Neno La Leo: Yesu Akasema; Simon, Acha Kuvua Samaki, E Nenda Ukawe Mvuvi Wa Watu"

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu Zangu,


Bwana Yesu alipotembelea mto Galilaya, aliwakuta wavuvi wakivua samaki, Simoni alikuwa ni miongoni mwa wavuvi hao. Yesu akasema; " Simoni, acha kuvua samaki,nifuate ukawe mvuvi wa watu. Naam. Watu wengi wanaangamia kwa kukosa uelewa. Kwa kutojitambua. Wanahitaji ukombozi wa kifikra.

Na siku zote, haki uinua taifa, vivyo hivyo, dhulma huangamiza taifa. Na mahala pasipo na haki, basi, hapo hapatukuwa na amani.Oneni, maovu yametamalaki katika dunia tunaoishi. Siku zote, kujipendelea ndilo shina la maovu.

Si tuna mifano hai. Oneni, wale wenzetu waliokaa na wakaamua kuuza nyumba za Serikali. John Magufuli ni mmoja wa watu hao. John alisimamia utekelezaji wa dhulma ile kwa Watanzania. Lililopelekea uamuzi wa hila na ghilba wa kuuza nyumba za serikali ni ubinafsi na hulka ya baadhi ya viongozi kutaka kujipendelea.

Karibu wote waliouziwa au kujiuzia nyumba hizo za Serikali, nyumba za wananchi, tayari walikuwa na nyumba kabla. Siku zoe, hamu inakuwa ni jambo jema, endapo binadamu ataweza kuitawala hamu/tamaa yake.

Wanadamu tusipoitawala hamu yetu, tukaanza kujipendelea, kuwasahau wengine, basi, hilo huwa ndio chimbuko la maovu. Hupelekea kutoelewana baina ya wanandugu, na hata kwa marafiki walioshibana.

Hupelekea vurugu na machafuko katika jamii. Tunazungumzia uwepo wa upendo, haki na usawa. Dini nyingi zinazungumzia umuhimu wa upendo, haki na usawa katika jamii. Iwe ni Uislamu na Ukristo vivyo hivyo. ”

Naapa kwa zama . Hakika binadamu wote wamo katika hasara isipokuwa wale walioamini na wakafanya matendo mema. Wakahusiana na haki na wakahusiana na subira” (Koran tukufu, Surat ASWR)

Biblia nayo inasema; kuwa Kaini alikuwa mtu wa kujipendelea mno, akamwua nduguye. Mfalme Saulo alijipendelea mno, akamdhulumu Daudi. Yuda alijipendelea mno, akalikubali kumsaliti Yesu kwa Vipande thelathini vya fedha. Hatimaye, akamsaliti Yesu.

Na ufufuko wa Bwana Yesu utukumbushe jukumu letu la kupambana na maovu katika jamii. Utukumbushe jukumu la kusaidia kazi ya kuwakomboa kifikra wanadamu wenzetu. Kama Bwana Yesu alivyomkumbusha Simoni kwa kumwambia; ” Simoni, acha kuvua samaki. E nenda ukawe mvuvi wa watu. Na hilo ndilo Neno la Leo. Pasaka Njema.


Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam
0788 111 765
http.//mjengwablog.com
 
Majjid siamini kama ni mgeni wakushindwa kujua jukwaa gani la kupost japokuwa nimeona kipande kimoja tu kinachoweza kukaa hapa cha Magufuli na uuzaji nyumba.

Ok, mimi nimependa sana ile aya ya Qurani iliyonakiri kusema kweli ni aya nzito kwa watu wenye kumjua Mungu. Nashukuru kwa message yako ya Easther.
 
Ndugu Zangu,


Bwana Yesu alipotembelea mto Galilaya, aliwakuta wavuvi wakivua samaki, Simoni alikuwa ni miongoni mwa wavuvi hao. Yesu akasema; " Simoni, acha kuvua samaki,nifuate ukawe mvuvi wa watu. Naam. Watu wengi wanaangamia kwa kukosa uelewa. Kwa kutojitambua. Wanahitaji ukombozi wa kifikra.

Na siku zote, haki uinua taifa, vivyo hivyo, dhulma huangamiza taifa. Na mahala pasipo na haki, basi, hapo hapatukuwa na amani.Oneni, maovu yametamalaki katika dunia tunaoishi. Siku zote, kujipendelea ndilo shina la maovu.

Si tuna mifano hai. Oneni, wale wenzetu waliokaa na wakaamua kuuza nyumba za Serikali. John Magufuli ni mmoja wa watu hao. John alisimamia utekelezaji wa dhulma ile kwa Watanzania. Lililopelekea uamuzi wa hila na ghilba wa kuuza nyumba za serikali ni ubinafsi na hulka ya baadhi ya viongozi kutaka kujipendelea.

Karibu wote waliouziwa au kujiuzia nyumba hizo za Serikali, nyumba za wananchi, tayari walikuwa na nyumba kabla. Siku zoe, hamu inakuwa ni jambo jema, endapo binadamu ataweza kuitawala hamu/tamaa yake.

Wanadamu tusipoitawala hamu yetu, tukaanza kujipendelea, kuwasahau wengine, basi, hilo huwa ndio chimbuko la maovu. Hupelekea kutoelewana baina ya wanandugu, na hata kwa marafiki walioshibana.

Hupelekea vurugu na machafuko katika jamii. Tunazungumzia uwepo wa upendo, haki na usawa. Dini nyingi zinazungumzia umuhimu wa upendo, haki na usawa katika jamii. Iwe ni Uislamu na Ukristo vivyo hivyo. ”

Naapa kwa zama . Hakika binadamu wote wamo katika hasara isipokuwa wale walioamini na wakafanya matendo mema. Wakahusiana na haki na wakahusiana na subira” (Koran tukufu, Surat ASWR)

Biblia nayo inasema; kuwa Kaini alikuwa mtu wa kujipendelea mno, akamwua nduguye. Mfalme Saulo alijipendelea mno, akamdhulumu Daudi. Yuda alijipendelea mno, akalikubali kumsaliti Yesu kwa Vipande thelathini vya fedha. Hatimaye, akamsaliti Yesu.

Na ufufuko wa Bwana Yesu utukumbushe jukumu letu la kupambana na maovu katika jamii. Utukumbushe jukumu la kusaidia kazi ya kuwakomboa kifikra wanadamu wenzetu. Kama Bwana Yesu alivyomkumbusha Simoni kwa kumwambia; ” Simoni, acha kuvua samaki. E nenda ukawe mvuvi wa watu. Na hilo ndilo Neno la Leo. Pasaka Njema.


Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam
0788 111 765
http.//mjengwablog.com

1.Kwa sababu wewe ni MWANDISHI wa HABARI tena ALIYEBOBEA umeandika ARTICLE ya KIDINI kwenye JUKWAA LA KISIASA na IKIWA HAINA MAUDHUI YOYOTE KISIASA!!
-My TAKE:
1:Wewe ni miongoni mwa BINADAMU wanao semekana na SEHEMU KUBWA YA DUNIA kuwa na AKILI SANA!

2-Kwa kuwa leo ni Pasaka nakusamehe na sikutuhumu tuhuma ya UKILAZA kwa ku POST KWENYE JUKWAA WRONG kwani kuna uwezekano uligonga kilaji!
 
Majjid siamini kama ni mgeni wakushindwa kujua jukwaa gani la kupost japokuwa nimeona kipande kimoja tu kinachoweza kukaa hapa cha Magufuli na uuzaji nyumba.

Ok, mimi nimependa sana ile aya ya Qurani iliyonakiri kusema kweli ni aya nzito kwa watu wenye kumjua Mungu. Nashukuru kwa message yako ya Easther.

Haya mambo ya biblia /quran yana ukweli si unaona Lema magamba wamemwambia Arusha inatosha sasa njoo uwakomboe watanzania wote
 
Majjid siamini kama ni mgeni wakushindwa kujua jukwaa gani la kupost japokuwa nimeona kipande kimoja tu kinachoweza kukaa hapa cha Magufuli na uuzaji nyumba.

Ok, mimi nimependa sana ile aya ya Qurani iliyonakiri kusema kweli ni aya nzito kwa watu wenye kumjua Mungu. Nashukuru kwa message yako ya Easther.

Mkuu usijali baada ya muda utaona Moved!
Kazi ya Mods kumuvuzisha
 
Ndugu Zangu,


Bwana Yesu alipotembelea mto Galilaya, aliwakuta wavuvi wakivua samaki, Simoni alikuwa ni miongoni mwa wavuvi hao. Yesu akasema; " Simoni, acha kuvua samaki,nifuate ukawe mvuvi wa watu. Naam. Watu wengi wanaangamia kwa kukosa uelewa. Kwa kutojitambua. Wanahitaji ukombozi wa kifikra.

Na siku zote, haki uinua taifa, vivyo hivyo, dhulma huangamiza taifa. Na mahala pasipo na haki, basi, hapo hapatukuwa na amani.Oneni, maovu yametamalaki katika dunia tunaoishi. Siku zote, kujipendelea ndilo shina la maovu.

Si tuna mifano hai. Oneni, wale wenzetu waliokaa na wakaamua kuuza nyumba za Serikali. John Magufuli ni mmoja wa watu hao. John alisimamia utekelezaji wa dhulma ile kwa Watanzania. Lililopelekea uamuzi wa hila na ghilba wa kuuza nyumba za serikali ni ubinafsi na hulka ya baadhi ya viongozi kutaka kujipendelea.

Karibu wote waliouziwa au kujiuzia nyumba hizo za Serikali, nyumba za wananchi, tayari walikuwa na nyumba kabla. Siku zoe, hamu inakuwa ni jambo jema, endapo binadamu ataweza kuitawala hamu/tamaa yake.

Wanadamu tusipoitawala hamu yetu, tukaanza kujipendelea, kuwasahau wengine, basi, hilo huwa ndio chimbuko la maovu. Hupelekea kutoelewana baina ya wanandugu, na hata kwa marafiki walioshibana.

Hupelekea vurugu na machafuko katika jamii. Tunazungumzia uwepo wa upendo, haki na usawa. Dini nyingi zinazungumzia umuhimu wa upendo, haki na usawa katika jamii. Iwe ni Uislamu na Ukristo vivyo hivyo. "

Naapa kwa zama . Hakika binadamu wote wamo katika hasara isipokuwa wale walioamini na wakafanya matendo mema. Wakahusiana na haki na wakahusiana na subira" (Koran tukufu, Surat ASWR)

Biblia nayo inasema; kuwa Kaini alikuwa mtu wa kujipendelea mno, akamwua nduguye. Mfalme Saulo alijipendelea mno, akamdhulumu Daudi. Yuda alijipendelea mno, akalikubali kumsaliti Yesu kwa Vipande thelathini vya fedha. Hatimaye, akamsaliti Yesu.

Na ufufuko wa Bwana Yesu utukumbushe jukumu letu la kupambana na maovu katika jamii. Utukumbushe jukumu la kusaidia kazi ya kuwakomboa kifikra wanadamu wenzetu. Kama Bwana Yesu alivyomkumbusha Simoni kwa kumwambia; " Simoni, acha kuvua samaki. E nenda ukawe mvuvi wa watu. Na hilo ndilo Neno la Leo. Pasaka Njema.


Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam
0788 111 765
http.//mjengwablog.com

Majjid,
Mbona unataka kumzibia mwenzio riziki? hujui Pombe anavyojikakamua kutaka kuomba ridhaa ya magamba kugombea urais?
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom