Taarifa kutoka katika vyombo mbalimbali vya habari vinasema mmoja wa baba wa Afrika, raisi wa kwanza wa Afrika ya kusini, Nelson Mandela, amefariki dunia.
Rest in Peace Nelson Mandela.
May the lord in heaven forgive your sins and accept you into his eternal life.
Kazi uliyotumwa na bwana ya kuwapigania weusi dhidi ya utawala dhalimu wa ubaguzi wa rangi kutoka kwa wakoloni wa kizungu ulishaimaliza Siku nyingi, kapumzike kwa amani mzee wetu Nelson Mandela. Amen!
Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, amefariki dunia. Kifo chake kimetangazwa na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma jana usiku. Mandela amefariki dunia nyumbani kwake mjini Johannesburg.
Wewe itakuwa unategemea kupata habari kutoka TBC otherwise usingepost habari hii saa hizi ambayo vyombo vya kimataifa vimeireport masaa 6 yaliopita wakati TBC ikiendelea na mirindimo ya pwani ya Asha mashauzi.
Inauma sana tu watu wazuri wanafariki ila wabaya wanadunda tu uraiani. kama wangekuwa wanaonana naamini atakua na jamaa ake Mwalimu JK anamjuza kitu gani kiliendelea Afrika hasa hasa Tanzania baada ya kufa kwake.
Umeikamilisha safari yako ndefu na yenye misukosuko mingi kwa mafanikio makubwa, Naam mwili umekufa lakini bado utaendelea kuishi mioyoni mwa wengi vizazi vingi vijavyo, Mwenyezi Mungu akusamehe Makosa yako kama binadamu na Akupumzishe Rahani mwake kwa amani. BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA, JINA LAKE LIHIMIDIWE.
inahuzunisha sana madiba hatunaye tena kitu muhimu kujifunza kwake ni uhuru na kusamehe ndio ilikuwa nguzo yake kubwa katika utawala wake na maisha yake
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.