NEMC na Polisi Watoe namba za wazi kwaajili ya kupokea taarifa kutoka kwa wananchi

Faana

JF-Expert Member
Dec 12, 2011
31,821
33,205
Hivi karibuni Mkurugenzi wa NEMC alitangaza uwepo wa ssheria ya kuzuia kelele na mitetemo kwenye makazi ya watu, kadhalika Waziri wa mambo ya ndani alirudia tangazo hilo na kuwataka wanaopiga muziki kwa sauti kubwa kuacha mara moja ama kufunga vizuia sauti.

Inaelekea maagizo hayo yote mawili, lile la Mkurugenzi wa NEMC na Waziri Lugola yamepuuzwa, labda kwasababu hakuna anayefanyia kazi maagizo hayo.

Ushauri: NEMC wanunue vifaa maalumu vinavyoweza kupima viwango vya kelele vilivyozidi kiasi kinachokubalika na kuajiri vijana watakaozunguka mitaani na kusoma kelele hizo kisha kutoa taarifa kwa mamlaka husika, hii itakuwa na faida mbili, moja ni ajira kwa waliokosa ajira na watalipwa kutokana na tozo zitakazopatikana, mbili serikali itaongeza mapato kutokana na adhabu kwa wanaokiuka maagizo ya viongozi husika.
POLICE: Watoe namba za wazi kwaajili ya kupokea taarifa kutoka kwa wananchi waliopo kwenye maeneo yenye viwango vya kelele vilivyokatazwa.

Nawasilisha
 
Sisi watu wa burudani wana tuonea sana mziki wana ita ni kelele yaani wazee sugu King kiki nyimbo zake ni kelele kweli?
 
Sisi watu wa burudani wana tuonea sana mziki wana ita ni kelele yaani wazee sugu King kiki nyimbo zake ni kelele kweli?


Mkuu hata ugali una sehemu yake ya kuliwa, hauliwi hovyohovyo tu ati uliwe njiani maliwatoni...
 
Kumbi zilizo mbali na makazi kwa dar hakuna pili hakuna kumbi za kisasa za kumeza sauti

Ndipo hapo tunawalalamikia wenye mamlaka ya kudhibiti hali hiyo watimize wajibu wao kuondoa adha hiyo kwa raia
 
Hivi karibuni Mkurugenzi wa NEMC alitangaza uwepo wa ssheria ya kuzuia kelele na mitetemo kwenye makazi ya watu, kadhalika Waziri wa mambo ya ndani alirudia tangazo hilo na kuwataka wanaopiga muziki kwa sauti kubwa kuacha mara moja ama kufunga vizuia sauti.

Inaelekea maagizo hayo yote mawili, lile la Mkurugenzi wa NEMC na Waziri Lugola yamepuuzwa, labda kwasababu hakuna anayefanyia kazi maagizo hayo.

Ushauri: NEMC wanunue vifaa maalumu vinavyoweza kupima viwango vya kelele vilivyozidi kiasi kinachokubalika na kuajiri vijana watakaozunguka mitaani na kusoma kelele hizo kisha kutoa taarifa kwa mamlaka husika, hii itakuwa na faida mbili, moja ni ajira kwa waliokosa ajira na watalipwa kutokana na tozo zitakazopatikana, mbili serikali itaongeza mapato kutokana na adhabu kwa wanaokiuka maagizo ya viongozi husika.
POLICE: Watoe namba za wazi kwaajili ya kupokea taarifa kutoka kwa wananchi waliopo kwenye maeneo yenye viwango vya kelele vilivyokatazwa.

Nawasilisha

Napenda kujua endapo NEMC ina network ya ofisi katika kila Mkoa / wilaya? pia je ina uwezo wa kuajiri vijana wa kupima hizo kelele Tanzania mzima na kama haiwezekani nini kifanyike ili kudhibiti kelele hizo?
 
Napenda kujua endapo NEMC ina network ya ofisi katika kila Mkoa / wilaya? pia je ina uwezo wa kuajiri vijana wa kupima hizo kelele Tanzania mzima na kama haiwezekani nini kifanyike ili kudhibiti kelele hizo?


Just a matter of creativity, wajipange tu hakuna kinachoshindikana
 
Itabidi washirikishe vituo vya Police kila kata na wawe na chombo hicho cha kupimia kelele?


Mkuu, ukiozeshwa mke hufundishwi cha kwenda kufanya naye, unajiongeza mweneywe, na wao NEMC na Polisi wajiongeze.
 
Back
Top Bottom