Neno 'mchakato' ni sera za ulaghai?

Kyachakiche

JF-Expert Member
Feb 16, 2009
983
207
Neno "Mchakato" limekuwa maarufu sana miongoni mwa wanasiasa hususani wa CCM na Serikali yake. Kila mara watu wanapotaka kujua ama kuelezwa juu ya ahadi ama utekelezwaji wa miradi mbalimbali, mara utasikia jitihada zinaendelea kufanyika, au mchakato unaendelea, upembufu yakinifu unaendelea... na mengine kama hayo. Je kwa wananchi wa kawaida wanaelewa haya au ni ulaghai tu wa viongozi katika kuomba kura? Na nini hasa maana ya mchakato na kwanini limeshika sana kasi kwenye awamu ya nne?
 
Hii ni sera mbadala ya maisha bora kwa kila mtanzania inawezekana. Tusubiri mchakato uishe mwakani.
 
Lakini neno lenyewe linamaanisha nini? Au ni kufunika kombe mwanaharamu apite!
 
Neno "Mchakato" limekuwa maarufu sana miongoni mwa wanasiasa hususani wa CCM na Serikali yake. Kila mara watu wanapotaka kujua ama kuelezwa juu ya ahadi ama utekelezwaji wa miradi mbalimbali, mara utasikia jitihada zinaendelea kufanyika, au mchakato unaendelea, upembufu yakinifu unaendelea... na mengine kama hayo. Je kwa wananchi wa kawaida wanaelewa haya au ni ulaghai tu wa viongozi katika kuomba kura? Na nini hasa maana ya mchakato na kwanini limeshika sana kasi kwenye awamu ya nne?

Mchakato ni neno la kiswahili na maana yake kwa lugha ya kiingereza ni 'process'
Maneno mengine na maana yake ni kama ifuatavyo:
Jitihada = Efforts
Upembuzi yakinifu = feasability Study
Sera = Policy
Mlishonyuma = Feedback

Kwa hiyo neno mchakato halina uhusiano wowote na neno 'ulaghai'
 
Neno "Mchakato" limekuwa maarufu sana miongoni mwa wanasiasa hususani wa CCM na Serikali yake. Kila mara watu wanapotaka kujua ama kuelezwa juu ya ahadi ama utekelezwaji wa miradi mbalimbali, mara utasikia jitihada zinaendelea kufanyika, au mchakato unaendelea, upembufu yakinifu unaendelea... na mengine kama hayo. Je kwa wananchi wa kawaida wanaelewa haya au ni ulaghai tu wa viongozi katika kuomba kura? Na nini hasa maana ya mchakato na kwanini limeshika sana kasi kwenye awamu ya nne?

Maneno haya 'mchakato' na 'tujipange upya' kwa kweli mimi yananiudhi sana maana ni maneno yanayopendwa sana kutumia na hawa viongozi uchwara hasa waliokuwemo katika awamu ya 3 na 4 kuonyesha kwamba they are doing something very important for the sake of our beloved country while in reality they are doing NOTHING AT ALL.

Tangu wameanza kufanya huo 'mchakato' na 'kujipanga upya' hatuoni lolote la maana zaidi ya ufisadi kushamiri. Ni maneno yanayotumiwa na hawa wanasiasa uchwara walioweka maslahi yao mbele badala ya nchi kama kutuzuga tu Watanzania lakini ukweli ni kwamba hakuna cha maana chochote wanachokifanya katika hiyo 'michakato' yao au 'kujipanga upya' .
 
Maneno haya 'mchakato' na 'tujipange upya' kwa kweli mimi yananiudhi sana maana ni maneno yanayopendwa sana kutumia na hawa viongozi uchwara hasa waliokuwemo katika awamu ya 3 na 4 kuonyesha kwamba they are doing something very important for the sake of our beloved country while in reality they are doing NOTHING AT ALL.

Tangu wameanza kufanya huo 'mchakato' na 'kujipanga upya' hatuoni lolote la maana zaidi ya ufisadi kushamiri. Ni maneno yanayotumiwa na hawa wanasiasa uchwara walioweka maslahi yao mbele badala ya nchi kama kutuzuga tu Watanzania lakini ukweli ni kwamba hakuna cha maana chochote wanachokifanya katika hiyo 'michakato' yao au 'kujipanga upya' .
Oyaaa! mchakato wa kuleta maisha bora kwa kila mtz unaendelea vema, aidha maadui wa CCM labda wajipange upya kama wanakusudia kuishinda CCM mwaka 2020
 
lakini hili neno sio linatumika na wana-ccm pekee hata vyama pinzani bungeni na uraiani wanatumia pia,ulaghai na ubabaishaji ni jadi yao hata kabla hawajabuni neno hili...ni mbinu mbadala tu
 
Mchakato ni neno la kiswahili na maana yake kwa lugha ya kiingereza ni 'process'
Maneno mengine na maana yake ni kama ifuatavyo:
Jitihada = Efforts
Upembuzi yakinifu = feasability Study
Sera = Policy
Mlishonyuma = Feedback

Kwa hiyo neno mchakato halina uhusiano wowote na neno 'ulaghai'

Nashukuru mkuu, ingawa hivyo, nafikiri hakuna 'process' isiyokuwa na takwimu(data) kwamba katika hili, limefanyika 1,2,3... na tunakusudia kufanya a, b,c..ili kumalizia. Lakini kutoa majibu ya ujumla kwamba mchakato unaendelea, kwanini tusiuite ulaghai?
 
[/I][/B]
Nashukuru mkuu, ingawa hivyo, nafikiri hakuna 'process' isiyokuwa na takwimu(data) kwamba katika hili, limefanyika 1,2,3... na tunakusudia kufanya a, b,c..ili kumalizia. Lakini kutoa majibu ya ujumla kwamba mchakato unaendelea, kwanini tusiuite ulaghai?

Matumizi ya neno 'mchakato' si lazima liambatane na takwimu kama unavyodai. Kwa mfano kama nipo katika mchakato wa kuoka keki, je nitatakiwa kutoa takwimu yeyote? Sidhani, kutoa takwimu katika jambo hakuna uhusiano wowote wa lazima na matumizi ya neno mchakato.
Kimsingi nadhani hili ni neno lisiloepukika hasa ikiwa ni lazima kufika ujumbe lengwa juu swala zima linaloongelewa. haijalishi unazungumzia wanasiasa au wanasayansi au wakulima nk
 
Maneno haya 'mchakato' na 'tujipange upya' kwa kweli mimi yananiudhi sana maana ni maneno yanayopendwa sana kutumia na hawa viongozi uchwara hasa waliokuwemo katika awamu ya 3 na 4 kuonyesha kwamba they are doing something very important for the sake of our beloved country while in reality they are doing NOTHING AT ALL.

Tangu wameanza kufanya huo 'mchakato' na 'kujipanga upya' hatuoni lolote la maana zaidi ya ufisadi kushamiri. Ni maneno yanayotumiwa na hawa wanasiasa uchwara walioweka maslahi yao mbele badala ya nchi kama kutuzuga tu Watanzania lakini ukweli ni kwamba hakuna cha maana chochote wanachokifanya katika hiyo 'michakato' yao au 'kujipanga upya' .
Mkuu tuko pamoja, na sasa wameingiza msemo 'mtikisiko wa uchumi duniani' wakati huko nyuma walishasema taifa letu halitakumbwa na hilo kana kwamba tulikuwa kwenye sayari nyingine. Hili nalo ni jiwe lingine la kukanyagia ili kuruka ahadi ya maisha bora kwa kila mtanzania mwakani kwenye uchaguzi.
 
Matumizi ya neno 'mchakato' si lazima liambatane na takwimu kama unavyodai. Kwa mfano kama nipo katika mchakato wa kuoka keki, je nitatakiwa kutoa takwimu yeyote? Sidhani, kutoa takwimu katika jambo hakuna uhusiano wowote wa lazima na matumizi ya neno mchakato.
Kimsingi nadhani hili ni neno lisiloepukika hasa ikiwa ni lazima kufika ujumbe lengwa juu swala zima linaloongelewa. haijalishi unazungumzia wanasiasa au wanasayansi au wakulima nk
Kwa mfano wako wa Kuoka keki, hata kwa kusema kuwa una mafuta au unga bado ni takwimu zinazoashiria umbali uliobaki ili keki iokwe.
 
Back
Top Bottom