New Israeli gov’t approves right-wing march through Jerusalem

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Oct 26, 2018
21,713
35,512
Palestinian Prime Minister Mohammad Shtayyeh describes the planned march through occupied East Jerusalem as ‘a provocation of our people’.



Naftali Bennett Once said "West Bank is not under occupation because “there was never a Palestinian state here,".

Israeli far-right groups are expected to participate in a so-called “March of the Flags” through the Damascus Gate of occupied East Jerusalem’s Old City and into its Muslim quarter on Tuesday, drawing warnings from Hamas of renewed hostilities should it proceed.

Heavily armed paramilitary border police and other forces patrolled the streets of the city, set up checkpoints, and blocked off roads throughout East Jerusalem. Iron barriers were placed outside the entrance to Damascus Gate, where Palestinians said they would gather to confront the Israelis.

The Israeli military has deployed Iron Dome air defense batteries and raised its level of alert ahead of the Jerusalem Flag March on Tuesday, as Hamas says it would respond to the right-wing march if it goes through as planned, potentially with rocket fire from the Gaza Strip.

Israel’s new government approved the controversial march by right-wing nationalists and pro-settler groups on Monday, a step that risks inflaming tensions with Palestinians, hours after Benjamin Netanyahu handed over power to Prime Minister Naftali Bennett.

The move came as tensions remain high in occupied East Jerusalem over Israel’s planned forced displacement of Palestinian families from the neighbourhood of Sheikh Jarrah, just north of the Old City.

It also comes as a fragile ceasefire is holding in the besieged Gaza Strip following Israel’s 11-day military bombardment of the enclave, which killed 253 people – including 66 children. At least 13 Israelis were killed by rockets fired by Palestinian armed groups in Gaza during the escalation in violence.

Palestinian factions in the occupied West Bank have called for a “Day of Rage” against the march. Last month, Israeli crackdowns on protesters at the Al-Aqsa Mosque compound left hundreds of Palestinians wounded.

“This is a provocation of our people and an aggression against our Jerusalem and our holy sites,” Palestinian Prime Minister Mohammad Shtayyeh said of the march.

After meeting with Israel’s police chief and other security officials, newly sworn-in Internal Security Minister Omer Barlev approved the march and said police were well prepared, according to a statement carried by the Israeli media.

“[Great] efforts are being undertaken to preserve the delicate fabric of life and public security,” Barlev was quoted as saying.

It was not clear whether participants would be allowed to enter the Old City’s Muslim quarter, on a route that Israeli police had previously barred. An original march on May 10 was rerouted at the last minute as tensions in Jerusalem had escalated.

Israeli rightists accused the government of caving into Hamas by changing its route. They rescheduled the procession after an Egyptian-mediated Gaza truce took hold.

A new route change or cancellation of the procession could expose Bennett’s patchwork coalition to accusations from Netanyahu, now in the opposition, and his right-wing allies of giving Hamas veto power over events in Jerusalem.

“The time has come for Israel to threaten Hamas and not for Hamas to threaten Israel,” prominent far-right lawmaker Itamar Ben-Gvir said on Twitter.

The march poses an immediate challenge for Bennett’s government, which was approved on Sunday by a 60-59 vote in parliament.
Suggesting that a route adjustment could be in store, Yoav Segalovitz, a deputy internal security minister, said past governments had stopped nationalists from visiting Muslim sites in times of tension.

NADHANI MMEANZA KUMUELEWA NAFTAL BENNETT NI MTU WA NAMNA GANI.


Now Jerusalem will be returned to its rightful OWNER

MUDA NI MWALIMU MZURI​

Screenshot_20210615-132342_Chrome.jpg
 
Hili jukwaa lina participants Wengi saana chagua kuleta habari nyingine au tazama zingine maana zipk nyingi sana.


Samahani kama hizi zinakukera
Hizi za Israel, Palestina na Iran ndio nyingi kuliko hizo nyingine ndo maana nimesema. Zinanikera kweli lakini nitafanyaje sasa ndio uhuru wenyewe huu.
 
Tangu angano la kale mji wa Yerusalem ulikuwa ndiyo makao makuu ya nchi ya Uyahudi

Waparestina (wafilisiti) kazi mnayo!!
Saana na jamaa alishaapa waendelea kujenga na kuwaondoa waarabu wote hapo Jerusalem
 
Hizi za Israel, Palestina na Iran ndio nyingi kuliko hizo nyingine ndo maana nimesema. Zinanikera kweli lakini nitafanyaje sasa ndio uhuru wenyewe huu.
Mkuu mbona zipo nyingi tu sema akili yako ipo attached na hizi ndio maana unaziona zaidi ya nyingine, zipo za Kongo, Uganda,

India na covid

china na nuclear arsenal

Uchaguzi wa Iran

Na nyingine nyiiingi pitia headings za hili jukwaa ujionee
 
. Dunia lazima iangalie nani ataanza kurusha maroketi. Dunia lazima iangalie kuwa HAMAS hawezi kuwa amrisha taifa huru la israel lisifanye sherehe ya kurusha bendera.Maajabu hakuna hata nchi moja ya kiarabu ambayo imeionya hamas kurusha maroket. Uturuki na Arab League wote zimekaa kimya tuu kungoja kuandamana HAMS akipigwa!!!!Uongozi mpya wa Israel una mawaziri wawili ambaop walijiuzuru nafasi zao za uwaziri wa ulinzi kwa sababu BIBI alikataa wasiivamie Gaza na kuiteketeza HAMAS. Libeman, na Naftal benet wananiku,busha enzi za menahem begin na Ariel Sharon.
 
Saana na jamaa alishaapa waendelea kujenga na kuwaondoa waarabu wote hapo Jerusalem
mji wa Jerusalem ni wa taifa la Israel na wana haki yote kumiliki ardhi ile. hawa wapalestina wanataka kuweka Sharia law ili wakristu wakienda hija pale watengwe na kujiona pale jerusalem sio pao. angalia Gaza hivi sasa kuna sharia law kama ilivyo jimbo la Kano, kaduna na mji wa khartoum.
 
mji wa Jerusalem ni wa taifa la Israel na wana haki yote kumiliki ardhi ile. hawa wapalestina wanataka kuweka Sharia law ili wakristu wakienda hija pale watengwe na kujiona pale jerusalem sio pao. angalia Gaza hivi sasa kuna sharia law kama ilivyo jimbo la Kano, kaduna na mji wa khartoum.
Huyu Bennett atawanyoosha tu
 
Palestinian Prime Minister Mohammad Shtayyeh describes the planned march through occupied East Jerusalem as ‘a provocation of our people’.



Naftali Bennett Once said "West Bank is not under occupation because “there was never a Palestinian state here,".

Israeli far-right groups are expected to participate in a so-called “March of the Flags” through the Damascus Gate of occupied East Jerusalem’s Old City and into its Muslim quarter on Tuesday, drawing warnings from Hamas of renewed hostilities should it proceed.

Heavily armed paramilitary border police and other forces patrolled the streets of the city, set up checkpoints, and blocked off roads throughout East Jerusalem. Iron barriers were placed outside the entrance to Damascus Gate, where Palestinians said they would gather to confront the Israelis.

The Israeli military has deployed Iron Dome air defense batteries and raised its level of alert ahead of the Jerusalem Flag March on Tuesday, as Hamas says it would respond to the right-wing march if it goes through as planned, potentially with rocket fire from the Gaza Strip.

Israel’s new government approved the controversial march by right-wing nationalists and pro-settler groups on Monday, a step that risks inflaming tensions with Palestinians, hours after Benjamin Netanyahu handed over power to Prime Minister Naftali Bennett.

The move came as tensions remain high in occupied East Jerusalem over Israel’s planned forced displacement of Palestinian families from the neighbourhood of Sheikh Jarrah, just north of the Old City.

It also comes as a fragile ceasefire is holding in the besieged Gaza Strip following Israel’s 11-day military bombardment of the enclave, which killed 253 people – including 66 children. At least 13 Israelis were killed by rockets fired by Palestinian armed groups in Gaza during the escalation in violence.

Palestinian factions in the occupied West Bank have called for a “Day of Rage” against the march. Last month, Israeli crackdowns on protesters at the Al-Aqsa Mosque compound left hundreds of Palestinians wounded.

“This is a provocation of our people and an aggression against our Jerusalem and our holy sites,” Palestinian Prime Minister Mohammad Shtayyeh said of the march.

After meeting with Israel’s police chief and other security officials, newly sworn-in Internal Security Minister Omer Barlev approved the march and said police were well prepared, according to a statement carried by the Israeli media.

