Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,304
- 12,965
Moja kwa moja kwenye mada.
Nashauri Baraza la Taifa la usimamizi wa Mazingira NEMC na Tume ya Taifa ya uchaguzi NEC kuweka muda maalumu kwa vyama kuondoa mabango na matangazo yote ya kampeni baada ya uchaguzi ili kuweka mazingira safi.
Sasa hivi uchaguzi umekwisha lakini mitaani, barabarani, kwenye vituo vya mabasi na nguzo za taa kumejaa mabango ya wagombea kana kwamba bado tupo kwenye kampeni. Baada ya uchaguzi yote hayo huwa ni uchafu hivyo ni lazima kuondolewa.
Vile vile kuwe na marufuku ya kuvaa nguo za kampeni kama kapelo, tshirts, vilemba na kanga baada ya uchaguzi kwani ni kujidhalilisha na kutojua maana na pia ni uchafuzi wa mazingira.
Yaani mpaka leo unakuta mtu kavaa kapelo au tshirt ya CHAGUA MKAPA au CHAGUA KIKWETE au CHAGUA MAGUFULI au ARI MPYA, NGUVU MPYA, KASI MPYA. Hayo yote iwe ni marufuku.
Mimi nashauri kuwe na sheria inayouazimishaviwanda vinavyo tengeza nguo za kampeni kutengeneza zile zitakazo dumu kwa muda usio zidi siku 70. Yaani ziwe zina expire ndani ya muda huo ili kuwakomoa wanaoendelea kuvaa hata baada ya uchaguzi. Yaani baada ya muda huo mtu akivaa tshirt au kanga au kapelo iwe inageuka lami na kuganda mwilini au akifua iwe inachanika na akianika iwe inageuka jivu. Kwa mtindo huu tutakuwa tunalinda mazingira kutokana na uchafu unaotokana na shughuli za uchaguzi.
Naomba kutoa hoja!
Nashauri Baraza la Taifa la usimamizi wa Mazingira NEMC na Tume ya Taifa ya uchaguzi NEC kuweka muda maalumu kwa vyama kuondoa mabango na matangazo yote ya kampeni baada ya uchaguzi ili kuweka mazingira safi.
Sasa hivi uchaguzi umekwisha lakini mitaani, barabarani, kwenye vituo vya mabasi na nguzo za taa kumejaa mabango ya wagombea kana kwamba bado tupo kwenye kampeni. Baada ya uchaguzi yote hayo huwa ni uchafu hivyo ni lazima kuondolewa.
Vile vile kuwe na marufuku ya kuvaa nguo za kampeni kama kapelo, tshirts, vilemba na kanga baada ya uchaguzi kwani ni kujidhalilisha na kutojua maana na pia ni uchafuzi wa mazingira.
Yaani mpaka leo unakuta mtu kavaa kapelo au tshirt ya CHAGUA MKAPA au CHAGUA KIKWETE au CHAGUA MAGUFULI au ARI MPYA, NGUVU MPYA, KASI MPYA. Hayo yote iwe ni marufuku.
Mimi nashauri kuwe na sheria inayouazimishaviwanda vinavyo tengeza nguo za kampeni kutengeneza zile zitakazo dumu kwa muda usio zidi siku 70. Yaani ziwe zina expire ndani ya muda huo ili kuwakomoa wanaoendelea kuvaa hata baada ya uchaguzi. Yaani baada ya muda huo mtu akivaa tshirt au kanga au kapelo iwe inageuka lami na kuganda mwilini au akifua iwe inachanika na akianika iwe inageuka jivu. Kwa mtindo huu tutakuwa tunalinda mazingira kutokana na uchafu unaotokana na shughuli za uchaguzi.
Naomba kutoa hoja!