Kuna siku wanafunzi tukaenda. Uzuri ama ubaya wala pombe siziwezagi kwahiyo nakua sober tu nashangaa shangaa. Sasa kuna jamaa alikua na nyoka wake. Yule jamaa alikuta nimekaa naangalia pochi za wenzangu wanacheza mziki. Wengine wako counter kufata vinywaji. Alikua na nyoka wake kama watano hivi. Tukasalimiana. Nikajua ananifahamu labda. Tukawa tunapiga story. Ana american English bana naona ananichanganya akili yangu tu
Sindo akaanza ning'ang'ania anataka tuondoke? Sijui yule kaka ni anaishi usa ama maigizo na ngeli yake. Acha aanze kunivutaaa. Namwambia sikujui. Machozi almost kutoka. Kama fujo hv ikaanza. Nikaona kama wale nyoka nao wanataka lianzisha. Nikawaza wasije kuwa na silaha maana hawa ni manyoka. Jamaa haelewi anataka tuondoke wote. Ubaya hata sikumwuliza ni nani. Mbaya zaidi meza ile nalinda pochi za wenzangu. Machozi si yakanianza maana nguvu sina za kupigana. Good thing akatokea mkaka tunajuana na crew lake akaona akaja akanishika mkono. Yule kaka naye akapoa. Akameuliza are u with her akamjibu yes, she is my girl. Akawa mpole akamwambia cool man, am sorry. Jamaa akaondoka na nyoka wake. Nililiaaaaa sikuwahi kurudi tena maisha sijui 2009 ileee. Ila niliwaza kama wewe mambo ya viwembe. Maisha pa kishenz sana. Nilienda tu kwaajili ya jina
Dah ila pombe mbaya sana yani unaweza ukafanya jambo kwasababu ni pombe, kuna siku ingine ilitokea vurugu mule ndani nikajachukuliwa na mabaunsa nikawavimbia mabaunsa watu imeshiba kinoma lakini nilitaka nisimame nao mkono, wakanitupa kwenye ma vyungu nje kule, kuna wamasai walikua nje wakanisaidia kunipeleka kwenye tax maana nilikua hoi