“[Great] efforts are being undertaken to preserve the delicate fabric of life and public security,” Barlev was quoted as saying.

It was not clear whether participants would be allowed to enter the Old City’s Muslim quarter, on a route that Israeli police had previously barred. An original march on May 10 was rerouted at the last minute as tensions in Jerusalem had escalated.

Israeli rightists accused the government of caving into Hamas by changing its route. They rescheduled the procession after an Egyptian-mediated Gaza truce took hold.

A new route change or cancellation of the procession could expose Bennett’s patchwork coalition to accusations from Netanyahu, now in the opposition, and his right-wing allies of giving Hamas veto power over events in Jerusalem.

“The time has come for Israel to threaten Hamas and not for Hamas to threaten Israel,” prominent far-right lawmaker Itamar Ben-Gvir said on Twitter.

The march poses an immediate challenge for Bennett’s government, which was approved on Sunday by a 60-59 vote in parliament.
Suggesting that a route adjustment could be in store, Yoav Segalovitz, a deputy internal security minister, said past governments had stopped nationalists from visiting Muslim sites in times of tension.

NADHANI MMEANZA KUMUELEWA NAFTAL BENNETT NI MTU WA NAMNA GANI.


Now Jerusalem will be returned to its rightful OWNER

MUDA NI MWALIMU MZURI​

View attachment 1819355
Yu karibu malangoni.
 
Yu karibu malangoni.
JE! NI MAPEMA KIASI GANI YESU ATARUDI?

Baada ya Yesu kuwaahidi wanafunzi wake kwamba angekuja tena katika ulimwengu huu kwa mara yake ya pili (Mathayo 23:39), je! ni swali gani walilomwuliza?

"Tuambie,' wakasema, 'mambo hayo yatatokea lini, tena, patakuwa na dalili gani ya kuja kwako, na ya mwisho wa dunia?" - (Mathayo 24:3).

Yesu alijibu waziwazi na pasipo shaka lo lote. Katika sura ya 24 ya Mathayo na sura ya 21 ya Luka yeye mwenyewe aliwapa "ishara" kadhaa, au ushahidi, ambao kwa huo sisi tunaweza kujua kuja kwake kunapokaribia. Unabii mwingine wa Biblia unasaidia kuijazia picha hiyo, unaonyesha kwa kinagaubaga hali ya dunia hii itakavyokuwa kabla tu ya kurudi kwake Kristo.

Kama tutakavyoweza kuona, unabii huo unaendelea kutimia kabisa mbele ya macho yetu; unaonyesha kwamba kuja tena kwa Kristo kumekaribia sana.

Hebu na tuziangalie ishara kumi za unabii wa Biblia zilizo katika njia ile kuu ya kwenda mbinguni.

Ishara ya (1) - DHIKI!HOFU NA MFADHAIKO!

"Tena, kutakuwa na ishara katika jua, na mwezi, na nyota; na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake; watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika. Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi. Basi mambo hayo yaanzapo kutokea changamkeni mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia" - Luka 21:25-28.

Hakuna maelezo yaliyo sahihi zaidi juu ya dunia yetu ya leo kama yalivyo maneno haya: 'Watu watazimia kwa hofu, wakitazamia mambo yatakayoipata dunia hii." Silaha kali zilizolundikana zina uwezo wa kuiteketeza sayari hii ...Yesu anatupa sisi msingi wa kuwa na tumaini katika kizazi hiki chenye maafa makubwa. Hali iliyopo sasa ya hatari inayoikabili dunia hii nzima itakayoleta "dhiki na mfadhaiko" inautilia tu nguvu ukweli usemao kwamba kuja kwake Kristo "kunakaribia." Watu siku hizi huomboleza mara kwa mara na kukata tamaa, wakisema, "Tazama ilivyo dunia hii!" Lakini mwanafunzi wa unabii wa Biblia anaweza kusema ghafla kwa sauti iliyojaa matumaini, akisema, "Tazama, NI NANI HUYO ajaye katika dunia yetu."

Ishara ya (2): MAAAFA KATIKA DUNIA HII

Je! maafa haya ya asili yanaingiaje na kukubaliana na matukio ya siku za mwisho?...."Kutakuwa na MATETEMEKO makubwa ya nchi, na njaa na TAUNI mahali mahali, na mambo ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni… Nanyi kadhalika mwonapo mambo hayo yanaanza kutokea, tambueni ya kwamba UFALME WA MUNGU U KARIBU" (Luka 21:11,31).

Hebu fikiria habari za njaa kwa dakika moja. Picha za watoto wanaokufa kwa njaa wenye matumbo yaliyovimba huendelea kutangazwa katika habari. Je!hilo si jambo la kushangaza sana kwamba dunia hii inayoweza kuwatuma watu mwezini, HAIWEZI kuwalisha watu wake wote? Yesu alijua kwamba njaa ingeendelea kuwako, kwamba tabia ya uchoyo ya kibinadamu ingezidi kuwa mbaya zaidi na zaidi karibu na ule mwisho wa wakati.

Lakini, je! vipi kuhusu hayo matetemeko ya nchi? Kwa mujibu wa World Almanac ya 1999, karne baada ya karne za kipindi hiki cha kikristo pamekuwa na ongezeko la kustaajabisha la matetemeko makubwa ya nchi: karne ya kumi na nane palikuwa na matetemeko makubwa ya nchi 6; karne ya kumi na tisa yalikuwa 7; karne ya20 yalikuwa zaidi ya 100. Kwa hiyo ushahidi unazidi kuwa wa kuvutia zaidi na zaidi kadiri tunavyokaribia kuzifikia siku hizi zetu.

Takwimu hizo zinauthibitisha unabii ule alioutoa Yesu. Njaa na matetemeko makubwa ya nchi yanazidi kuongezeka taratibu - yakisema, "ufalme wa Mungu umekaribia!"

Ishara ya (3): KUJILIMBIKIZIA MALI

Hivi maana yake ni nini kwamba utajiri unateleza na kuingia katika mikono ya watu wachache kwa wingi zaidi na zaidi, huku watu wengi zaidi na zaidi wakizidi kuwa maskini?.."Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho" - (Yakobo 5:3).

Licha ya ujuzi wetu wote wa uchumi, matajiri wanazidi kuwa matajiri, na maskini wanazidi kuwa maskini. Utajiri wa kuwa na mamilioni mengi ya dola [za Kimarekani] ni -ishara nyingine ituonyeshayo kwamba "kuja kwake Bwana kunakari

Ishara ya 4 -MISUKOSUKO YA KIRAIA

Kwa nini hali hii ya kutoridhika na misukosuko miongoni mwa wafanyakazi imeongezeka kwa namna inayojionyesha wazi mno?
"Angalieni! Ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu ninyi mliouzuia kwa hila unapiga kelele dhidi yenu na VILIO VYAO VYA WALIOVUNA vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi… Nanyi vumilieni mthibitishe mioyo yenu kwa maana KUJA KWAKE BWANA KUNAKARIBIA" - (Yakobo 5:4,8).

Baada ya kutabiri dhidi ya kujilimbikizia mali nyingi zisizo na idadi katika siku hizi zetu, Yakobo aliona misukosuko ya watu ikitokana na wafanyakazi wasioridhika. Migogoro iliyopo kati ya wale"walio nacho" na wale "wasio nacho" inazidi kuongezeka. Hiyo ni ishara nyingine inayoonyesha kwamba "kuja kwake Bwana kunakaribia."

Ishara ya (5): MMOMONYOKO WA MAADILI

Mbona uzi wa maadili ya jamii unaonekana kana kwamba unakatika vipande vipande?
"Lakini ufahamu neno hili; ya kuwa siku za mwisho kutakuwako na NYAKATI ZA HATARI. Watu watakuwa wakijipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasio wapenda wa kwao, wasiotaka suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu - wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake hao nao ujiepushe nao.... LAKINI WATU WABAYA NA WADANGANYAJI WATAENDELEA, NA KUZIDI KUWA WAOVU, wakidanganya na kudanganyika" - (2 Timotheo 3:1-5,13).

Je! kuna mtu ye yote ambaye angeweza kufikiria na kutoa maelezo yaliyo sahihi zaidi ya hayo kuihusu hii dunia yetu? Hebu elekeza kamera yako upande wo wote katika hizi siku tulizo nazo, nawe utapiga picha inayoonyesha ufedhuli utokanao na ile tamaa ya kupenda anasa za ulimwengu huu. Utainasa picha ya kushtua inayoonyesha ukatili wa kuwatenda vibaya watoto wadogo, pamoja na maudhi yanayoletwa kwa makusudi mazima. Utapata matukio mengi yasiyo na idadi ya vijana wasioweza kudhibitika kabisa, pamoja na watoto walio katika ule umri wa miaka ya mwanzo ya ujana wao, yaani, kuanzia miaka kumi na mitatu na kuendelea juu kidogo, ambao wanawaua watu ovyo ovyo na kuwafanya watu vilema. Mambo hayo yote yanajenga chumba kidogo kirefu ambacho kinaonyesha picha zinazotangaza kwa sauti kuu kwamba kuja kwake Yesu kumekaribia sana.

Ishara ya (6): KUENEA KWA DINI ZA UONGO (Kiinimacho)

Hivi kwa nini tunauona mlipuko wa kupendezwa sana wa dini za kibabeli miongoni mwa watu?
"Kwa maana watatokea wakristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu [miujiza] wapate kuwapoteza kama yamkini hata walio wateule" -(Mathayo 24:24).

Vifungu hivi vya maneno vinatabiri kwamba wakati huu wa mwisho itaonekana miujiza ya kila namna, pamoja na ishara, yaani maonyesho ya bandia ya uwezo usio wa kawaida kwa wanadamu. Wanawake wachawi na wanaume wachawi wafanyao uchawi wataonekana katika maonyesho mbalimbali[mikutano ya kidini wakijiita Manabii,mitume, Maaskofu nk] wameshika Biblia wakizungumza na huku wanataja Jina la Yesu ,Hayo yote huyafanya mambo yawe wazi zaidi kama Yesu alivyotabiri kwamba sisi tunaishi katika kipindi cha "kuja kwake Mwana wa Adamu" (fungu la 27.)

Ishara ya (7) - Dunia Iliyozinduka

Huko kuzinduka kunakohusu mambo ya dunia hii kunamaanisha nini kwa Afrika, Mashariki ya Kati, Ulaya Mashariki, na kwa matatifa yale ya Mashariki ya Mbali?
"'MATAIFA NA WAJIHIMIZE;… haya utieni mundu, maana mavuno yameiva… kwani uovu wao ni mwingi sana!' Makutano makubwa, makutano makubwa, wamo katika bonde la kukata maneno [kuamua mwisho wa kila mtu]" - (Yoeli 3:12-14).

Leo hii katika nchi za Asia na Afrika, Ulaya Mashariki, Muungano wa Zamani wa Kisovieti, na nchi za Mashariki ya Kati, huenda sisi tunashuhudia kuona mwamko mkubwa sana wa taifa moja moja katika historia yote iliyopata kuandikwa, "kwa maana siku ya BWANA I KARIBU."

Ishara ya (8) - MIPANGO YA AMANI NA MAANDALIZI YA VITA

Tunaishi katika ulimwengu huu wa ajabu. Kila mmoja anaafiki kwamba tungeipatia nafasi amani; lakini basi, zile chuki zilizokandamizwa kwa kipindi cha karne fulani zilizopita, zinalipuka na kuwa vita ya wazi. Nabii Mika na Yoeli walitabiri kwamba wakati ule ule mataifa yatakapokuwa yanasema juu ya shauku yao ya kuwa na amani (Mika 4:1-3) watalazimika kujiandaa kwa VITA kutokana na shauku yao waliyo nayo dhidi ya majirani zao (Yoeli 3:9-13).

Zamani sana Biblia ilionyesha picha hii ya mgogoro wetu wa sasa wa kuwa na amani au vita, kisha ikatangaza kwamba amani ya kudumu itatawala katika dunia hii wakati ule tu Yesu atakapokuja.

Ishara ya (9 ) MAENDELEO YA KISASA

Mbona usafiri na mawasiliano vimeuleta ulimwengu huu kuwa karibu mno baada ya karne nyingi za historia ya wanadamu?
"HATA WAKATI WA MWISHO, wengi wataenda mbio huko na huko maarifa yataongezeka" - (Danieli 12:4).

Hapo Danieli anadokeza kwamba maarifa ya kuuelewa unabii wake yataongezeka "katika" (KJV), au "hata wakati wa mwisho." Lakini utabiri huo pia unaonekana kana kwamba unasonda kidole chake kwenye kizazi chetu hiki kilichoyaweka maarifa katika kompyuta. Maarifa ya kila namna yameongezeka kwa kasi kubwa inayolandana na umeme katika miaka hii michache iliyopita. Pamekuwako na mabadiliko mengi sana katika kipindi cha miaka hamsini iliyopita kuliko katika kipindi kile cha miaka elfu mbili kabla yake.

"WENGI WATAENDA HUKU NA KULE kuongeza maarifa." Kabla ya mwaka ule wa 1850, watu walisafiri kwa magari yaliyovutwa na farasi, ikiwa karibu sawa kabisa na vile ilivyokuwa tangu mwanzo wa wakati. Hivi sasa tunasafiri kasi kuliko sauti na kuizunguka dunia hii kwa ndege za konkodi (concorde) hata kwa roketi za safari fupi katika anga za juu.

Ongezeko la safari na gharika ya uvumbuzi ya hivi karibuni hutoa ushahidi mwingine zaidi kuonyesha kwamba sisi tunaishi "katika siku za mwisho."

Ishara ya (10) - INJILI ULIMWENGUNI KOTE

Yesu alitabiri kwamba, muda mfupi tu kabla ya kuja kwake, injili ingefika katika ulimwengu wote:
"Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote, hapo ndipo ule mwisho utapokuja" - (Mathayo 24:14).

Kwa miongo mingi [makumi mengi ya miaka] karibu nusu ya dunia hii ilikuwa imefungiwa nyuma ya pazia la chuma, ilifungiwa mbali na ile Habari Njema. Lakini baadaye, karibu kwa usiku mmoja Ulaya Mashariki iliteleza kutoka katika kubanwa na chuma cha Ukomunisti. Ukuta wa (Berlin) ukaanguka chini na kuvunjika vipande vipande, na ile dola yenye nguvu nyingi ya Kisovieti ikasambaratika. Ghafla karibu nusu ya sayari hii ilikuwa ikinyoosha mikono yake ili kuipokea injili.

Injili hii inakwenda katika "ulimwengu wote" kwa namna isivyopata kufanyika katika siku zile za nyuma. Kwa njia ya Satelaiti ujumbe wa Kikristo kwa wakati uo huo unaendelea kutangazwa karibu kwa kila taifa. Tunaishi katika kipindi kile kile hasa ambacho Yesu alisema habari zake alipotangaza hivi: "Injili hii itahubiriwa katika ulimwengu wote
...........
Baada ya kuyaelezea yale matukio yaliyokusudiwa kuonyesha kipindi kile kinachotangulia muda mfupi tu kabla ya kuja kwake mara ya pili, Yesu anahitimisha maneno yake kwa kusema hivi,
"Amini nawaambia, kizazi hiki hakika hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia " - (Mathayo 24:34).

Hitimisho hilo ni dhahiri - yaani, kizazi hicho kilichodokezwa kwa kwa-ishara za unabii ndicho kitakachojaliwa kumwona Yesu akirudi duniani mara ya pili. Muda hautakuwa mrefu hadi hapo atakapoifagilia mbali dhambi na mateso, na kuusimika ufalme wake ule wa milele. Yesu anatutahadharisha sisi, anasema, "Hakuna aijuaye.. siku ile au saa ile" (fungu la 36.)

Tena, Yesu anaendelea kusema hivi:
"Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja" - (Mathayo 24:44)

Mwokozi wetu alitayarisha njia ya kututoa kutoka katika dunia yetu hii inayovunjika-vunjika kwa kutoa kafara mwili wake na damu yake. Na Yesu yule yule, ambaye siku moja atayaponya magonjwa ya dunia hii kwa kuiteketeza dhambi
["Atendaye dhambi [avunjaye Amri Kumi] ni wa Ibilisi, kwa kuwa Ibilisi amekuwa akitenda dhambi [akizivunja Amri Kumi - Yn. 8:44) tangu mwanzo. Sababu ya kuja kwa Mwana wa Mungu ilikuwa ni kuzivunjilia mbali kazi za Ibilisi" - (1 Yohana 3:8)]
, hivi sasa anakupa wewe haki yake inayoifutilia mbali hatia ya dhambi katika maisha yako. Huna haja ya kungoja mpaka siku ya kuja kwake mara ya pili ili upate kuwekwa huru mbali na hatia yako na mbali na wasiwasi wako pamoja na ile tabia yako ileayo uharibifu. Yesu yu tayari sana kukupa wewe amani yake katika dakika hii hii.
FB_IMG_1623897078831.jpg
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom