Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 8,848
- 15,252
Poleni na Majukumu,
Serikali yetu kwa sasa inapitia katika kipindi kigumu cha tatizo la ajira rasmi kwa vijana na watu wazima pia. Pamoja na Yote Serikali imekuwa ikisisitiza vijana wajiajiri bila kuwawezesha ni kwa namna gani vijana waweze kujiajiri.
Jijini Arusha mzungu mmoja aitwae Michael fortson yeye na mke wake wameanzisha kituo kiitwacho Neema Village ambapo mbali na kusaidia watoto yatima, wameamua kuwawezesha Wanawake Wajane, Waliotelekezwa(single mothers) na wale wasiokuwa na ajira au shughuli yoyote kwa kuwa patia yafuatayo :
MITAJI YA BIASHARA
mzungu huyo kwa kupitia taasisi aliyoianzisha yeye na mkewe bi Doris fortson huwapatia wanawake tajwa hapo juu mitaji ya biashara mbalimbali kulingana na uhitaji na uzoefu wao. Mfano mitaji ya mifugo ya kufuga kama vile kuku , biashara za sokoni nk.
MALIPO YA KILA MWEZI
Michael fortson hutoa kiasi cha pesa kila mwezi Kwa ajili ya Kujikimu wao na watoto wao kwa Wanawake wote tajwa hapo juu.
KODI YA NYUMBA NA VYOMBO VYA. NDANI
Wakina Mama wote ambao hawako kwenye nyumba zao huwezeshwa kwa kulipiwa kodi ya Miezi sita pamoja naKununuliwa vyombo vya ndani kama vile majiko ya gesi, majaba ya kuhifadhia maji, vitanda Magodoro na mashuka yake nk.
ELIMU /UFUNDI
Kuna wale wanawake wenye kupenda kujifunza kazi za ushonaji, ubunifu, ufugaji nk. Hupewa mafuzo yote hapo Neema Village bure na baada ya mafuzo hupewa vyeti pamoja na Kuwezeshwa kufanya kile walichokisomea au kujifunzia hapo kwenye kituo .
WAZAZI
Kuna wale wanawake waliotelekezwa na watoto wachanga Hospitalini na. Majumbani baada ya kujifungua ambao bado ni wazazi. Basi wanawake hao hupewa huduma zote muhimu katika kipindi chote cha uzazi ikiwa ni pamoja na chakula, maziwa ya unga ya watoto, pampers,lishe pamoja na nguo za watoto na gharama za kumpeleka mtoto kiliki.
Pamoja na mambo mengine mengi ambayo Neema Village imekuwa ikisaidia kwa wakinama wote wenye uhitaji mkoani Arusha pia imetoa huduma ya kuchimba visima vya maji na kuweka masimtank kwenye viunga bure kwa wananchi wote wanao zunguka eneo hilo.
Lengo la Neema Village ni kupanua wigo zaidi na Kufikia walengwa tofauti tofauti.
Je serikali yetu imeshindwa kuwawezesha vijana wetu kwa namna yoyote ile? mfano wa large scale agriculture, kilimo chenye tija.
Kuwataftia masoko ya bidhaa zetu nje ya nchi,mosoko nje ya nchi yangesaidia sana katika uchumi wetu maana yanaleta /yanaingiza pesa ndani ya nchi na hivyo kuongezeka Kwa mapato
Kufungua Ranch kila wilaya ambapo vijana wengi wangeajiriwa huko
Kuomba misaada mbali mbali katika mataifa ya magharibi ikiwemo ajira za vijana na Masomo katika nchi hizo kuliko kila siku kukopa fedha ambazo hatujui zinaenda wapi.
Serikali yetu kwa sasa inapitia katika kipindi kigumu cha tatizo la ajira rasmi kwa vijana na watu wazima pia. Pamoja na Yote Serikali imekuwa ikisisitiza vijana wajiajiri bila kuwawezesha ni kwa namna gani vijana waweze kujiajiri.
Jijini Arusha mzungu mmoja aitwae Michael fortson yeye na mke wake wameanzisha kituo kiitwacho Neema Village ambapo mbali na kusaidia watoto yatima, wameamua kuwawezesha Wanawake Wajane, Waliotelekezwa(single mothers) na wale wasiokuwa na ajira au shughuli yoyote kwa kuwa patia yafuatayo :
MITAJI YA BIASHARA
mzungu huyo kwa kupitia taasisi aliyoianzisha yeye na mkewe bi Doris fortson huwapatia wanawake tajwa hapo juu mitaji ya biashara mbalimbali kulingana na uhitaji na uzoefu wao. Mfano mitaji ya mifugo ya kufuga kama vile kuku , biashara za sokoni nk.
MALIPO YA KILA MWEZI
Michael fortson hutoa kiasi cha pesa kila mwezi Kwa ajili ya Kujikimu wao na watoto wao kwa Wanawake wote tajwa hapo juu.
KODI YA NYUMBA NA VYOMBO VYA. NDANI
Wakina Mama wote ambao hawako kwenye nyumba zao huwezeshwa kwa kulipiwa kodi ya Miezi sita pamoja naKununuliwa vyombo vya ndani kama vile majiko ya gesi, majaba ya kuhifadhia maji, vitanda Magodoro na mashuka yake nk.
ELIMU /UFUNDI
Kuna wale wanawake wenye kupenda kujifunza kazi za ushonaji, ubunifu, ufugaji nk. Hupewa mafuzo yote hapo Neema Village bure na baada ya mafuzo hupewa vyeti pamoja na Kuwezeshwa kufanya kile walichokisomea au kujifunzia hapo kwenye kituo .
WAZAZI
Kuna wale wanawake waliotelekezwa na watoto wachanga Hospitalini na. Majumbani baada ya kujifungua ambao bado ni wazazi. Basi wanawake hao hupewa huduma zote muhimu katika kipindi chote cha uzazi ikiwa ni pamoja na chakula, maziwa ya unga ya watoto, pampers,lishe pamoja na nguo za watoto na gharama za kumpeleka mtoto kiliki.
Pamoja na mambo mengine mengi ambayo Neema Village imekuwa ikisaidia kwa wakinama wote wenye uhitaji mkoani Arusha pia imetoa huduma ya kuchimba visima vya maji na kuweka masimtank kwenye viunga bure kwa wananchi wote wanao zunguka eneo hilo.
Lengo la Neema Village ni kupanua wigo zaidi na Kufikia walengwa tofauti tofauti.
Je serikali yetu imeshindwa kuwawezesha vijana wetu kwa namna yoyote ile? mfano wa large scale agriculture, kilimo chenye tija.
Kuwataftia masoko ya bidhaa zetu nje ya nchi,mosoko nje ya nchi yangesaidia sana katika uchumi wetu maana yanaleta /yanaingiza pesa ndani ya nchi na hivyo kuongezeka Kwa mapato
Kufungua Ranch kila wilaya ambapo vijana wengi wangeajiriwa huko
Kuomba misaada mbali mbali katika mataifa ya magharibi ikiwemo ajira za vijana na Masomo katika nchi hizo kuliko kila siku kukopa fedha ambazo hatujui zinaenda wapi.