Thamani ya maneno POLE na SAMAHANI katika Mahusiano

Dr Lizzy

Platinum Member
May 25, 2009
30,778
59,133
images
images
images


Ladies, kwako mume/mpenzi wako anapokukosea una-prefer aombe samahani ya aina gani?

Ipi unadhani ni ya dhati?

Anyamaze kimya ila ajaribu kuku-WIN kwa kukununulia zawadi na kukufanyia vitu vizuri ambavyo alikuwa hafanyi mwanzo mf. Kukutoa out, kukusaidia vikazi vidogo vidogo nyumbani, kujali hisia zako na mahitaji yako binafsi, kuwahi kurudi nyumbani, kukushirikisha mambo yake n.k

Au kukuambia SAMAHANI, NILIKUKOSEA, HAITOTOKEA TENA halafu basi?

Wakaka/wababa huwa mnamaanisha nini pale mnapogoma kusema samahani na badala yake kuanza kumwaga mazawadi na pesa kwa wenzi wenu?
 
Habari wanaJf,
Hivi utafanyaje au utatumia njia gani ili kumuomba msamaha mwenza wako?:sorry:
Naomba mnisaidie.!
 
Habari wanaJf,
Hivi utafanyaje au utatumia njia gani ili kumuomba msamaha mwenza wako?
Naomba mnisaidie.!

Muombe katika hali ya utaratibu...mara nyingi kama yeye ana hasira we jishushe na uongee kwa ustaarabu!Muonyeshe kwamba unamaanisha unachokisema..yani kua sincere sio "We nisamehe bwana!"Kama inawezekana ahidi kutorudia tena kosa na ujitahidi kutorudia huko mbeleni!Na usisahau kuonyesha unajutia kosa lako!
 
Mtoe out luch or dinner hivi halafu mweleze kwa utaratibu usianze mambo kutafuta vijisababu sijui mungu kasema samehe saba mara sabini aaaahhhh wewe sema wewe kama wewe na uonyeshe nia ya kweli kabisa toka rohoni mwako usiongezee misitari yoyote zaidi ya ya kwako mwenyewe
 
Asante kwa ushauri lakini nimejaribu kumuomba msamaha lakini ananiambia kuwa nimemfanyia hilo kosa makusudi ili nimuombe msamaha coz najua tu kuwa atanisamehe.


Onyesha dhamira ya kweli kuwa unachosema kinatoka moyoni mfano unaweza shirikisha hata marafiki au ndugu zake kwa kutengeneza mazingira ya kukutanika pamoja halafu ukamwomba msamaha mbele ya wote (mashahidi) kwamba umedhamiria.

kama hutaki kujumuisha wengine (mf kama ni kosa la faragha) onyesha dhamira ya kweli kwa kuahidi kufanya kitu usichopenda (ambacho yeye pia anajua hupendi kufanya) kama dhamana endapo utarudia kosa ili hali kuonyesha umedhamiria kujirudi.
 
WanaJF,

Maneno pole na samahani yakitumika katika muda muafaka kwa wanandoa yanachangia kuongeza au kuleta upendo na heshima. Mathalani mume au mke anapofika nyumbani toka kazini au safari,akikaribishwa ndani na kupokewa mizigo kisha akaambiwa pole kwa kazi au safari hufarijika sana kwani huona mume au mke anampenda,anamheshimu na kumjali!

Ni aghalabu sana kwa mume au mke kumpa pole au samahani mwenzake kwa kutomfikisha kileleni au kwa kutowajibika vyema mara baada ya kufanya kile wanandoa wanaruhusiwa kukifanya na ambacho wapenzi hukifanya kwa kuiba pasipo kuwa na kibari maalumu! Mume au mke akimkosea mwenzake anapaswa kuomba msamaha,kwani kutokufanya hivyo kunaondoa upendo na heshima na kusababisha ndoa kuvunjika au wapenzi kuachana!
 
Yap! True but kuna watu ni wagumu kuomba msamaha hata wanapokosea even kumsamehe mwenzie utachuniwa wiki nzima had jasho likutoke ndo utasamehewa! Ila kuomba omba msamaha kila wakati napo ni udhaifu mwingine!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom