Neno La Leo: Mwadhama Kardinali Pengo, Nina Nyongeza Ya Neno

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Na Maggid Mjengwa,

" SIO kila mmoja ataridhishwa na matokeo, isipokuwa, jambo la msingi ni kulinda lengo kuu ambalo ni amani ya taifa". Hiyo ni kauli ya Askofu Mkuu Jimbo Kuu la Dar es Slaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo alipozungumza kwenye kipindi cha ujumbe wa Askofu Pengo kilichorushwa na Redio Tumaini na kuripotiwa na gazeti la Mwananchi, Ijumaa, Novemba 5, 2010.

Kwa ye yote mwenye kuitakia mema nchi yetu, basi, atakubali, kuwa, kauli ya Mwadhama Kardinali Pengo ni kauli iliyojaa busara na hekima nyingi. Ni ya kuungwa mkono. Na hapa nina nyongeza ya neno, maana, Kardinali Pengo amenukuliwa pia akitamka; kuwa mataifa mengi ulimwenguni yamejikuta yakitumbukia katika maafa kutokana na kutoridhishwa na matokeo ya uchaguzi. Askofu Pengo akawataka viongozi wa vyama na jamii wasichukue hatua zinazoweza kuliangamiza taifa. Akatamka;

"Mungu atujalie moyo wa kupokea matokeo yalivyo na hata tusiporidhika tujipe moyo ili tusije tumbukia katika maafa ambayo yatachukua muda mrefu kuondoka". ( Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo, Mwananchi, Novemba 5, 2010)

Na hapa tena nina nyongeza nyingine ya neno. Hakika, ni busara na hekima, kwa mwanadamu kutambua na kuheshimu mamlaka iliyopo na zaidi, inayotokana na watu. Kutambua na kuheshimu mamlaka inayotokana na sheria, kanuni na taratibu za mahali husika, hivyo basi, mamlaka inayotokana na Katiba ya wakati huo. Na mwanadamu huyo, midhari amefanya mawili hayo, hana lazima ya kufanya jambo la tatu; kuyaenzi mamlaka hayo.


Yawezekana kabisa, kuwa katika kuyapata mamlaka hayo kukawa na mapungufu ya sheria, kanuni na taratibu. Lakini, hayo yasipewe nafasi ya kufanya mchakato wa kisiasa katika jamii ukakwama. Maana, siasa ina maana ya majadiliano endelevu. Ni majadiliano yasiyo koma. Muhimu katika siasa ni kubaki katika meza ya majadiliano.


Na hilo ni Neno La Leo.

Maggid
Iringa, Novemba 9


( Ni Sehemu ya makala yangu ya Raia Mwema ikichapwa kesho Jumatano)
 
Sasa hili ndo neno la leo? Huna style nyingine ya kuwakilisha ujumbe wako?

Mbona unachafua gazeti la Rai Mwema? Nakushauri upeleke hii kitu RAI
 
Haki ni muhimu zaidi kuliko hayo manene unayoyaita ni ya busara, JK na CCM yake wameichafua nchi hii kwa kupandikiza hisia za kidini na kikabila Pengo kakaa kimya tu, Juzi baada ya kuapishwa JK anaviomba vyombo vya habari virekebishe madonda waliyoyatengeneza kwa kupitia JK na CCM yake lakini pengo kaona hilo ni sawa tu, JK, CCM na NEC wamearibu uchaguzi waziwazi na kilio cha watanzania kinasikika kwamba hujuma imefanyika Pengo kakaa kimya tu.

Hii kauli unayoita ni ya busara haina maana yoyote ikiwa haki ya raia inaporwa na yeye anaona ni sawa tu
 
[FONT="]Na hapa tena nina nyongeza nyingine ya neno. Hakika, ni busara na hekima, kwa mwanadamu kutambua na kuheshimu mamlaka iliyopo na zaidi, inayotokana na watu. Kutambua na kuheshimu mamlaka inayotokana na sheria, kanuni na taratibu za mahali husika, hivyo basi, mamlaka inayotokana na Katiba ya wakati huo. Na mwanadamu huyo, midhari amefanya mawili hayo, hana lazima ya kufanya jambo la tatu; kuyaenzi mamlaka hayo. [/FONT]
Tukikwepa kuzungumzia dhuluma kwa kutumia neno amani kama kichaka cha kuhalalisha uonevu basi kamwe hiyo amani mnayotudoboshia nayo hatutaipata.............lakini penye dhuluma usifikiri Mwenyezi Mungu kwa kukaa kimya ameafiki kama Kardinali Pengo anavyojipotosha..........................

Soma PSALMS 50:21"These things you have done I kept silent, and you thought I was altogether like you, but I will rebuke you and set them in order before your eyes."


Viongozi wengi wa dini hivi sasa ni wabinafsi na wanatanguliza masilahi yao.........hivi Askofu Mkuu Kilaini aliongea lini na Mwenyezi Mungu akamwambia JK ni chaguo la Mungu kama siyo utapeli kwa kumdhihaki Mwenyezi Mungu.................Hivi chaguo la Mungu litajihusisha na ufisadi kweli na kuchakachua matokeo ya kura?

Na ndiyo maana Yesu Kristu kwenye utukufu wake alijua hata makanisa yataingiliwa na matapeli na alionya yafuatayo:-

Mathew 7: 21 "Not everyone who says to Me, "LORD, LORD.." shall enter the kingdom of heaven, but he who does the word of My Father in heaven."


Hakuna kwenye maandiko matakatifu ambapo Mwenyezi Mungu amehalalisha dhuluma kama Kardinali Pengo anavyojaribu kufanya........................mtoa haki ni Mwenyezi Mungu na kwenye hili atatenda haki na sote tutabaki vinywa wazi.................
 
Kings Of Kings,
Ahsante,
Hilo ndilo neno la leo. Na hiyo ndio style yangu ya kuwasilisha ujumbe. Hayo mengine ni mawazo yako. Ni haki yako kuyatoa.
 
vipi kuhusu wizi wa kura na uchaguzi unaoitwa huru lakini usio wa haki?
hakuzungumza lolote?
 
Tukikwepa kuzungumzia dhuluma kwa kutumia neno amani kama kichaka cha kuhalalisha uonevu basi kamwe hiyo amani mnayotudoboshia nayo hatutaipata.............lakini penye dhuluma usifikiri Mwenyezi Mungu kwa kukaa kimya ameafiki kama Kardinali Pengo anavyojipotosha..........................

Soma PSALMS 50:21"These things you have done I kept silent, and you thought I was altogether like you, but I will rebuke you and set them in order before your eyes."


Viongozi wengi wa dini hivi sasa ni wabinafsi na wanatanguliza masilahi yao.........hivi Askofu Mkuu Kilaini aliongea lini na Mwenyezi Mungu akamwambia JK ni chaguo la Mungu kama siyo utapeli kwa kumdhihaki Mwenyezi Mungu.................Hivi chaguo la Mungu litajihusisha na ufisadi kweli na kuchakachua matokeo ya kura?

Na ndiyo maana Yesu Kristu kwenye utukufu wake alijua hata makanisa yataingiliwa na matapeli na alionya yafuatayo:-

Mathew 7: 21 "Not everyone who says to Me, "LORD, LORD.." shall enter the kingdom of heaven, but he who does the word of My Father in heaven."


Hakuna kwenye maandiko matakatifu ambapo Mwenyezi Mungu amehalalisha dhuluma kama Kardinali Pengo anavyojaribu kufanya........................mtoa haki ni Mwenyezi Mungu na kwenye hili atatenda haki na sote tutabaki vinywa wazi.................


"mtoa haki ni Mwenyezi Mungu na kwenye hili atatenda haki na sote tutabaki vinywa wazi" ni kweli kabisa maana mpaka sasa umebaki kinywa wazi hujielewi! sifa zimuendee mwenyezi mungu kwa kutoa haki!
 
Bado watu wanajibu hoja za Maggid. Haya endeleeni.
 
1SAMWELI 15:23 - 'Kwa maana kuasi ni kama dhambi ya uchawi, na chukizo nikama uovu wa kuabudu sanamu. Kwasababu umelikataa neno la Bwana, yeye amekukataa kama mfalme'
 
Tukikwepa kuzungumzia dhuluma kwa kutumia neno amani kama kichaka cha kuhalalisha uonevu basi kamwe hiyo amani mnayotudoboshia nayo hatutaipata.............lakini penye dhuluma usifikiri Mwenyezi Mungu kwa kukaa kimya ameafiki kama Kardinali Pengo anavyojipotosha..........................

Soma PSALMS 50:21"These things you have done I kept silent, and you thought I was altogether like you, but I will rebuke you and set them in order before your eyes."


Viongozi wengi wa dini hivi sasa ni wabinafsi na wanatanguliza masilahi yao.........hivi Askofu Mkuu Kilaini aliongea lini na Mwenyezi Mungu akamwambia JK ni chaguo la Mungu kama siyo utapeli kwa kumdhihaki Mwenyezi Mungu.................Hivi chaguo la Mungu litajihusisha na ufisadi kweli na kuchakachua matokeo ya kura?

Na ndiyo maana Yesu Kristu kwenye utukufu wake alijua hata makanisa yataingiliwa na matapeli na alionya yafuatayo:-

Mathew 7: 21 "Not everyone who says to Me, "LORD, LORD.." shall enter the kingdom of heaven, but he who does the word of My Father in heaven."


Hakuna kwenye maandiko matakatifu ambapo Mwenyezi Mungu amehalalisha dhuluma kama Kardinali Pengo anavyojaribu kufanya........................mtoa haki ni Mwenyezi Mungu na kwenye hili atatenda haki na sote tutabaki vinywa wazi.................

ama kweli mtoa haki ni mwenyezi mungu na ametenda haki yake tayari na ndio maana umebaki kinywa wazi!
 
hivi kumbe kila kiumbe anaweza andikia raia mwema akijitahidi eeh! I am stunned.
maggid analinajisi gazeti la raia mwema si apelekwe rai mi makala zake huwa sizielewielewi kama za johnkibaso hawa watu wanataka kujichanganya na wenye uchungu na nchi kumbe ni vibaraka wa ccm
 
Na hapa tena nina nyongeza nyingine ya neno. Hakika, ni busara na hekima, kwa mwanadamu kutambua na kuheshimu mamlaka iliyopo na zaidi, inayotokana na watu. Kutambua na kuheshimu mamlaka inayotokana na sheria, kanuni na taratibu za mahali husika, hivyo basi, mamlaka inayotokana na Katiba ya wakati huo. Na mwanadamu huyo, midhari amefanya mawili hayo, hana lazima ya kufanya jambo la tatu; kuyaenzi mamlaka hayo.


Maggid,

Kwa mara ya kwanza nimekubalina na neno lako hasa hapo nilipoonyesha kwa herufi kubwa. Kwa hiyo mamlaka iliyopatika kinyume cha sheria ifanyweje. Sasa hivi tuna mamlaka iliyopatikana kwa kutofuata sheria ya uchaguzi, kwa hiyo ipo pale kinyume cha sheria. Je tufanyeje?

................Fafanua......
 
Mi naona sasa tunakuwa na jazba zisizo na mpangilio. What is wrong with the article? Katoa tu mawazo yake na sisi tumwage ya kwetu.

Back to the topic, Mimi nafikiri hawa viongozi wa dini siamini kama wanaitendea haki Tanzania na watanzania wake. Kama waliamu kuwa hawatojihusisha na siasa za nchi na kuamua kukaa kimya basi ni vema wakaendelea kukaa kimya hivyo hivyo. Kwani kwa mtazamo wangu hakuna mantiki ya kukaa kimya wakati wa zoezi zima la uchaguzi halafu uje ujitokeze leo baaday ya uchaguzi kuja kuhubiri so called 'amani'.

Kama waliona kuwa yaliyokuwa yanatokea wakati wa kampeni na kipindi cha uchaguzi chenyewe havikuwa uvunjifu wa amanina hivyo wao kuwa mabubu basi wameshindwa kuwasemea waumini wao na ni bora wakaendelea kuwa mabubu kwani kwa watu kama wao hatukuwategemea kukaa kimya pale amani na haki zilivyokuwa zinapotezwa na kundi dogo la watu wenye uroho wa madaraka na wasiojali kundi kubwa la wananchi na kuwatumia wanavyotaka kisa tu kwa wananchi wa Tanzania na umaskini wao wakawa vulnerable na hongo na rushwa za vitu vidogo na kupoteza utu na haki zao za kuchagua viongozi walio bora na wenye uchungu na nchi hii.

Ni nini kuhubiri kudumisha amani wakati sote tunajua kuwa amani is not merely absence of political conflicts lakini katika jamii kuna social conflicts na nyingi ni kutokana na umaskini ambao tumeletewa leo hii na hawa viongozi wetu.

Wamekaa kimya pale ambapo CCM walikuwa wakipiga kampeni za udini ili wapinzani waonekane wabaya na kuwaogopesha wananchi kwa mbegu hiyo mbaya, je unafikiri ni nani aliyepandikiza mbegu ya udini kama siyo JK na CCM yake? Leo hii anakuja kutuambia kwa kejeli kuwa tukatibu majeraha waliyoyasababisha ya udini na ukabila. Viongozi wa dini walikuwa wapi hapa? Kama wao ni wa dini wanatakiwa waseme kweli tupu na si kuufinyanga uongo kwa mafuta ya ukweli na hija za kimungu ili usionakane mbaya, HUU NI USALITI.

Kama huamini CCM imepandikiza chuki ya udini na ukabila, hebu jaribu kufanya analysis ya ushindi wa CCM kwa majimbo, utagundua kuwa CCM imepata ushabiki mkumbwa sehemu za mamwinyi na hii ni matokeo ya strategy za Kikwete na CCM kwa kutumia neno udini.

NENO LA LEO

Mjengwa kama muumini wa Nyerere, mimi ningekuwa nina nafasi ya kumuuliza Kikwete, swali langu lingekuwa, je anafikiri Tanzania ina amani ya kweli? Na je yeye kama mwanafunzi wa JK Nyerere (kama aliyokuwa akitamba kampeni za 2005) anafikiri ni Nyerere angependezwa na uongozi wake wa kukumbatia mafisadi? Je anafikiri angesalimika kutoka katika mdomo wa yule mzee? Angesalimika na siasa zake za kupandikiza udini na chuki za kikabila?

Nawasilisha
 
Mimi sikubali kuwa mtu ukinyimwa haki yako basi ukae kimya..

Pengo huyo naye ni mmoja ya watu wanaoheshimika sana katika kanisa, yeye anakubalije matokeo huku akijua kuwa CCM wamechakachua???

Mimi sikubaliani na msimamo wake.. kama anataka kutubali bali ukweli ujulikane na haki itendeke....

Asitulazimishe kukubali wizi kwa kisingizio cha Amani ya nchi.. Amani ipi wakati watu ni maskini hivi????

HIvi kweli inaingia akilini mtu kuwa na amani wakati huna hata kumi mfukoni na familia inataabika nyumbani.. elimu mbovu namna hii.??

Mimi sikubali hadi kieleweke...
 
Na Maggid Mjengwa,

" SIO kila mmoja ataridhishwa na matokeo, isipokuwa, jambo la msingi ni kulinda lengo kuu ambalo ni amani ya taifa". Hiyo ni kauli ya Askofu Mkuu Jimbo Kuu la Dar es Slaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo alipozungumza kwenye kipindi cha ujumbe wa Askofu Pengo kilichorushwa na Redio Tumaini na kuripotiwa na gazeti la Mwananchi, Ijumaa, Novemba 5, 2010.


Kwa ye yote mwenye kuitakia mema nchi yetu, basi, atakubali, kuwa, kauli ya Mwadhama Kardinali Pengo ni kauli iliyojaa busara na hekima nyingi. Ni ya kuungwa mkono. Na hapa nina nyongeza ya neno, maana, Kardinali Pengo amenukuliwa pia akitamka; kuwa mataifa mengi ulimwenguni yamejikuta yakitumbukia katika maafa kutokana na kutoridhishwa na matokeo ya uchaguzi. Askofu Pengo akawataka viongozi wa vyama na jamii wasichukue hatua zinazoweza kuliangamiza taifa. Akatamka;


" Mungu atujalie moyo wa kupokea matokeo yalivyo na hata tusiporidhika tujipe moyo ili tusije tumbukia katika maafa ambayo yatachukua muda mrefu kuondoka". ( Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo, Mwananchi, Novemba 5, 2010)

Na hapa tena nina nyongeza nyingine ya neno. Hakika, ni busara na hekima, kwa mwanadamu kutambua na kuheshimu mamlaka iliyopo na zaidi, inayotokana na watu. Kutambua na kuheshimu mamlaka inayotokana na sheria, kanuni na taratibu za mahali husika, hivyo basi, mamlaka inayotokana na Katiba ya wakati huo. Na mwanadamu huyo, midhari amefanya mawili hayo, hana lazima ya kufanya jambo la tatu; kuyaenzi mamlaka hayo.


[FONT=&quot[COLOR=red]]Yawezekana kabisa, kuwa katika kuyapata mamlaka hayo kukawa na mapungufu ya sheria, kanuni na taratibu[/COLOR]. Lakini, hayo yasipewe nafasi ya kufanya mchakato wa kisiasa katika jamii ukakwama. Maana, siasa ina maana ya majadiliano endelevu. Ni majadiliano yasiyo koma. Muhimu katika siasa ni kubaki katika meza ya majadiliano.
[/FONT]


Na hilo ni Neno La Leo.

Maggid
Iringa, Novemba 9



mjengwa


( Ni Sehemu ya makala yangu ya Raia Mwema ikichapwa kesho Jumatano)






Matokea yalitona na mizengwe, mabomu ya machozi na uchakachuaji mwingine hayawezi kuwa na idhini ya mungu, labda kama Mungu wa hapo Mwembe Tongwa anyebariki dhuruma. Majina ya watu kibao yameondolewa kwenye daftari ili wasipige kura, Matokeo yamechukuwa muda mrefu kutangazwa, kisingizio computer. Mwogopeni Mungu, Msimhusishe na uchafu wa kifisadi.
 
Kings Of Kings,
Ahsante,
Hilo ndilo neno la leo. Na hiyo ndio style yangu ya kuwasilisha ujumbe. Hayo mengine ni mawazo yako. Ni haki yako kuyatoa.

USA kuna NGO inaitwa Rasmussen Poll ilitabiri kishabiki kuwa Democrats itapoteza hata nguvu ya Seneta ktk uchaguzi wa juzi na hata ikataja wazi wazi kuwa kiongozi Harry Reid atapigwa vibaya kule Nevada;Mama Pat Muray atashindwa kule Washington-Seattle na Bennet atapoteza Colorado;lkn kinyume chake haikuwa hivyo na hivi sasa Rasmusen anavurumishiwa kila aina ya masimango kwa upotoshaji na hata heshima yake imepungua sana machoni mwa watu na wengine wamefikia mbali kusema"Rasmussen poll is not legitimate any more"!

Maggid maana wewe ulisema Dr Slaa atakuwa wa 3 lkn haijawa hivyo,ukasema CUF kitakuwa chama kikuu cha upinzani Bungeni lkn haitakuwa hivyo na ukafikia hata kusema kuwa "sasa mama Mbega ukikutana nae Iringa anacheka tu"lkn haikuwa hivyo maana badala yake sasa analia tu!!

Maggid angalia sana na wewe usije ukawa Rasmussen wetu na hata wa TZ wengi wakafikia hatua kukuambia kuwa"Maggid posts are not legitimate any more"!


 
Inasikitisha sana kwa viongozi wa dini kusisitiza aliyeibiwa anyamaze na anaonekana mwovu anayetaka kusababisha kuvunjika kwa amani na wakati huo huo wanamwombea na kumbariki asiyetenda haki (mwizi, mbadhirifu, jangili, fisadi).

Siku hizi hasa inapokuja suala na kudai haki na maslahi ya wanyonge hapa nchini viongozi wa dini wamekuwa Mafarisayo kwa 100%.

Enzi za Mwinyi, pengo alikuwa machachari sana, sijui nini kimetokea ilhali ukilinganisha ufisadi ule na wa leo, wa leo ni hatari sana.
- Ni kama mwinyi alitunyoa nywele akaziuza nje (Pengo na wenzake wakamlaani)
-Mkapa, JK na wenzake wamegeuka mumiani wanauza damu zetu nje (Pengo na wenzake wanawabariki)

Eee Mungu Utulipie kisasi sisi wanao wanyonge, huyu kibaraka wao waliyemweka ikulu atoke huko akiwa katika coffin, na wizi wote alioufanya asiufaidi.
 
Ndugu Maggid,

Amani na utulivu ni kitu chema na yeyote anayeipenda inchi yake ataiombea hicho siku zote. Kwanja ni kwamba msingi wa amani na utulivu ni wananchi kuwa na imani na vyombo vinavyo simamia na kuhakiki amani na utulivu huo; thamana hiyo ni nzito sana. Ukiangalia vijana walivyo chachamaa kulinda vituo vya uchaguzi na sehemu za kuhakiki matokeo, unajua fika watu hawana imani na vyombo vilivyopewa thamana na watawala (siyo viongozi).

Akiongea mkuu wa ma jeshi, mkuu wa TUKURURU, NEC n.k watu wanaona inaongea ngoma ya mtawala si chombo chao. Hii ni hatari kwa amani na utulivu tunaouimba kuliko hao wanaoitwa wachochezi. Watu wote waotaka mabadiliko huitwa wachochezi dunia nzima tangu enzi za Nabii Issa bin Mariam hadi kwa Mandela. Ameongea maalim Seif, ameongea Prof. Libumba, watawala wetu wasiposikiliza na kutambua maandiko ya nyakati, nyimbo za amani hazitasaidia chochote. Hakuna jeshi au vyombo vya usalama duniani vinavoweza kuzuia mabadiliko yakifika.

Tafakari.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom