Negro Tom: Mtumwa wa Kiafrika aliyekuwa na uwezo wa ajabu wa kufanya Hesabu kichwani kiasi cha kuitwa 'Calculator'

Farolito

JF-Expert Member
Sep 10, 2018
11,634
26,373
Jina lake halisi ni Thomas Fuller, Mwafrika aliyezaliwa huko Benin mwaka 1710 na kuuzwa utumwani huko Alexandria,Virginia USA mwaka 1724 akiwa na mika 14.

Alipewa jina la "Virginia Calculator" kutokana na uwezo wake wa ajabu wa kufanya kufanya mahesabu magumu kichwani.

Mfano aliulizwa kuna sekunde ngapi katika mwaka mmoja na nusu?ndani ya dakika mbili alijibu kwa usahihi kwamba ni 47,304,000.
Aliulizwa tena mtu mwenye miaka 70 Siku 17 na saa 12 ameishi kwa sekunde ngapi?Ndani ya dk moja na nusu aliweza kujibu kwa usahihi kwamba ni sekunde 2,210,500,800.

Hio ni mifano michache tu kati ya mingi ambayo Negro Tom aliweza kujaribiwa kujua uwezo wake lakini alikuwa akifanya maajabu mengi tu ya kimahesabu kichwani.

Alikuwa na uwezo wa kufanya hesabu ya tarakimu tisa uizidishe kwa Tisa au saba izidishwe kwa saba na jibu lake lizidishwe kwa saba iende hivo mpaka Mara saba kichwani na akatoa jibu sahihi kwa muda mfupi tena akiwa kazungukwa na watu huku wakimkatisha kwa maswali na kelele na hapa na pale lakini alikuwa na uwezo wa kuwajibu kisha kurudia pale alipoishia na kutoa jibu.

Pia alikuwa na uwezo wa kufanya hesabu hizo huku kichwani akijumlisha au kutoa miaka mirefu na mifupi, kuhesabu idadi ya nywele kwenye mikia ya ngo'mbe, farasi nk.

Kilichowashangaza zaidi wengi ni kwamba Negro Tom pamojana na kufanya mahesabu magumu hivyo hakuwahi kujua kusoma na kuandika mpaka alipofariki mwaka 1790 akiwa na miaka 80 huko Virginia USA.

Je, Waafrika huu uwezo tuliupotezea wapi mpaka wazungu wanajidai kwamba wapo juu kuliko watu weusi?

IMG_20220207_113747.jpg
 
Mtumwa kuacha mbegu sidhani,atampata wapi demu?

Mkuu,

Watumwa walizaana ndio maana mpaka leo kuna watu weusi marekani, Brazili, colombia, Venezuela, jamaica, Cuba, Haiti, Barbados, Dominica, and the Caribbeans.

Wangekuwa hawaruhusiwi kuzaana ungekuta kizazi cha hawa Wamarekani weusi kimeshafutika siku nyingi sana!

Mfano mzuri ni nchi za kiarabu ambapo licha ya watumwa weusi wengi kupelekwa kufanyakazi za ndani na nyinginezo kule uarabuni lakini wanaume weusi wote waliopelekwa uarabuni walihasiwa ili wasiweze kuzaa! Hivyo kizazi cha watu weusi waliopelekwa kule kilipotea kabisa.

Argentina pia ilikuwa na watu weusi kama brazili na colombia lakini wao waliwatumia watu weusi kwenye mstari wa mbele vitani, kisha waliobaki waliuawa baada ya matumizi yao Kwisha! Very sad story but ndio hivyo bora hata marekani waliwaacha kidogo waendelee kuishi hata kama katika mazingira magumu ya ubaguzi, lakini wapo, ni bora kuliko kuwaua au kuwavunja nguvu za kiume ili kukomesha kizazi chao kama kule uarabuni.
 
Mkuu,

Watumwa walizaana ndio maana mpaka leo kuna watu weusi marekani, Brazili, colombia, Venezuela, jamaica, Cuba, Haiti, Barbados, Dominica, and the Caribbeans.

Wangekuwa hawaruhusiwi kuzaana ungekuta kizazi cha hawa Wamarekani weusi kimeshafutika siku nyingi sana!

Mfano mzuri ni nchi za kiarabu ambapo licha ya watumwa weusi wengi kupelekwa kufanyakazi za ndani na nyinginezo kule uarabuni lakini wanaume weusi wote waliopelekwa uarabuni walihasiwa ili wasiweze kuzaa! Hivyo kizazi cha watu weusi waliopelekwa kule kilipotea kabisa.

Argentina pia ilikuwa na watu weusi kama brazili na colombia lakini wao waliwatumia watu weusi kwenye mstari wa mbele vitani, kisha waliobaki waliuawa baada ya matumizi yao Kwisha! Very sad story but ndio hivyo bora hata marekani waliwaacha kidogo waendelee kuishi hata kama katika mazingira magumu ya ubaguzi, lakini wapo, ni bora kuliko kuwaua au kuwavunja nguvu za kiume ili kukomesha kizazi chao kama kule uarabuni.
Uko sahihi,ila huyu jamaa nimejaribu kuangalia mitandaoni sijaona kama alikuwa na watoto au mke,huenda hakuacha kizazi chake.
 
Jina lake halisi ni Thomas Fuller, Mwafrika aliyezaliwa huko Benin mwaka 1710 na kuuzwa utumwani huko Alexandria,Virginia USA mwaka 1724 akiwa na mika 14.

Alipewa jina la "Virginia Calculator" kutokana na uwezo wake wa ajabu wa kufanya kufanya mahesabu magumu kichwani.

Mfano aliulizwa kuna sekunde ngapi katika mwaka mmoja na nusu?ndani ya dakika mbili alijibu kwa usahihi kwamba ni 47,304,000.
Aliulizwa tena mtu mwenye miaka 70 Siku 17 na saa 12 ameishi kwa sekunde ngapi?Ndani ya dk moja na nusu aliweza kujibu kwa usahihi kwamba ni sekunde 2,210,500,800.

Hio ni mifano michache tu kati ya mingi ambayo Negro Tom aliweza kujaribiwa kujua uwezo wake lakini alikuwa akifanya maajabu mengi tu ya kimahesabu kichwani.

Alikuwa na uwezo wa kufanya hesabu ya tarakimu tisa uizidishe kwa Tisa au saba izidishwe kwa saba na jibu lake lizidishwe kwa saba iende hivo mpaka Mara saba kichwani na akatoa jibu sahihi kwa muda mfupi tena akiwa kazungukwa na watu huku wakimkatisha kwa maswali na kelele na hapa na pale lakini alikuwa na uwezo wa kuwajibu kisha kurudia pale alipoishia na kutoa jibu.

Pia alikuwa na uwezo wa kufanya hesabu hizo huku kichwani akijumlisha au kutoa miaka mirefu na mifupi, kuhesabu idadi ya nywele kwenye mikia ya ngo'mbe, farasi nk.

Kilichowashangaza zaidi wengi ni kwamba Negro Tom pamojana na kufanya mahesabu magumu hivyo hakuwahi kujua kusoma na kuandika mpaka alipofariki mwaka 1790 akiwa na miaka 80 huko Virginia USA.

Je, Waafrika huu uwezo tuliupotezea wapi mpaka wazungu wanajidai kwamba wapo juu kuliko watu weusi?
Huyu alikuwa na autism, watu wa aina hii ndiyo huwa wana uwezo wa kufanya kitu fulani kiajabu sana. Kama ni muziki basi utashangaa akisikia muziki fulani mara moja tu anauelewa wote, na kama ni mahesabu basi atafanya macalculation ya ajabu ambayo binaadamu wa kawaida hawezi.

Kuna filam moja ya kihindi 'My name is Khan' na yeye ana autism basi alionyesha kipaji cha aina hii.
 
Huyu alikuwa na autism, watu wa aina hii ndiyo huwa wana uwezo wa kufanya kitu fulani kiajabu sana. Kama ni muziki basi utashangaa akisikia muziki fulani mara moja tu anauelewa wote, na kama ni mahesabu basi atafanya macalculation ya ajabu ambayo binaadamu wa kawaida hawezi.

Kuna filam moja ya kihindi 'My name is Khan' na yeye ana autism basi alionyesha kipaji cha aina hii.
Kwani autism si anakuwa na kasoro Fulani katika ubongo wake inakuwaje anakuwa na uwezo mkubwa namna hio?
 
Back
Top Bottom