tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,799
- 18,224
Hata kama serikali haina dini lakini hapa tulipofika sasa kuna haja ya serikali kuingilia kati. Hapa mtaani kwangu leo hakukaliki kwa sababu ya kelele za maspika ya ibada. NEMC walisema wataweka utaratibu wa kufanya ibada lakini sijui wanakwama wapi mpaka sasa hawajachukua hatua zozote. Hadi natamani niuze nyumba hii nihamie mkoa mwingine.
Kuna nyumba nne za ibada kuzunguka makazi yangu na kila nyumba ina spika nne – kila spika imetazama upande mmoja wa dunia (kusini, kaskazini, magharibi na mashariki). Jumla ya maspika ni 16 na wote wanahubiri kwa wakati mmoja, tena kwa sauti kubwa sana. Wewe fikiria maspika 16 yamekuweka kati na yote yanaunguruma kwa wakati mmoja! Kuna kusikilizana hapo?
Halafu leo ni kama vile wameamua kuongeza sauti kwa makusudi ili kutukomesha. Nipo hapa nafanya kazi zangu za kujenga taifa lakini nahisi kichwa kinawaka moto. Sasa kama watu wanaohubiriwa wapo ndani ya nyumba ya ibada kuna haja gani ya kuning’iniza maspika juu ya paa kama sio ukorofi?
Na hapo bado kesho na keshokutwa wenzetu watakapoungurumisha mavinanda na kuimba mapambio. Na wao nyumba zao za ibada zipo hapa hapa jirani. Ni kero kubwa sana kwa kweli, hasa unapokuwa unafanya kazi inayohitaji utulivu.
Naomba NEMC waingilie kati mara moja kwa kuweka utaratibu wa ibada wa kiistarabu badala ya huu utaratibu wa ovyo wa kuhanikiza kelele mtaa mzima.
Pia soma:
Kuna nyumba nne za ibada kuzunguka makazi yangu na kila nyumba ina spika nne – kila spika imetazama upande mmoja wa dunia (kusini, kaskazini, magharibi na mashariki). Jumla ya maspika ni 16 na wote wanahubiri kwa wakati mmoja, tena kwa sauti kubwa sana. Wewe fikiria maspika 16 yamekuweka kati na yote yanaunguruma kwa wakati mmoja! Kuna kusikilizana hapo?
Halafu leo ni kama vile wameamua kuongeza sauti kwa makusudi ili kutukomesha. Nipo hapa nafanya kazi zangu za kujenga taifa lakini nahisi kichwa kinawaka moto. Sasa kama watu wanaohubiriwa wapo ndani ya nyumba ya ibada kuna haja gani ya kuning’iniza maspika juu ya paa kama sio ukorofi?
Na hapo bado kesho na keshokutwa wenzetu watakapoungurumisha mavinanda na kuimba mapambio. Na wao nyumba zao za ibada zipo hapa hapa jirani. Ni kero kubwa sana kwa kweli, hasa unapokuwa unafanya kazi inayohitaji utulivu.
Naomba NEMC waingilie kati mara moja kwa kuweka utaratibu wa ibada wa kiistarabu badala ya huu utaratibu wa ovyo wa kuhanikiza kelele mtaa mzima.
Pia soma:
KKKT DMP kuondoa Spika kubwa kwenye Makanisa yake ili Kudhibiti makelele, yasema kupigiana makelele ni " Ushamba"
Kanisa la KKKT DMP limesema litaondoa Spika kubwa kwenye Makanisa yake yote kuitikia wito wa NEMC wa kupambana na Uharibifu wa Mazingira Kwa sasa takribani Makanisa 9 ya KKKT DMP yana Kesi NEMC zilizofunguliwa na Majirani zao Naye askofu wa KKKT DMP Dr Malasusa amesema wakati mwingine haya...
www.jamiiforums.com