Nenda Gavana Luoga, uliipeleka Tanzania uchumi wa kati

Kulwa Jilala

JF-Expert Member
Sep 6, 2022
3,510
7,755
Gavana profesa Florence Luoga amemaliza muda wake kwa mujibu wa sheria za utumishi pale benki kuu, lakini jina lake litapakwa wino wa dhahabu kwa utumishi wake uliotukuka. Ni katika kipindi cha Gavana Luoga sheria za fedha na uchumi wa Tanzania vilisimamiwa kwelikweli kwa vitendo na siyo kwa maneno na kupelekea Tanzania kuingia uchumi wa kati mapema zaidi mwaka 2020 kuliko ilivyokuwa imetabiriwa na mabeberu kuwa Tanzania itaingia uchumi wa kati 2025.

Wazalendo wa nchi yetu ya Tanzania tunaamini bila uthubutu na ujasiri wako Prof Luoga isingewezekana kupata hayo mafanikio ndani ya muda mfupi hivyo.

20230108_195713.jpg
Screenshot_20230108-195606_YouTube.jpg
 
Moja ya vitu ambavyo atakumbukwa ni issue ya Maduka ya kubadilishia fedha! Ijapokuwa wapo walioumia ila ukweli ni kuwa yale maduka yalikuwa ni uchochoro wa kupitishia fedha.

Jambo lengine ambalo nitamkumbuka kuifanya Tsh iwe na stable.
Umenena vyema
 
Moja ya vitu ambavyo atakumbukwa ni issue ya Maduka ya kubadilishia fedha! Ijapokuwa wapo walioumia ila ukweli ni kuwa yale maduka yalikuwa ni uchochoro wa kupitishia fedha.

Jambo lengine ambalo nitamkumbuka kuifanya Tsh iwe na stable.
huna exposure nchi za nje maduka ya kubadilisha pes za kigeni ni mengi na yamejaa kila kona
 
Back
Top Bottom