Neno shukrani linafariji na pia ni ishara ya uungwana kwa yule aliyekutendea mambo makubwa katika maisha yako

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,189
39,954
Sisi binadamu huwa tunajisahau kushukuru pale tunapotendewa mambo makubwa na watu fulani, tukiamini ilikuwa ni haki yako kutendewa vile. Wapo wanaojengewa nyumba au kupewa maisha mazuri na watu fulani, lakini badala ya wale wanufaika kushukuru, wao wanaona ilikuwa ni lazima au haki yao kuyapata.

Mfano mgonjwa aliyekata tamaa ya kuishi na baadaye kufanyiwa upasuaji wa viungo vyake iwe; miguu, mikono, moyo, uzazi, tumbo, macho, mapafu n.k na baada ya matibabu akapona kabisa; na baada ya kupona akashindwa kutoa neno la shukrani kwa wauguzi au madaktari waliompatia huduma mpaka kuishi, atakuwa hajafanya uungwana kwa waliompatia huduma.

Neno 'appreciation' ni muhimu sana kwa mtu aliyekufanyia makubwa, na pia ni uungwana.

Wengine watasema ilikuwa ni wajibu wake kupata hizo huduma; Swali, je wangezembea kidogo, ingekuwaje?
 
Sisi binadamu huwa tunajisahau kushukuru pale tunapotendewa mambo makubwa na watu fulani, tukiamini ilikuwa ni haki yako kutendewa vile. Wapo wanaojengewa nyumba au kupewa maisha mazuri na watu fulani, lakini badala ya wale wanufaika kushukuru, wao wanaona ilikuwa ni lazima au haki yao kuyapata.
Watakuja wanaojiita wasomi kukubeza kuwa haliwaongezei hata senti 5 ktk maisha na wako tayari lifutwe ktk lugha zote za ;

1. Kiswahili = Asante.

2. Malkia = Thanks

3. Kurya = Okorire buya

4. Sukuma = Wabeja sana.
 
Asieweza kumshukuru binaadamu mwenzake aliemsaidia, huyo hawezi kumshukuru hata Mola wake ambae hamuoni.
Asie shukuru kwa kidogo, hawezi shukuru hata akipewa kingi.
Asante na samahani ni maneno mafupi lakini thamani yake ni kubwa sana kwa yule alieyatamka kwa kumaanisha.
 
Back
Top Bottom