nepotism, bureaucracy katika ajira na elimu

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
hii Tanzania ya Kikwete ndo nchi ya hovyo kabisa katika ukanda wa Afrika Mashariki, pengine Afrika kwa ujumla. tunapopoteza muda kujadili siasa za chadema na ccm, ni vema tukajikumbusha mambo muhimu ambayo yanasimamiwa katika mfumo wa business as usual. hivi inakuwaje, inakuwa vipi, katika muda ambao zimesalia wiki mbili tu kabla ya shule za sekondari kufunguliwa, hatima ya mwanao, aliyefaulu vema, bado hujajuwa amepangiwa shule gani ya sekondari atasoma?

hivi kweli waziri wa elimu na team yake wanatenda kazi sawasawa, au ni kitu gani hiki wanafanya? juzi tukaandikiwa kwenye magazeti idadi ya waliochaguliwa na waliokosa nafasi, lakini hadi leo hakuna majina yao. serikali inasubiri nini?

mbona watanzania tupo watu wa ajabu sana? au majina ya waliochaguliwa yanapatikana wapi, si watuambie twende huko tukapange foleni?!

aseee!
 
hii Tanzania ya Kikwete ndo nchi ya hovyo kabisa katika ukanda wa Afrika Mashariki, pengine Afrika kwa ujumla. tunapopoteza muda kujadili siasa za chadema na ccm, ni vema tukajikumbusha mambo muhimu ambayo yanasimamiwa katika mfumo wa business as usual. hivi inakuwaje, inakuwa vipi, katika muda ambao zimesalia wiki mbili tu kabla ya shule za sekondari kufunguliwa, hatima ya mwanao, aliyefaulu vema, bado hujajuwa amepangiwa shule gani ya sekondari atasoma?

hivi kweli waziri wa elimu na team yake wanatenda kazi sawasawa, au ni kitu gani hiki wanafanya? juzi tukaandikiwa kwenye magazeti idadi ya waliochaguliwa na waliokosa nafasi, lakini hadi leo hakuna majina yao. serikali inasubiri nini?

mbona watanzania tupo watu wa ajabu sana? au majina ya waliochaguliwa yanapatikana wapi, si watuambie twende huko tukapange foleni?!

aseee!

Nakubaliana na wewe mkuu, mambo mengi hovyohovyo mtu!
 
Back
Top Bottom