tete'a'tete
JF-Expert Member
- Feb 10, 2010
- 472
- 62
Wakuu wote!
Natumai muu wazima na mungu aendelee kuwatangulia kwa kila mlifanyalo.
Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa woote mliojumuika nami tokea nimewapa taarifa ya msiba wa mama mkaungana nami kunifariji kuniombea mungu akaniwezesha nikatapa nguvu ya kuweza kumzika kwa heshima mama yangu mzazi huko Marangu Moshi tarehe 29/03/2010 kwa kweli si rahisi kwa binadamu yeyote kupata ujasiri lakini kwa sala zenu niliweza kupata ujasiri mkubwa kwani siku ya maziko niliweza kwenda KCMC kumvalisha mama na kumhudumia mpaka alipopumzishwa katika nyumba yake ya milele.
Wakuu nimerudi jumatano kwa bahati mbaya nilikuta forum yetu imesitishwa kwa muda kwa hivyo sikuweza kutoa shukrani zangu.
Nawashukuru woote mliowasiliana nami kwa njia simu muda wote kwa kunifariji na wale woote mlionitumia message kupitia jamii forum. Mungu azidi kuwabariki.
Napenda kuwajulisha kuwa baada ya kifo cha mama nimeamini kweli tumezaliwa na ipo siku tutakufa kwani sisi binadamu ni kama mshumaa ambao unawaka na kumulika sana na mwisho wake huzimika bila hata taarifa.
Nawaombeni wanajamii wote tuendelee na moyo huu mliuonyesha katika kipindi hiki kigumu na tuendelee kusaidiana si wakati wa furaha tuu bali hata kwenye matatizo katika maisha.
Asanteni! Asanteni! Asanteni! na Mungu awabariki katika maisha yenu.
Nawapenda woteee....
RIP my beloved Mother!
Tete'a'tete
Natumai muu wazima na mungu aendelee kuwatangulia kwa kila mlifanyalo.
Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa woote mliojumuika nami tokea nimewapa taarifa ya msiba wa mama mkaungana nami kunifariji kuniombea mungu akaniwezesha nikatapa nguvu ya kuweza kumzika kwa heshima mama yangu mzazi huko Marangu Moshi tarehe 29/03/2010 kwa kweli si rahisi kwa binadamu yeyote kupata ujasiri lakini kwa sala zenu niliweza kupata ujasiri mkubwa kwani siku ya maziko niliweza kwenda KCMC kumvalisha mama na kumhudumia mpaka alipopumzishwa katika nyumba yake ya milele.
Wakuu nimerudi jumatano kwa bahati mbaya nilikuta forum yetu imesitishwa kwa muda kwa hivyo sikuweza kutoa shukrani zangu.
Nawashukuru woote mliowasiliana nami kwa njia simu muda wote kwa kunifariji na wale woote mlionitumia message kupitia jamii forum. Mungu azidi kuwabariki.
Napenda kuwajulisha kuwa baada ya kifo cha mama nimeamini kweli tumezaliwa na ipo siku tutakufa kwani sisi binadamu ni kama mshumaa ambao unawaka na kumulika sana na mwisho wake huzimika bila hata taarifa.
Nawaombeni wanajamii wote tuendelee na moyo huu mliuonyesha katika kipindi hiki kigumu na tuendelee kusaidiana si wakati wa furaha tuu bali hata kwenye matatizo katika maisha.
Asanteni! Asanteni! Asanteni! na Mungu awabariki katika maisha yenu.
Nawapenda woteee....
RIP my beloved Mother!
Tete'a'tete