field marshall1
JF-Expert Member
- Sep 17, 2017
- 1,171
- 2,730
Kuna taarifa leo kuwa Binyamin Netanyahu au Bibi ameshtakiwa na mwendesha mashtaka (DPP) pamoja na Mwanasheria Mkuu (Attorney General) wa serikali ya Israel kwa kosa la rushwa, ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.
Kwa vyovyote vile hataweza kushinda, kama ilivyotokea kwa Ehud Olmert aliyekuwa mtangulizi wake ambaye pia alishtakiwa kwa rushwa na kuripoti kuuza nyumba kwa bei ya chini jijini Jerusalem. Olmert alifungwa kifungo cha mwaka mmoja.
Marekani, Donald Trump naye amekalia kuti kavu huenda likakatika wakati wowote, kosa lake ni kutumia madaraka yake vibaya na kutumia mbinu ovu ili kushinda uchaguzi mkuu kwa kuwahusisha Russia (Bado ya Ukraine, Rushwa nk).
Akipatikana na kosa ataondolewa na huenda akafungwa kulingana na katiba ya Marekani.
Hiyo ni mifano miwili tu ya mambo yanayoendelea wiki hii, Katika dunia iliyostaarabika hayo mambo ni ya kawaida.
Ukiiba unafungwa, ukitumia vibaya rasilimali za nchi unafungwa au unatolewa na bunge/congress/senate etc. Mifano ni mingi mno.
Kwa wizi na matumizi mabovu anayojifanyia bila vibali vya bunge huyo Magufuli angekuwa indicted tayari kama ingekuwa nchi zilizostaarabika.
Tangu alivyouza nyumba za serikali na kuwagawia nduguze na rafiki zake hadi anavyojipendelea kujijengea kiwanja cha kimataifa cha ndege kijijini kwake, kuwaonea wanaompinga, kumpendelea Makonda asiye kuwa na vyeti na kugawagawa fedha ovyo.
Tungekuwa nchi ya demokrasia huyo Magufuli angeshakuwa nje ya taasisi ya uraisi pengine angekuwa anatumikia kifungo gerezani, lakini kwa kuwa nchi yetu ni hovyo hovyo(Kinachotufanya Africa tudharaulike).
Ameshakuwa kama Mungu kwa jinsi anavyosifiwa na kutukuzwa kiasi kwamba tunaambiwa na viongozi waliovimbiwa kuwa Mungu amshukuru Magufuli.
WHAT A SHAME?
Kwa vyovyote vile hataweza kushinda, kama ilivyotokea kwa Ehud Olmert aliyekuwa mtangulizi wake ambaye pia alishtakiwa kwa rushwa na kuripoti kuuza nyumba kwa bei ya chini jijini Jerusalem. Olmert alifungwa kifungo cha mwaka mmoja.
Marekani, Donald Trump naye amekalia kuti kavu huenda likakatika wakati wowote, kosa lake ni kutumia madaraka yake vibaya na kutumia mbinu ovu ili kushinda uchaguzi mkuu kwa kuwahusisha Russia (Bado ya Ukraine, Rushwa nk).
Akipatikana na kosa ataondolewa na huenda akafungwa kulingana na katiba ya Marekani.
Hiyo ni mifano miwili tu ya mambo yanayoendelea wiki hii, Katika dunia iliyostaarabika hayo mambo ni ya kawaida.
Ukiiba unafungwa, ukitumia vibaya rasilimali za nchi unafungwa au unatolewa na bunge/congress/senate etc. Mifano ni mingi mno.
Kwa wizi na matumizi mabovu anayojifanyia bila vibali vya bunge huyo Magufuli angekuwa indicted tayari kama ingekuwa nchi zilizostaarabika.
Tangu alivyouza nyumba za serikali na kuwagawia nduguze na rafiki zake hadi anavyojipendelea kujijengea kiwanja cha kimataifa cha ndege kijijini kwake, kuwaonea wanaompinga, kumpendelea Makonda asiye kuwa na vyeti na kugawagawa fedha ovyo.
Tungekuwa nchi ya demokrasia huyo Magufuli angeshakuwa nje ya taasisi ya uraisi pengine angekuwa anatumikia kifungo gerezani, lakini kwa kuwa nchi yetu ni hovyo hovyo(Kinachotufanya Africa tudharaulike).
Ameshakuwa kama Mungu kwa jinsi anavyosifiwa na kutukuzwa kiasi kwamba tunaambiwa na viongozi waliovimbiwa kuwa Mungu amshukuru Magufuli.
WHAT A SHAME?