New Age: Dini mpya ya ulimwengu

Kwa kifupi, New Age ni nini? Ni mkusanyiko wa dini zote; matendo mbalimbali ya kidini, ambayolengo lake ni kumfanya mwanadamu awe mungu. Ni mwavuli ambao chini yake dini zote zinaweza kujificha, ingawaje mafundisho yanaweza kuwa kinyume kabisa dini tulizozizoea kwa mana uislam& ukristo.


Yako mafundisho na dini ambazo asili yake ni ubudha, imani za siri za kishetani, na hata baadhi ya dini ambazo zina mafundisho ya msingi ya Kikristo, kwa mfano kanisa la Moon na Mashahidi wa Yehova hawa walipigwa marufuku Urusi, Wana wa Mungu au kile kinachoitwa ‘Sayansi ya Kikristo’ Church of Scientology pamoja na madhehebu ya kiislamu yanayoamini kwenye meditation.


Ziko falsafa: Ukonfyushasi wa Kichina (Chinese Confucianism), imani za siri (occult) na mafundisho ya unajimu, mashamani, ma-guru, Krishna, n.k. Makundi haya na mengineyo yanatengeneza namna ya kundi moja ambalo kiini chake hasa ni ushetani. Nguvu zingine zote za kichawi na imani za siri zinatokea hapa.

Pamoja na hayo, ni watu wachache sana waliomo ndani ya New Age wanaofahamu juu ya ukweli huu. Ndiyo sababu kuna Watu wengi walio kwenye kundi hili bila wao kujijua wanapotea.


Kwa kuwa, kwa nje kundi hili linaonekana ni la kiutu na ni chanya, hiki ni kishawishi kwa Watu na malengo yake yaliundwa kwa ajili hasa ya Watu wasio wanachama, ili kwamba wazimwe nguvu zao; na waweze kupelekwa mbali na Mungu . Baadhi ya mambo yanayofanyika ni yoga, kutoka katika mwili (astral projection), kuelea (levitating), namna zote za uchawi na upigani bao. Mambo haya ni vishawishi.
Mambo yote ya Meditation ni Ushetani wa kusalimu amri pamoja na akili ili kuruhusu kitu usicho kijua kichukue ufahamu wako.

Wanaanza kwa kufundisha kwamba Wakristo au waislamu wanatakiwa kuwa wavumilivu kwa makundi mengine, kwa mfano, kwa ajili ya maslahi ya wanadamu na amani ya dunia. Maneno yanayohusiana na upendo yanaweza kuwadanganya kirahisi Watu wengi.


Wako watu wengi wanaojifanya ni watumishi wa Mungu na wanaokuja kuhubiri na kutoa mawaiza kumbe ni wasanii tuu kajamaba8 washauza nafsi. Lakini pia wako watu kutoka kundi la New Age, wanaojiita guru, ambao nao wanakuja. Na kama mtasikiliza mafundisho yao na kutenda yale watakayowafundisha basi mungu atageuzia uso wake mbali na ww na jina lako litafutwa kwenye kitabu. .

Nisisitize tena kwamba, matendo na mafundisho haya ya kundi la New Age yanaweza kuharibu maisha yenu, lakini baya zaidi ni kuwa, yanaweza kuharibu roho yako pamoja na familia yako.

Binafsi nimeshashuhudia Wakristo na waislamu waliorudi nyuma na kumwacha Mungu aliye hai.kwa mfano wapo watu hapa jf wenye falsafa za ki new age ambao wana hadaa watu na meditation au astral prjection nakushauri usiingie humo madhara yake ni makubwa utaalika mapepo wachafu ndani ya nafsi yako au roho yako na kuharibu maisha yako kwa ujumla. Ndugu zangu msipende miujiza najua mnadanganywa kwenye meditation kuna miujiza hamna kitu ni majini tuu na mapepo yanachezea ufahamu wenu.

Ziko njia nyingi na matendo mengi ambayo Watu huingizwa humo. Kwa mfano, yoga, na hasa hatha-yoga, ambayo inajumuisha mazoezi ya viungo na kupumua. Wako binadamu wengi wa Marekani na nchi za magharibi ambao wanajihusisha na jambo hili.

Yoga ni nini? Ni mfumo wa vitendo vya kidini kwa ajili ya mtu kurudi tena baada ya kufa (reincarnation). Neno linasema kwamba Na kama vile watu walivyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu (Ebr. 9:27). Hakuna mtu anayeweza kurudi tena duniani kwa njia nyingine baada ya kufa hawezi kurudi kama mti au myama au mdudu. Yoga asili yake ni Uhindu, na ni mfumo wa vitendo vya dini nyingi. Vitendo hivi vinaaminika kuwa vinavunja nira kwenye maisha yako, ambazo, kwa imani zao, zitaanzisha mchakato wa “kuzaliwa tena baada ya kufa”. Kwa hiyo, kupitia yoga, tunafungulia mlango kwa mapepo ya Kihindu.

Wanaotetea falsafa ya Reicarnation ni wale wanaohusisha De Ja Vu na Maisha ya Zamani

Watu walegevu au wapuuzi wanasema kuwa hawaamini juu ya mambo haya bali kwamba hatha-yoga ni mazoezi tu mazuri kwa ajili ya mwili. Kwa kusema hivyo, tayari wameshaamini uongo wa ibilisi.

Iweje Shetani atakuruhusu ujenge mwili wako, na kujisikia vizuri? Inamana anakuoenda Sana? maana anajua kuwa Watu kama hao hawawezi kuona kilicho nyuma katika ulimwengu wa roho. Ni nini basi kitatokea? Matokeo yote ya kimwili na kiroho yanajengwa juu ya nguvu iitwayo Shiva. Hili ni pepo la Kihindu, ambalo wanalifungulia mlango.

Katika upande wa chini wa uti wa mgongo wetu, kuna nafasi wanayoiita “nguvu ya nyoka” au Kundalini kwa wanaofanya Mambo haya wanajua Unapofanya mazoezi ya yoga, unakuwa kimsingi unasujudu kwa huyu Shiva; ile nguvu ya nyoka inaamshwa kwenye mwili wako. Inapokuwa kubwa, watu wanapata na uwezo fulani usiokuwa wa kibinadamu.

Mambo haya hayatoki kwa Mungu aliye hai. Asili yake ni kwenye ulimwengu wa giza wa kipepo. Kwa hiyo, kumbuka kuwa mambo yote tunayofanya kimwili wakati wa yoga yana asili ya ulimwengu wa giza wa kipepo; haijalishi tunafikia ngazi gani. Hata hatua za kwanza kabisa zinakuwa zinaelekea kwenye vifungo hivyo – tuwe tunakubaliana au hatukubaliani.


Namna ya pili ambayo ni kishawishi kwa Watu, hata walio makanisani au Miskitini na imeenea sana nchi za magharibi pamoja na hapa jamii forum kuna mafundisho yake ni “kutoka nje ya mwili” (astral projection). Hii ni aina ya mazoezi ambayo yanaweze kufanya roho ya mtu ikatengana na mwili. Kwa uamuzi wako mwenyewe, unaweza kupeleka roho yako kwenye mahali au wakati wowote, kwa mfano ukarudi nyuma ya wakati kwenye maisha yaliyopita (time travel) ukaenda kwenye anga au kokote kwingineko.

Mara nyingi hili linawezekana, lakini ambacho watu wa namna hii hawatambui ni kuwa, roho zao zinakuwa haziingii kwenye ufalme wa Mungu bali wa mapepo.

Kwa njia hii, unafungulia mlango kwa viumbe wengine wa kiroho wasioonekana. Shetani ameweka tayari mtego wake kwa ajili yako pale. Watu wanapoanza kufanya mambo haya, kwa mara ya kwanza wanakuwa na hisia nzuri za kunyanyuliwa. Hisia hizi zinatoka kwenye asili ya dhambi.

Kuna hatari kubwa hapa. Kwa kitambo kidogo unakuwa unaweza kuitawala hali hiyo, lakini baada ya kufikia mahali fulani, unaanza kupoteza udhibiti wa mwili wako na unakuwa ni uwanja wa mapepo kufanya kila watakacho. Wengi walipoteza hata uwezo wao wa kurudi.


Res ipsa loquitur,
Badison.


View attachment 1015716

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha kutupotosha, ni heri dini ya New age kuliko ma Alshabab na Antibalaka wanaochinja watu kama kuku kwa kisingizio cha Mungu wa kweli. Ni upuuzi mtupu kujifanya mfia dini zilizoletwa kwenye majahazi na hao chinjachinja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nmepitia comment naona mtoa mada anashambuliwa Sana.Mtoa mada Ana hoja ajibiwe kwa hoja na sio kejeli na dhihaka.Leteni hoja kwa hoja tubaini ukweli wenu na wa mtoa mada.Other wise tutaamini mtoa mada ni mkweli kwa 100%.Mshana uje huku uthibitishe hizo meditation zenu mnatumika.
 
Nitajaribu Kufafanua Mkuu. Lakini ombi langu ni Moja. Kama utanipa elimu kuhusiana na Reptilians nami nitakufafanulia hilo fumbo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ishu ya reptilians naimani imezungumzwa sana humu JF na watu kama kina Eiyer na mkuu Juve2012 ni ishu pana zaidi kama unavyofahamu nashindwa nianze kuizungumzia wapi kwendana na mapana yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo mambo nizijaribu sana sijui kutoka kurudi, hizo mambo naona hazina tofauti na uteja yaani nilale ushirombo alafu nitoke niende Toronto usingizini kisha nikiamka niko hapo hapo, aisee bora Ndum kwa kweli kuliko hayo mambo yanavuruga akili
Umeona eeeh, ni sawa kabisa na mtu kukaa akiamini kwamba akifa kuna siku atafufuka...niuchizi uliopitiliza mammae!
 

Similar Discussions

18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom