NEC yaweka masharti matumizi ya simu vituoni Oktoba 28

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
1600257234605.png

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) nchini Tanzania imeweka masharti ya matumizi ya simu katika vituo vya kuhesabu, kupigia na kujumulishia kura katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Masharti hayo ni miongoni mwa Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2020 yaliyotolewa na NEC ikielezea mambo sita yasiyotakiwa kufanywa na vyama vya siasa wakati wa upigaji kura mpaka kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi huo.
Mambo hayo yasiyotakiwa ni;

Mosi; mtu yeyote kutumia simu ya kiganjani ndani ya kituo cha kupigia, kuhesabia au kujumlishia kura isipokuwa msimamizi wa kituo, wasaidizi wake na mlinzi wa kituo cha kupigia kura ambao watatumia simu zao pale itakapobidi kwa shughuli za uchaguzi tu na simu hizo wakati wote ziwe zimeondolewa mlio na ziwe kwenye mtetemo.

Pili; viongozi wa vyama vya siasa, wagombea au wafuasi wao kufanya vitendo vinavyoweza kusababisha fujo, vurugu katika vituo vya kupigia, kuhesabu na kujumlishia kura.

Tatu; vyama vya siasa, wagombea na wafuasi wao katika siku ya kupiga kura kufanya kampeni ya aina yoyote ikiwa ni pamoja na kuvaa vazi lolote au kuwa na kitu chochote kinachoashiria kushawishi watu kumpigia kura mgombea Fulani.

Hii ni pamoja na matumizi ya vyombo vya usafiri vilivyokuwa vinatumika wakati wa kampeni vinavyoashiria utambuzi wa chama Fulani.

Nne, kiongozi, mgombea au mtendaji yeyote wa chama cha siasa kutoa lugha ya matusi kwa mtendaji wa uchaguzi.

Endapo kuna changamoto au lalamiko lolote kuhusiana na mchakato au taratibu za uchaguzi katika kituo cha kupigia kura, changamoto hizo zitawasilishwa kwa maandishi kwa msimamizi wa kituo kupitia kwa wakala.

Tano; kiongozi au mtendaji wa chama cha siasa, mwanachama au mfuasi kuvamia au kukaa kwa nguvu ndani ya kituo cha kupigia, kuhesabia au kujumlishia kura.

Sita; kiongozi, mgombea au mtendaji wa chama cha siasa, mwanachama au mfuasi kujihusisha na vitendo vifuatuvyo:

I. Kuwahamasisha wanachama au wafuasi kupiga kura zaidi ya mara moja katika uchaguzi mmoja
II. Kununua kadi ya mpiga kura, kununua kura au kutoa hongo, zawadi, shukrani au aina yoyote ya malipo ya fedha au vifaa kwa mpiga kura au mtendaji wa uchaguzi.
 
Tume nao wahakikishe wasimamizi wao wa uchaguzi hawafanyi jambo lolote litakalo sababisha kuzua taharuki kwa umma, kazi ya kuhesabu kura na kutangaza matokeo ifanyike kwa weledi, uaminifu, na wepesi wa hali ya juu ili kuepuka vurugu zozote.
 
Siku hizi kuna jammer za kuweka hata mfukoni,simu zote zinazima kwa mita kadhaa,,wakitaka niwauzie,nnazo container mbili hapa hong kong..
 

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) nchini Tanzania imeweka masharti ya matumizi ya simu katika vituo vya kuhesabu, kupigia na kujumulishia kura katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mambo hayo yasiyotakiwa ni;

Mosi; mtu yeyote kutumia simu ya kiganjani ndani ya kituo cha kupigia, kuhesabia au kujumlishia kura isipokuwa msimamizi wa kituo, wasaidizi wake na mlinzi wa kituo cha kupigia kura ambao watatumia simu zao pale itakapobidi kwa shughuli za uchaguzi tu na simu hizo wakati wote ziwe zimeondolewa mlio na ziwe kwenye mtetemo.

Pili; viongozi wa vyama vya siasa, wagombea au wafuasi wao kufanya vitendo vinavyoweza kusababisha fujo, vurugu katika vituo vya kupigia, kuhesabu na kujumlishia kura.

Tatu; vyama vya siasa, wagombea na wafuasi wao katika siku ya kupiga kura kufanya kampeni ya aina yoyote ikiwa ni pamoja na kuvaa vazi lolote au kuwa na kitu chochote kinachoashiria kushawishi watu kumpigia kura mgombea Fulani.

Hii ni pamoja na matumizi ya vyombo vya usafiri vilivyokuwa vinatumika wakati wa kampeni vinavyoashiria utambuzi wa chama Fulani.

Nne, kiongozi, mgombea au mtendaji yeyote wa chama cha siasa kutoa lugha ya matusi kwa mtendaji wa uchaguzi.

Endapo kuna changamoto au lalamiko lolote kuhusiana na mchakato au taratibu za uchaguzi katika kituo cha kupigia kura, changamoto hizo zitawasilishwa kwa maandishi kwa msimamizi wa kituo kupitia kwa wakala.

Tano; kiongozi au mtendaji wa chama cha siasa, mwanachama au mfuasi kuvamia au kukaa kwa nguvu ndani ya kituo cha kupigia, kuhesabia au kujumlishia kura.

Sita; kiongozi, mgombea au mtendaji wa chama cha siasa, mwanachama au mfuasi kujihusisha na vitendo vifuatuvyo:

I. Kuwahamasisha wanachama au wafuasi kupiga kura zaidi ya mara moja katika uchaguzi mmoja
II. Kununua kadi ya mpiga kura, kununua kura au kutoa hongo, zawadi, shukrani au aina yoyote ya malipo ya fedha au vifaa kwa mpiga kura au mtendaji wa uchaguzi.
Mungu ni huyu wa nec na tz kwa ujumla, sim zina shida gani kwa mfano, cheo ni kizuri ila kwa mwaka huu Kuna vyeo ,nec mna wakati mgum ngoja tuombee
 
Back
Top Bottom