NEMC yaitoza Lake Oil faini ya bilioni 3.3 kwa kutozingatia utunzaji wa mazingira

Ok ..wale jamaa hawana haraka . wakijenga wanajenga kweli Pia huduma zao ziko high quality
Ok ..wale jamaa hawana haraka . wakijenga wanajenga kweli Pia huduma zao ziko high quality
Sijapata wasaa nao ila all i need is wese lisiloungua haraka kama ilivyo lake oil! Madala dala na boda boda wote wanakimbilia kule sababu inawalipa 😅😅😅😅😅 huwezi kuta dala dala anajaza wese Total
 
Dah kuna kituo cha mafuta mwanza nimekisahau jina kipo geti la nyumba la kuingia Rock City mall aisee ni kikali balaaa
 
Duh low quality tena?

We ubora wa sheli kwako ni branding? Sababu kwa branding iliosimamia ukucha ni Oryx na Total tu station zao zina mvuto wa kimataifa😋!

Ila kwa mafuta mie hupendelea Lake oil zaidi sababu yanadumu kwa muda mrefu zaidi kwenye tank
umeongea point sana.. kuna issue ya branding halafu kuna issue ya ubora wa mafuta... watu wanadhani masheli yaliyorembeka vizuri ndo yana mafuta mazuri kitu ambacho sio
 
:D:Dcomedy, watendaji wa ardhi mipango miji, halmashauri wamekalia kupokea bahasha tu, huku mtu anajenga, kuna kituo cha Lakeoil Mbagala, AISEE! Kipewe tuzo, kiko sehemu HATARISHI hatuombei ila kikilipuuuukaaah!

Tutakuja kulaumiana kwanini hawakuambiwa wakivunje. Faini haitoshi vingine wavunje, Al-Saedy Morogoro kajenga kituo ukuta unapakana na nyumba, Abood kajenga kituo shule ya Msingi Msamvu haiko mbali, basi tuzidi kumtegemea Mungu.

Everyday is Saturday................................:cool:
 
Kabla Kituo cha Mafuta hakijajengwa, kuna vibali lazima mtu uwe navyo, na cha kwanza kabisa inakuaga EIA (Environmental Impact Assessment) ambacho hao hao NEMC ndio wanakitoa.

Sasa kweli mtu ajenge Letrol station bila kibali iko?
 
Nimeona mpaka katikati ya makazi wamejenga aisee.. Ila NEMC walikuwa wapi? Vibali vya ujenzi vilitokaje bila kuwashirikisha? Je baada ya kulipa faini watavunja au wataendelea na biashara?
Biashara ya kujenga Fuel pump sio kama hivyo kaka, sheria inataka usiendeleze eneo hata kufyeka bila kupata kibali, sasa ukute walishapata eneo wakaanza matengenezo madogo ndipo hapo NEMC wanakula 20M kwa kila kituo
Sio kwamba biashara haitaendelea, itaendelea ila hiyo sheria ni ya moto usipime.
 
Nimeona mpaka katikati ya makazi wamejenga aisee.. Ila NEMC walikuwa wapi? Vibali vya ujenzi vilitokaje bila kuwashirikisha? Je baada ya kulipa faini watavunja au wataendelea na biashara?
Wakishalipa basi watasajiliwa rasmi Kama wadau wakubwa wa maendeleo
 
Wanabodi kuna hii Taarifa nimeiona Kwenye media zingine ikisema Shirika la Mazingira Nchini NEMC Limeitoza Kampuni ya Lake Oil Fine ya Tsh Bil 3.3 kwa kujenga vituo vingi sehemu tofauti za Nchi bila Kibali.

Hili limekua kama mshituko hasa kwa kuzingatia ukweli kwamba suala la mipango miji nchini hapa sio kipaumbele. Au Wengi wetu hatuzingatii.

Ni vyema kutimiza wajibu kuepuka matatizo makubwa kama haya. Bil 3 naamini ni hela nyingi sana kwa kampuni yeyote.
Kutii sheria na kufuata taratibu ni jambo la msingi sana.

=====

NEMC iimeagiza kampuni ya mafuta ya Lake Oil kulipa faini hiyo ndani ya siku 14 la sivyo itaamuru kufungwa kwa vituo vyake vya mafuta 66 kote nchini, ikitoa mfano wa vifungu vya sheria vinavyohusika. Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt Samuel Gwamaka aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa baraza hilo lilifikia uamuzi huo kufuatia malalamiko mengi ya umma katika maeneo ambayo vituo vya mafuta vilijengwa.

"Tunaendelea na uchunguzi kwa wamiliki wengine wa vituo vya mafuta na wale watakaobainika wamejenga vituo vya mafuta bila vyeti vya EIA watatozwa faini. Hiyo ni kwa mujibu wa sheria, kwani tumegundua kuwa vituo vya mafuta vimekuwa vikiongezeka kila mahali. Hatuwezi kuendelea kuwakumbusha wamiliki wake juu ya majukumu yao kwani tumeshafanya mengi tayari, ”alisema.

Alitoa siku saba kwa wamiliki wa vituo vya mafuta vilivyojengwa bila vyeti vya EIA kuripoti kwa ofisi za NEMC kuelezea ni kwanini hatua hazipaswi kuchukuliwa dhidi yao. Ni miaka 17 tangu sheria ya sasa ya mazingira itungwe na NEMC imekuwa ikitoa elimu kwa njia anuwai. Lakini wamiliki wengi wa vituo vya mafuta walipuuza maagizo haya, kwa hivyo wakati wa kuchukua hatua umewadia, alisema zaidi.

"Kuna vituo vya mafuta karibu 3,000 kote nchini lakini ni 600 tu ndio wameandikisha tathmini ya athari za mazingira. Kujenga vituo vya mafuta bila EIA ni hatari kwa watu katika eneo hilo ikiwa kuna dharura, kwa hivyo hatuwezi kuvumilia hii tena, ”alisisitiza. "Kila mtu anaona jinsi vituo vya mafuta vinavyoenea kila mahali, na NEMC imekuwa ikijiuliza ni kwanini wamiliki hawaripoti katika ofisi za NEMC kujiandikisha na kupata EIA,". mkurugenzi alibaini.

Alisema kanuni zinahitaji kwamba umbali kati ya kituo kimoja cha mafuta na kingine haipaswi kuwa chini ya mita 200 ili kuepuka dharura za moto, lakini wajenzi wa kituo cha mafuta wamekuwa hawazingatii mahitaji haya, alisema. Wamiliki wengi wa vituo vya mafuta huunda vituo vyao na kisha hutafuta vyeti vya EIA, na mara nyingi akitaka kuhonga maafisa wanaohusika, alishtaki, akibainisha pia kwamba watu wanaoishi karibu na mahali kituo cha mafuta kina haki ya kushiriki katika kukuza ufahamu juu ya nini cha kufanya ikiwa kuna dharura ya moto .. Kuhitaji wakaazi wa thst kuhusika wakati wa kutoa vibali vya EIA inakusudiwa kuwawezesha kujua juu ya hatari za kiafya wanazopaswa kuishi nazo, ameongeza.
Industrial espionage na Industrial sabotage ni vitu viwili vinavyofanya kazi pamoja,kama vile uchawi na majini huwa haviachani sana,ukiona mtu au Kampuni inapigwa faini ya mabilioni kunakuwa na maswali ya kufikirisha.
 
lake oil hawatalipa fine na wataendelea kufanya biashara zao Nemc hawajui hiyo biashara ni ya mzee Mh yumo humo utaona hii habari itakuwa kimyaa wala hutoisikia tena ya fine au ya kufunga vituo
 
UKITAKA KUJENGA LAZIMA UPATE KIBALI ANAYEKUPA KIIBALI LAZIMA AWE AMEJIRIDHISHA KUWA UMEKIDHI VIGEZO VYOTE SASA BASI LAKE OIL MSILIPE ANAYETAKIWA KULIPA NI MKURUGENZI ALIYETOA KIBALI CHA KUJENGA KITUO CHA MAFUTA
 
UKITAKA KUJENGA LAZIMA UPATE KIBALI ANAYEKUPA KIIBALI LAZIMA AWE AMEJIRIDHISHA KUWA UMEKIDHI VIGEZO VYOTE SASA BASI LAKE OIL MSILIPE ANAYETAKIWA KULIPA NI MKURUGENZI ALIYETOA KIBALI CHA KUJENGA KITUO CHA MAFUTA
Kibali cha kujenga na EIA report ni vitu viwili tofauti

Tambua EIA ina kagua athari za maradi husika ktk mazingira sasa mbali na EIA kuna ukaguzi mwingine hufanyika baada ya mradi kuamza kazi kwa kipindi fulani endapo ikionekana una viashiria vya uchafuzi wa mazingira kwa kimombo wanasema Environmental audit (EA)

Sasa ikibainika mradi unachafua mazingira hapo lazima ulipe faini ya fedha

EIA hufanyika kabla ya mradi kuanza
 
Back
Top Bottom