NEC yaweka masharti matumizi ya simu vituoni Oktoba 28

Hata Malawi simu janja iliwaponza sana ndio maana uchaguzi ukarudiwa.Vyama vya upinzani nawashauri wanunue vyombo vya kurekodi na kupiga picha kama kalamu, saa, miwani nk vitawasaidia mbeleni.

Vinapatikana wapi vitu hivyo na kwa bei gani?
 
Simu janja inaogopwa kama bom !! CCM mtakuja kuwambia ata Mawakala muda wa kuhesabu wafunge macho!
Huu uoga umepitiluza aisee yaani ni ili uchakachuaji usijulikane, hili lilitakiwa lipingwe kwa nguvu zote.
 
Saba: Matokeo yaliyosainiwa kubandikwa nje ya kituo Cha kupiga kura kabla ya kutangazwa kwa mashindi.
Nane: Kura kuhesabiwa hadharani .
Mkuu hiyo kuhesabiwa hadharani ndiyo kabisa hawataki kuisikia. Zile mbwembwe za uwazi kwenye uteuzi wa wagombea kwenye vyama vyao kuwa live huku hawataki kabisa!!!
 
Tume nao wahakikishe wasimamizi wao wa uchaguzi hawafanyi jambo lolote litakalo sababisha kuzua taharuki kwa umma, kazi ya kuhesabu kura na kutangaza matokeo ifanyike kwa weledi, uaminifu, na wepesi wa hali ya juu ili kuepuka vurugu zozote.


Wasimamizi wa uchaguzi nao wafuate Kanuni za uchaguzi.

Mambo yaliyotokea Kinondoni kwenye uchaguzi wa marudio yasijirudie.

RIP AA.
 
Hiyo kuzuia simu lengo lake ni kuhakikisha hujuma zote zitakazofanyika kituoni hazifahamiki. Nawashauri watu wawe na silaha za jadi za kutosha kuzunguka vituo vya kura. Wakala wa upinzani akiona hujuma wakati wa upigaji, uhesabuji na kutangaza matokeo apige kelele ya mwizi mwizi. Hapo wananchi wenye hasira kali wavamie na kutoa kipigo kikali.
 
Hawa WAHUNI wa CCM Mpya ni suala la muda tu, hakuna Mwananchi anayejitambua anayependa kuendelea tena na hii Serikali ya WATEKA NYARA, Kubambikia kesi zisizo na dhamana Watu, Kulipisha Kodi mara mbili zaidi ya gharama halisi za manunuzi, Kukandamiza demokrasia na kuminya uhuru wa habari n.k
 

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) nchini Tanzania imeweka masharti ya matumizi ya simu katika vituo vya kuhesabu, kupigia na kujumulishia kura katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mambo hayo yasiyotakiwa ni;

Mosi; mtu yeyote kutumia simu ya kiganjani ndani ya kituo cha kupigia, kuhesabia au kujumlishia kura isipokuwa msimamizi wa kituo, wasaidizi wake na mlinzi wa kituo cha kupigia kura ambao watatumia simu zao pale itakapobidi kwa shughuli za uchaguzi tu na simu hizo wakati wote ziwe zimeondolewa mlio na ziwe kwenye mtetemo.

Pili; viongozi wa vyama vya siasa, wagombea au wafuasi wao kufanya vitendo vinavyoweza kusababisha fujo, vurugu katika vituo vya kupigia, kuhesabu na kujumlishia kura.

Tatu; vyama vya siasa, wagombea na wafuasi wao katika siku ya kupiga kura kufanya kampeni ya aina yoyote ikiwa ni pamoja na kuvaa vazi lolote au kuwa na kitu chochote kinachoashiria kushawishi watu kumpigia kura mgombea Fulani.

Hii ni pamoja na matumizi ya vyombo vya usafiri vilivyokuwa vinatumika wakati wa kampeni vinavyoashiria utambuzi wa chama Fulani.

Nne, kiongozi, mgombea au mtendaji yeyote wa chama cha siasa kutoa lugha ya matusi kwa mtendaji wa uchaguzi.

Endapo kuna changamoto au lalamiko lolote kuhusiana na mchakato au taratibu za uchaguzi katika kituo cha kupigia kura, changamoto hizo zitawasilishwa kwa maandishi kwa msimamizi wa kituo kupitia kwa wakala.

Tano; kiongozi au mtendaji wa chama cha siasa, mwanachama au mfuasi kuvamia au kukaa kwa nguvu ndani ya kituo cha kupigia, kuhesabia au kujumlishia kura.

Sita; kiongozi, mgombea au mtendaji wa chama cha siasa, mwanachama au mfuasi kujihusisha na vitendo vifuatuvyo:

I. Kuwahamasisha wanachama au wafuasi kupiga kura zaidi ya mara moja katika uchaguzi mmoja
II. Kununua kadi ya mpiga kura, kununua kura au kutoa hongo, zawadi, shukrani au aina yoyote ya malipo ya fedha au vifaa kwa mpiga kura au mtendaji wa uchaguzi.
Uoga wote wa Nini wakati mna madaraja, mandege, maflyover
 
Siku zote watu waovu hupenda kufanya mambo yao kifichoni, ili kuweza kukamilisha uovu wao. Uwazi na ukweli wowote ule ambao unaweza kifuchua njia zao uovu huwekea vizingiti vingi, na hata kuutafutia kila aina ya hila ili uonekane kuwa wenyewe ndiyo ni tishio.

Hivi ndivyo vikaragosi vilivyofichwa ktk sura ya NEC ndiyo vinavyofanya. Wengi wao ni makada wasiokuwa na maadili ambao wamewekwa kimkakati kuzuia machaguo sahihi ya wapigakura.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom