Ndugu zangu,
KATIKA kuadhimisha miaka kumi ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi, CCM na miaka 20 ya Azimio la Arusha, Mwalimu Julius Nyerere alikubali kufanya mahojiano ya kipekee na ya aina yake na Mhariri wa gazeti la Uhuru. Huo ulikuwa ni mwaka 1987.
Katika mahojiano yale Mwalimu, akiwa Mwenyekiti wa CCM hakusita kutamka bayana, kuwa Chama alichokuwa akikiongoza kilikuwa na kasoro na mapungufu mengi.
Mwalimu aliona dalili za kupungua kwa moyo wa kujitolea. Aliona dalili za kupungua kwa maadili ya uongozi. Mwalimu aliona dalili za mioyo ya kimamluki ilivyoanza kuingia na kuenea ndani ya CCM na nchi yetu. Mwalimu alifikia kumtamkia mhariri yule wa gazeti; " Tumewapa uongozi watu wasiofaa. Nadhani wengi ndani ya Chama tumeanza kuutambua ubovu huu. Hatua ya kwanza kutibu maradhi ni kuyatambua." Alitamka Mwalimu.
Ndio, Mwalimu aliona mbali, hii leo viongozi wanaofanya matendo maovu na ya kimamluki ndani ya vyama vya siasa na nchi kwa ujumla ndio wale aliowatabiri Mwalimu miaka 23 iliyopita.
Ni dhahiri, kuwa demokrasia yetu bado ni changa mno. Huu ni wakati wa kuwa makini katika kujenga misingi imara ya demokrasia yetu.
Makala yangu ( Raia Mwema) juma la jana ilizungumzia amani. Nilirejea kauli ya ya Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo juu ya suala hilo. ( Mwananchi, Novemba 5, 2010)
Mwadhama Kardinali Pengo alizungumzia umuhimu wa uwepo wa amani. Katika makala yangu hayo nilikwenda mbele zaidi. Nilibainisha, kuwa pasipo haki hakuna amani. Na swali ni je, haki inapatikana vipi?
Hivyo, nikaongeza kuandika, kuwa swali tusilopaswa kujisumbua kujiuliza ni juu ya nani atakuwa Rais wetu mwaka 2015, bali, tujisumbue kwa kujiuliza; Je, Rais wetu wa 2015 tutampata kwa katiba ipi, na kwa mfumo gani wa uchaguzi? Sote, wakiwamo viongozi wa dini, tuna lazima ya kuyatafuta majibu ya maswali haya.
Kwa mfano, wenzetu kule Marekani katiba yao ina zaidi ya miaka mia mbili. Kubadili kipengele tu katika katiba ya Marekani inaweza kuwa ni mchakato wa miaka kumi. Hakuna hata Rais wa Marekani anayeweza kuichezea Katiba ya Marekani kwa maslahi yake, anaweza kuishia gerezani anayejaribu kufanya hivyo. Wamarekani wale hata wakimweka ‘mwendawazimu' Ikulu wanajua namna ya kumdhibiti kikatiba.
Ni tofauti na sisi. Mwanafalsafa Charles Montesque aliyeasisi nadharia ya mihimili mitatu ya dola alikuwa na maana pia ya kumpunguzia Rais nguvu nyingi. Wakati huo huo alitaka kuongeza nguvu kwa Bunge na Mahakama. Katika nchi zetu hizi, unapozungumzia kuliongezea nguvu Bunge na Mahakama, ina maana pia ya kutoa tafsiri ya kuipunguzia nguvu Serikali na kwa maana hiyo kumpunguzia nguvu Rais.
Hilo la mwisho ndilo hufanya nchi zetu hizi siku zote zibaki zikipiga makitaimu, ziko pale pale. Na hapo ndipo kilipo kiini cha matatizo mengi ya nchi zetu za Kiafrika. Afrika kujenga hoja za kumpunguzia nguvu za kimamlaka ‘Bwana Mkubwa' maana mara nyingi Afrika Marais ni wanaume, yaweza kuwa ni kujitafutia balaa.
Kama tuna dhamira za kweli za kuviandalia vizazi vijavyo mazingira mazuri ya kuishi, kuifurahia na kujivunia nchi yao, basi, tuna lazima ya kuandaa mazingira ya kuwapo kwa Mkutano wa Kitaifa wa Katiba. Mkutano utakaojumuisha viongozi wa makundi yote ya jamii hii. Hapo yaandaliwe mazingira ya kuandikwa kwa Katiba mpya itakayokuwa na maslahi kwa Watanzania walio wengi, na kwa miaka mingi ijayo.
Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini, kuwa tiba ya maradhi yetu tuliyoyatambua, ikiwamo ufisadi uliotamalaki, ni kuendelea kuumiza vichwa kufikiri jina la nani atakayekuwa rais 2015. Huko ni sawa na kuendelea kutwanga maji kwenye kinu.
Rai yangu; Watanzania msijiulize, nani atakuwa Rais 2015, Jiulizeni, Rais tunayemtaka 2015 tutampata kwa Katiba ipi, na kwa mfumo gani wa Uchaguzi?
Na hilo ni Neno la Leo.
Maggid,
Iringa,
Jumapili, Novemba 14, 2010
mjengwa
KATIKA kuadhimisha miaka kumi ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi, CCM na miaka 20 ya Azimio la Arusha, Mwalimu Julius Nyerere alikubali kufanya mahojiano ya kipekee na ya aina yake na Mhariri wa gazeti la Uhuru. Huo ulikuwa ni mwaka 1987.
Katika mahojiano yale Mwalimu, akiwa Mwenyekiti wa CCM hakusita kutamka bayana, kuwa Chama alichokuwa akikiongoza kilikuwa na kasoro na mapungufu mengi.
Mwalimu aliona dalili za kupungua kwa moyo wa kujitolea. Aliona dalili za kupungua kwa maadili ya uongozi. Mwalimu aliona dalili za mioyo ya kimamluki ilivyoanza kuingia na kuenea ndani ya CCM na nchi yetu. Mwalimu alifikia kumtamkia mhariri yule wa gazeti; " Tumewapa uongozi watu wasiofaa. Nadhani wengi ndani ya Chama tumeanza kuutambua ubovu huu. Hatua ya kwanza kutibu maradhi ni kuyatambua." Alitamka Mwalimu.
Ndio, Mwalimu aliona mbali, hii leo viongozi wanaofanya matendo maovu na ya kimamluki ndani ya vyama vya siasa na nchi kwa ujumla ndio wale aliowatabiri Mwalimu miaka 23 iliyopita.
Ni dhahiri, kuwa demokrasia yetu bado ni changa mno. Huu ni wakati wa kuwa makini katika kujenga misingi imara ya demokrasia yetu.
Makala yangu ( Raia Mwema) juma la jana ilizungumzia amani. Nilirejea kauli ya ya Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo juu ya suala hilo. ( Mwananchi, Novemba 5, 2010)
Mwadhama Kardinali Pengo alizungumzia umuhimu wa uwepo wa amani. Katika makala yangu hayo nilikwenda mbele zaidi. Nilibainisha, kuwa pasipo haki hakuna amani. Na swali ni je, haki inapatikana vipi?
Hivyo, nikaongeza kuandika, kuwa swali tusilopaswa kujisumbua kujiuliza ni juu ya nani atakuwa Rais wetu mwaka 2015, bali, tujisumbue kwa kujiuliza; Je, Rais wetu wa 2015 tutampata kwa katiba ipi, na kwa mfumo gani wa uchaguzi? Sote, wakiwamo viongozi wa dini, tuna lazima ya kuyatafuta majibu ya maswali haya.
Kwa mfano, wenzetu kule Marekani katiba yao ina zaidi ya miaka mia mbili. Kubadili kipengele tu katika katiba ya Marekani inaweza kuwa ni mchakato wa miaka kumi. Hakuna hata Rais wa Marekani anayeweza kuichezea Katiba ya Marekani kwa maslahi yake, anaweza kuishia gerezani anayejaribu kufanya hivyo. Wamarekani wale hata wakimweka ‘mwendawazimu' Ikulu wanajua namna ya kumdhibiti kikatiba.
Ni tofauti na sisi. Mwanafalsafa Charles Montesque aliyeasisi nadharia ya mihimili mitatu ya dola alikuwa na maana pia ya kumpunguzia Rais nguvu nyingi. Wakati huo huo alitaka kuongeza nguvu kwa Bunge na Mahakama. Katika nchi zetu hizi, unapozungumzia kuliongezea nguvu Bunge na Mahakama, ina maana pia ya kutoa tafsiri ya kuipunguzia nguvu Serikali na kwa maana hiyo kumpunguzia nguvu Rais.
Hilo la mwisho ndilo hufanya nchi zetu hizi siku zote zibaki zikipiga makitaimu, ziko pale pale. Na hapo ndipo kilipo kiini cha matatizo mengi ya nchi zetu za Kiafrika. Afrika kujenga hoja za kumpunguzia nguvu za kimamlaka ‘Bwana Mkubwa' maana mara nyingi Afrika Marais ni wanaume, yaweza kuwa ni kujitafutia balaa.
Kama tuna dhamira za kweli za kuviandalia vizazi vijavyo mazingira mazuri ya kuishi, kuifurahia na kujivunia nchi yao, basi, tuna lazima ya kuandaa mazingira ya kuwapo kwa Mkutano wa Kitaifa wa Katiba. Mkutano utakaojumuisha viongozi wa makundi yote ya jamii hii. Hapo yaandaliwe mazingira ya kuandikwa kwa Katiba mpya itakayokuwa na maslahi kwa Watanzania walio wengi, na kwa miaka mingi ijayo.
Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini, kuwa tiba ya maradhi yetu tuliyoyatambua, ikiwamo ufisadi uliotamalaki, ni kuendelea kuumiza vichwa kufikiri jina la nani atakayekuwa rais 2015. Huko ni sawa na kuendelea kutwanga maji kwenye kinu.
Rai yangu; Watanzania msijiulize, nani atakuwa Rais 2015, Jiulizeni, Rais tunayemtaka 2015 tutampata kwa Katiba ipi, na kwa mfumo gani wa Uchaguzi?
Na hilo ni Neno la Leo.
Maggid,
Iringa,
Jumapili, Novemba 14, 2010
mjengwa