WilsonKaisary
JF-Expert Member
- Apr 4, 2017
- 392
- 935
Kwa takribani miaka 27 Nelson Mandela (Tata/Madiba) amekuwa gerezani Hadi mwaka 1990 alipoachiwa.
Hadi kufikia mwaka 1990 nchi zote za kiafrika zilikuwa zimepata Uhuru kutoka kwa wakoloni. Ikumbukwe Afrika Kusini ilipata Uhuru wake mnamo 1931, mwaka 1994 haukuwa mwaka wa kupata Uhuru kwa Afrika Kusini bali ilikuwa end of Apartheid.
Mchango wa Nelson Mandela kwenye harakati za kusaidia bara la Afrika kujikomboa Ni mdogo Sana. Ni tofauti sana na ule Hayati baba wa taifa Mwalimu Julius .K. Nyerere aliyeifanya Tanzania kambi kuu ya wapigania uhuru Kama Robert Mugabe (Zimbabwe), Sam Nujoma (Namibia), Mozambique (Samora Machel, Eduardo Mondlane),Afrika Kusini yenyewe n.k
Katika Historia ya ukombozi wa Afrika mchango wa Nelson Mandela ni mdogo Sana.
1: Kipi kilichompelekea mpaka kupata tuzo ya amani ya Nobel?
2: Kipi kilicho pelekea kuonekana kiongozi mashuhuri na Bora kwa Afrika nzima?
3: Umaarufu wake umepikwa na wabepari?
4: kwa Nini sio J.K Nyerere na Ni Nelson Mandela?
5: Nyuma ya heshima ya kimataifa aliyopewa Nelson Mandela ni Nini?
6: Ni kweli Nelson Mandela aliingia makubaliano ya Uhuru kwa wa-afrika?
7: Toka mwisho wa Apartheid ni kipi kimebadilika kwa wa-afrika Kusini? Ardhi umerudi kwa wa-afrika Kusini? Serikali ya Afrika Kusini inayo kauli asilimia Mia juu ya ardhi yake?
Ni maswali ya kujiuliza sana na Ni maswali ya kupatia ufumbuzi.
Na hi ni tokana na mchango mdogo Sana wa Nelson Mandela hususa kwenye harakati za Afrika.
Mnamo mwaka 2009 umoja wa mataifa ulisimika tarehe 18 ya mwezi wa 7 kuwa sikukuu ya kimaitaifa ikiitwa Mandela day na ndio siku ya kuzaliwa kwa Mandela, kwa lengo la kumhenzi Mandela.
How Nelson Mandela betrayed us, says ex-wife Winnie