New Age: Dini mpya ya ulimwengu

Jibu swali_nyakati za kwanza ulikuwepo..?

Utoto ni huo wa kuotaota nyakati zimeisha

We unajuaje kama labda ndio kwanza tunaanza..!?

ManchoG
Hahaha ....safi sana ...eti wanaambiwa nyakati zimeisha ..mbaya zaidi waweza kukuta hata binaadamu aliyeishi miaka 2000iliyopita alikuwa anaamini hivi hivi kuwa nyakati zimeisha lakini ndio kwanza watu wanazidi kufa nakuzaliana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu aliye hai yupi? Yeye alitokea wapi, kwani kuna wengine waliokufa?

Ni dini gani inakupeleka kwa huyu Mungu aliye hai wakati yeye mwenyewe hakuna dini aliyoshusha kutoka ili tuiabudu.

Ni hukumu gani atatupa sisi tuliokengeuka na kukataa kanisa na misikiti. Wanasema tutachomwa moto milele, kuna moto gani unaweza kuchoma roho?

Unasema hii dini mpya asili yake ni shetani inatupeleka mbali na Mungu, kwani hujui kuwa siku nyingi tuko mbali na mungu shetani ndiye mtawala wa hii dunia? Jehova na kina Alah washaiacha siku nyingi hii dunia wako huko kwenye solar system ingine na shughuli zao.

Kwanini huyu Mungu aliyetuumba atupe akili ndogo kiasi kwamba tushindwe kujua chanzo chake yeye au mwanzo wake maana kwa akili alizotupa tunajua hakuna kiti kisicho na mwanzo wala mwisho, je mwisho wake yeye ukifika sisi viumbe alivyotuumba tutakuwaje ?
Hahaha nasubiri Majibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaongea kuhusu new age and yet unasema chanzo chake ni ubudha na uhindu na chinese traditions

Unajua how old are those civilization?

How old are the Christian and islamic religion?


Sent using Jamii Forums mobile app
Huyu jamaa kapuyanga sana .... yaani laiti kama angelijua kuwa dini za budha na hindu ni dini enyeji duniani basi nadhani angekubaliana. Nami bila shaka kuwa uislam.na ukristo ndio new Ages alizozisema ..dini hizo zinazaidi ya miaka 4000 wakati dini zake za uislam na ukiristo ni za juzi juzi tu kama ukiristo ni miaka 2000 uislam hata miaka 1800 hauna...ila kwakuwa haujui ngoja tumuache

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Namaanisha huyo huyo anayeitwa BWANA_ambaye wakati anaumba hakuwa na mshauri yeyote

Yeye bila shaka ndiye shetani mkuu huyo mwengine geresha tu_umenipata..?

ManchoG
Yeahh yeahh ....haiwezekani uwaumbe binaadamu na wanyama uwaumbie shetani na kila aina ya mabalaa magonjwa vipunga vita na matetemeko

Halafu useme kuwa wewe huna hatia ..mbaya zaidi ubaya unampachika shetani kuwa yeye ndiye mbaya wkati unajinadi kuwa wewe ndiye uliyemuumba ...ebo sasa kwanini usingeuzuia ubaya wake kwa kuto muumba . .kwanini baada ya kumuumba usinge muangamiza " maana tayari ulikuwa unajua kwamba umekiumba kiumbe kitakacho kuja kuleta kero kwa binaadamu ... wakati huo huo unajinadi kuwa wewe ni muweza wa yote .upendo kwa wote .mjuzi wa kila kitu "

(1)Sasa mbona umeshindwa kuutumia ujuzi wako wa yote kutambua kuwa utakiumba kiumbe ambacho kitakuja kuleta shida kwa binaadamu duniani

(2) je kama ulikuwa unajua kuwa unakiumba halafu kitakuja kuleta shida
Kama tukisema kwamba huna ule upendo kwa wote kama unavyo jinadi tutakuwa na makosa ...haingii akilini uwe naujuzi wa yote ..upendo wa yote 'halafu uumbe kiumbe ambacho kinakuja kuwa umiza binaadamu ambao unajinadi kuwa unaupendo nao tena kwa wote (haha)

(3) Bado inafikirisha kuona mjuzi wa yote akiwa ameacha kutumia ujuzi wake kupambana.na shetani halafu ameamu kuwaachia binaadamu. Ndio wamsaidie kupambane nae " inastaajabisha " sana




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuhusu mambo ya cults naweza kukubaliana na wewe. Lakini ulipotaja Buddhism na Hindu etc hapo ndo ninapo pingana na wewe. Hizi dini kazisome vizuri sio za kishetani kama ulivosema.
Na kuhusu Biblia na Quran kuwa ni 100% chanya kwa binadamu sio kweli kwasababu vinasababisha sana migogoro na vurugu zisizo na msingi.
Indeed

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu jamaa kapuyanga sana .... yaani laiti kama angelijua kuwa dini za budha na hindu ni dini enyeji duniani basi nadhani angekubaliana. Nami bila shaka kuwa uislam.na ukristo ndio new Ages alizozisema ..dini hizo zinazaidi ya miaka 4000 wakati dini zake za uislam na ukiristo ni za juzi juzi tu kama ukiristo ni miaka 2000 uislam hata miaka 1800 hauna...ila kwakuwa haujui ngoja tumuache

Sent using Jamii Forums mobile app
Ha Ha Ha Ha Ha........

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya maneno yanaukweli maana kwenye vitabu vya Dini zote kubwa hakuna haya mambo sijui Astra projection, meditation wala hatukusikia mitume km walikua wanafanya mambo haya

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaweza niambia kitabu gani katika biblia ya vitabu 66, 73, 81 na 86 wameandika Mungu au Manabii au Mitume walianzisha dini au madhehebu?

Kwanini maisha ya manabii mfano Eliya, Elisha n.k walipendelea sana kukaa mbali na jamii zilizowazunguka especially Milimani?





Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom