Maendeleo mapya: Mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Uzalendo

Duuh,una elimu Gani kama unaipima katiba katka kipengele kimoja cha cha uchaguzi huru na haki tuu?VP uwepo wa serikali tatu,nguvu ya wananchi kuwajibisha viongozi,kupunguzwa kwa madaraka ya mkuu wa nchi,nk
Na ndipo ilipo tageti ya wanasiasa wa upinzani wao wanafikiria wakipata katiba itawapeleka Ikulu ..

sawa katiba ina vitu vingi lakini hatuwezi kuficha ukweli inaangaliwa kwa umakini kwenye mgawanyo wa madaraka na uchaguzi

hatuwezi kuepuka ilo.
 
Na ndipo ilipo tageti ya wanasiasa wa upinzani wao wanafikiria wakipata katiba itawapeleka Ikulu ..

sawa katiba ina vitu vingi lakini hatuwezi kuficha ukweli inaangaliwa kwa umakini kwenye mgawanyo wa madaraka na uchaguzi

hatuwezi kuepuka ilo.
Acha ulimbukeni wewe Katiba nzuri ya nchi ni nyenzo muhimu Sana ya kuendesha nchi Kwa utaratibu unaofaa.
Ndio tatizo la wanasiasa wapumbavu na wapuudhi kama wewe, katiba ni Mali ya wananchi wote na sio wanasiasa tu kwamba eti wanasiasa wa upinzani wataenda ikulu.
Una akili fupi Sana we kima utafikiria na wewe upo kwenye list ya dudu baya.
Katiba tuliyonayo ni ya hovyo sana na imepitwa na wakati.
Ukitaka kujua hilo rejea rasimu ya tume ya warioba.
Wewe lazima utakuwa huna marinda
 
Tufike sehemu tuwe wakweli kwa serikali za kiafrika hata tuwe na katiba nzuri kiasi gani sio suluhisho la matatizo yetu hasa kuna watu wanasema .

Tukipata katiba tutaweza kuwa na uchaguzi ulio huru thubutu hakuna kitu kama hicho na hakitakaa kitoke

Matatizo ya uchaguzi ni busara za vyombo vya ulinzi na usalama wa nchi na utashi wa viongozi waliopo madarakani

Kama mnabisha angalia uchaguzi wa mwaka 2017 nchini kenya Mpaka kijana mmoja mzalendo wa tume ya uchaguzi IEBC alikatwa kiganja ili tu Uhuru Kenyatta aendelee kuwa madarakani

Kenya ndio nchi yenye katiba bora kuliko nchi zote barani africa lakini kilichotokea mwaka 2017 ilikuwa ni ubakaji wa democrasia waziwazi.

angalia Marekani mwaka 2016 Trump alizidiwa popular votes million 3 lakini mpaka sasa eti yupo ikulu sijui anawakilisha wananchi wapi upuuzi mtupu.

tufike sehemu tuwe wakweli hata kama tungetengeneza katiba ya namna gani kama hakuna utashi wa watawala na watu wa usalama kama police na jeshi hawajaamua kuwa wazalendo na kuacha kutumikishwa na wao kuwa na wagombea hasa africa tutaendelea kupiga kelele mpaka kiama ..

Hivi unategemea mtu kama Magufuli akupe katiba mpya halafu akuruhusu kwenda IKULU?
nani kasema anataka katiba mpya ili ituletee maji na barabara??kuna mtu kasema anahtaji katiba mpya ili iboreshe huduma za kijamii??ni wapi ulisikia mtu anadai katiba mpya ili itujengee viwanda??? constitution is the body which governs the state,tunahtaji katiba ambayo itaweka mifumo na misingi ili rais atakayepatikana awe kichaa au timamu misingi ndyo im'shape
 
..Ghana wana demokrasia madhubuti.

..Wanabadilisha serekali bila matatizo.

..Tujitahidi tuwakaribie na hata kuwazidi.

..Ninaamini Mwalimu aliposema tunahitaji siasa safi ili tuendelee, ktk mazingira ya sasa hivi siasa safi zinategemea katiba bora na utawala wa demokrasia.

..Tukiondokana na mikwaruzano ya demokrasia tutapata muda mwingi zaidi wa kujielekeza kwenye maendeleo.
 
Na swali moja tu. Alichofanya Jecha alifuata katiba au hakufuata katiba? Baada ya hapo urudi uniambie umuhimu wa kubadilisha katiba kwenye Jamii ambayo haifuati wala kuitetea hiyo katiba inapovunjwa.
 
Hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu.hata hiyo iliyopo imeamriwa kutoka juu.
Mamlaka zinatoka kwa Mungu lakini applications za mamlaka zaweza kuingiliwa na mashetani. Mfano ni Nebuchadnezzar, Hitler na IDD Amin Dada

Hata iliyoko yaweza kuingiliwa
 
Mamlaka zinatoka kwa Mungu lakini applications za mamlaka zaweza kuingiliwa na mashetani. Mfano ni Nebuchadnezzar, Hitler na IDD Amin Dada

Hata iliyoko yaweza kuingiliwa
Hili andiko wengi huwa wanalichukulia literally. Ile mamlaka ya utawala ni Mungu ameiweka na anakuwa anaweka vipawa kwa watu fulani ili waongoze nchi kwa mafanikio.

Kinachotokea ni kuwa watu wengi wanaotaka kutawala wanakwenda kwa waganga na wasoma nyota ambao wamewezeshwa na shetani kutambua vipawa vilivyomo ndani ya watu (nyota).

Ndipo mganga anapoyatuma mashetani kuiba vipawa na kuwawekea watu wanaowaendea. Hayo yanahusisha mikataba ya kuua watu, watoto na mambo yanayofanana na hayo.

Kimsingi watawala hao wanakuwa wanatembelea nyota za watu. Ndio maana ya andiko linalosema shetani ni mwizi, anaiba vitu vya rohoni.
 
Ni sawa na kusema watu wote ni wa MUNGU lakini kuna wanaotenda matendo ya kishetani
 
Na swali moja tu. Alichofanya Jecha alifuata katiba au hakufuata katiba? Baada ya hapo urudi uniambie umuhimu wa kubadilisha katiba kwenye Jamii ambayo haifuati wala kuitetea hiyo katiba inapovunjwa.
Jecha! Mhuuu,Alifuata katiba lakini alivunja sheria.Maana ili ufute uchaguzi ni lazima uwe na vigezo ,kikibwa chao iwe upigaji kita uligubikwa nafujo ,mauwaji,upotevu wa visanduku na au lolote lilisababishwa mchakato wa kupiga kura na kuhesabu usifanyike.Tena ili ufute uchaguzi iwe hali hii ni kwa nchi nzima.siobaadhi ya vituo.
Hivyo alivyoamua jecha bila vigezo hivyo ni wizi wa mchana kiba kwa ajili ya maslahi ya chama fulani dhidi ya kingine ambayo kwa mujibu wa sheria ni jinai.
Lakini katiba inampa nguvu kuwa maamuzi yake ni ya mwisho hayahojiwi mahakamani.Hata kama ni batili hashtakiwi.
Hapoooooo ndipo palipo na ulazima wa kuitafuta katiba kwa hali na mali na kwa maana hiyo ni bora kutoshiriki chaguzi zifuatazo mpaka katiba ibadilike,kinyume chake ni kuumizana na kutiana vilema au kupotezeana uhai.
Au tupambane kwa nia hiyo kufa kupona mpaka kieleweke kuliko kukimbizana kwenye mikutano na kampeni za siasa tukiamini eti ccm itajitia kitanzi yenyewe kuachia madaraka kwa hiari.
 
Mamlaka zinatoka kwa Mungu lakini applications za mamlaka zaweza kuingiliwa na mashetani. Mfano ni Nebuchadnezzar, Hitler na IDD Amin Dada

Hata iliyoko yaweza kuingiliwa
, xz,,,*__**,_,*_†,,*"__†"__''. X. Z , f ccxxzxxzxxxçxxxcxxzl ccfzZcvcvvvçvçc vccl f
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom