NECTA na matokeo: Kwanini mnaonesha majina?

JAYJAY

JF-Expert Member
Oct 31, 2008
7,291
7,238
mara nyingi nimekuwa nikijiuliza kwa nini baraza la mitihani la Taifa linaonesha majina ya watahiniwa wakati wa kutoa matokeo. mimi kwa mtazamo wangu naona matokeo ya mtahiniwa ni siri kati yake na baraza (au mwalimu na mwanafunzi) au pia mtu/watu ambao mtahiniwa ameridhia au anawajibika kwake/kwao. kwenye vyuo, zamani kabla ya kuenea kwa huduma za mawasiliano ya internet walikuwa wanaweka matokeo ya wanafunzi kwa karatasi zenye kuonesha namba tu za watahiniwa na matokeo yao, ambapo kwa sasa mwanafuzi anakuwa na account yake kwa internet ambapo huweza kuangalia matokeo yake popote pale alipo kwenye huduma hiyo. baraza la mitihani linaweka matokeo kwenye website yake ambayo yana majina ya watahiniwa, nadhani wangebadilisha utaratibu na kuweka namba tu ya mtahiniwa na matokeo yake, na hiki kitu walikifanya kama miaka 3 iliyopita (sina uhakika), sasa sijui kwa nini wamerudia tena huu mfumo wa kuanika majina ya watahiniwa, anayefahamu anaweza kunielewesha. hii inachochea watu kufatilia hata matokeo ya watu yasiyowahusu kwenye mitandao kisa tu wanaishi mtaa mmoja au sababu nyingine za kijinga, na pia inasababisha mateso ya kisaikolojia na aibu kwa familia hasa kwa wale wanafunzi wenye matokeo mabaya. wangesambaza vitabu vyenye majina na matokeo huko mashuleni kisha kwenye website waweke namba na matokeo tu, mwanafunzi mwenye wasiwasi na matokeo yake anaweza kuwasiliana na shule yake kwa uthibitisho.
 
utaratibu wa sasa ni sawa kwani umeturahisishia sisi wazazi na walezi kufuatilia matokeo ya watoto wetu kwa urahisi. Awali tulikuwa tunadaganywa kwa kupewa namba za uongo na hivyo kutojua matokeo. Njia nzuri ya kuondokana na aibu ni kujitahidi katika masomo.
Utaratibu huu wa sasa ni mzuri na uendelee.
 
Kuna watu hapa nilipo wanafanya mtihan wa taifa,,,,,lakin ukimuuliza wewe INDEX NO:YAKO NGAPI HAKUMBUKI,,,,JE WAKIWEKA NAMBA KWENYE MATOKEO,,,,UNADHAN ITAKUWAJE????na wapo ambao wanajikuta wanaandika namba si zao,,,so mfumo wa majina uko palepale,hata wakitoa kwa namba still utaona tu
 
mara nyingi nimekuwa nikijiuliza kwa nini baraza la mitihani la Taifa linaonesha majina ya watahiniwa wakati wa kutoa matokeo. mimi kwa mtazamo wangu naona matokeo ya mtahiniwa ni siri kati yake na baraza (au mwalimu na mwanafunzi) au pia mtu/watu ambao mtahiniwa ameridhia au anawajibika kwake/kwao. kwenye vyuo, zamani kabla ya kuenea kwa huduma za mawasiliano ya internet walikuwa wanaweka matokeo ya wanafunzi kwa karatasi zenye kuonesha namba tu za watahiniwa na matokeo yao, ambapo kwa sasa mwanafuzi anakuwa na account yake kwa internet ambapo huweza kuangalia matokeo yake popote pale alipo kwenye huduma hiyo. baraza la mitihani linaweka matokeo kwenye website yake ambayo yana majina ya watahiniwa, nadhani wangebadilisha utaratibu na kuweka namba tu ya mtahiniwa na matokeo yake, na hiki kitu walikifanya kama miaka 3 iliyopita (sina uhakika), sasa sijui kwa nini warerudia tena huu mfumo wa kuanika majina ya watahiniwa, anayefahamu anaweza kunielewesha. hii inachochea watu kufatilia hata matokeo ya watu yasiyowahusu kwenye mitandao kisa tu wanaishi mtaa mmoja au sababu nyingine za kijinga, na pia inasababisha mateso ya kisaikolojia na aibu kwa familia hasa kwa wale wanafunzi wenye matokeo mabaya. wangesambaza vitabu vyenye majina na matokeo huko mashuleni kisha kwenye website waweke namba na matokeo tu, mwanafunzi mwenye wasiwasi na matokeo yake anaweza kuwasiliana na shule yake kwa uthibitisho.


Umesema jambo la msingi sana. Matokeo ni siri ya mtu, ni sawa na ugonjwa wa mtu huwa ni siri kubwa. Baraza la mitihani liangalie na mlifanyie kazi. One's exam results is not for public consumption at all. Mimi nitakwenda mahakamani kuomba baraza la mitihani lipewe order ya kutotoa majina ya watu kwenye internet. Namba zinatosha kwa mhusika kujua matokeo basi.
 
kwani wazazi wa wanafunzi zamani walikuwa wanafuatilia vipi? mzazi asiyefuatilia maendeleo ya mtoto wake ndiye anayeweza kudanganywa tuu!
utaratibu wa sasa ni sawa kwani umeturahisishia sisi wazazi na walezi kufuatilia matokeo ya watoto wetu kwa urahisi. Awali tulikuwa tunadaganywa kwa kupewa namba za uongo na hivyo kutojua matokeo. Njia nzuri ya kuondokana na aibu ni kujitahidi katika masomo.
Utaratibu huu wa sasa ni mzuri na uendelee.
 
ndio maana nikatoa ushauri kuwa vitabu vyenye majina na matokeo vipelekwe mashuleni huku kwenye mtandao ibaki namba tu! huyo anayesahau namba atapaswa kwenda au kuwasiliana na shule yake!
Kuna watu hapa nilipo wanafanya mtihan wa taifa,,,,,lakin ukimuuliza wewe INDEX NO:YAKO NGAPI HAKUMBUKI,,,,JE WAKIWEKA NAMBA KWENYE MATOKEO,,,,UNADHAN ITAKUWAJE????na wapo ambao wanajikuta wanaandika namba si zao,,,so mfumo wa majina uko palepale,hata wakitoa kwa namba still utaona tu
 
Biafsi sioni tatizo lolote kuweka wazi majina. Mbona kuna wazazi wengine hufanya party kwa ajili ya kuwapongeza wanao wanapokuwa wamefanya vizuri, mkialikwa mbona tunakwenda, hatusemi ni siri yake? Hii ni self defense kwa wanafunzi wavivu darasani.Sina hakina ni miaka ni miaka mitatu gani unayosema,lakini nachoelewa ni kwamba tangu kuanzia mwishoni mwa miaka ya 90 majina yalikuwa yakichapishwa kwnye magazeti bila malalamiko yoyote. Tunasahau magazeti yanavyonunuliwa baada ya matokeo kutoka. OK, fine kama unaona matokeo ni udhalilishaji basi,huna haja ya kununua magazeti yale wala kuingia kwenye website ya NECTA.Mimi naona ni msaada kwa wanafunzi zaidi ya hivyo tunavyofikiria. Unamfikiriaje mtoto wa masikini aliyemaliza shule Newala halafu akarudi kwao Biharamulo,kipi rahisi kati ya kununua gazeti au kwenda internet cafe kwa Tsh 500 au kusafiri kuendea matokeo yake Mtwara kisha kurudi tena Kagera kujiandaa kwa hatua nyingine inayofuata??? Jiongeze!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
utaratibu wa sasa ni sawa kwani umeturahisishia sisi wazazi na walezi kufuatilia matokeo ya watoto wetu kwa urahisi. Awali tulikuwa tunadaganywa kwa kupewa namba za uongo na hivyo kutojua matokeo. Njia nzuri ya kuondokana na aibu ni kujitahidi katika masomo.
Utaratibu huu wa sasa ni mzuri na uendelee.

Umenena mwn,kw hao wanaotaka namba pekee wafanye bdii km hawatak aibu pia watoto wa cku hz wanapenda starehe kulko kusoma so matokeo na majina ndo mpango mzima cz unaleta maendeleo makubwa sn ktk elimu.
 
Hivi hebu fikiria matokeo yako umejenga vibanda (kibanda= A) 7 au 9 na jina lako linatokea wenzako wote wanaona, utajisikia vipi? Kuandika Jina ni motisha pia kuwafanya msome kwa bidii, huku wavivu wakiadhibiwa kwa kupokea funguo hadharani.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom