ACT Wazalendo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 608
- 1,540
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza nafasi ya kazi kwa Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi kwa Jimbo la Konde.
Utaratibu huu ni tofauti na utaratibu wa awali ambapo Wasimamizi wa Uchaguzi wa Majimbo kwa Zanzibar walikuwa wakiteuliwa moja kwa moja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi na wengi wao wakiwa Makada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) au wafanyakazi katika vyombo vya ulinzi na usalama.
Kwa kuzingatia kuwa Chama chetu kiliiandikia Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuhakikisha kuwa waliohujumu Uchaguzi wa marudio wa Jimbo la Konde hawarejeshwi kusimamia uchaguzi ujao, tunaunga mkono hatua hii.
Hata hivyo, hatua hii itakuwa na maana iwapo NEC itahakikisha kuwa wanaoteuliwa siyo Makada wa CCM, Watumishi wa Vyombo vya ulinzi na usalama au watumishi ambao rekodi zao za upendeleo wa kisiasa zinafahamika. Chama chetu kinafuatilia kwa karibu mchakato huo kuhakikisha haki inatendeka.
Hatua hii ilipaswa pia kuwagusa Wasimamizi wa Vituo vya Kupigia Kura ambao ndio wamekuwa ni waharibifu wakubwa wa uchaguzi.
Pia, Chama chetu kinatoa rai kwa NEC kutangaza nafasi kwa Msimamizi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Ushetu na kuachana na Wakurugenzi wa Halmashauri ambao wengi wao ni Makada wa Chama Cha Mapinduzi.
Katika kuhitimisha, tunaendeleza wito wetu kuwa Katiba na Sheria za Uchaguzi ziandikwe upya ili Tume ya Taifa ya Uchaguzi ifanye shughuli zake kwa uhuru. Tunatoa rai kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa mchakato huo uanze sasa.
Ni lazima Tume ya Taifa ya Uchaguzi iwe na watumishi wake wanaowajibika kwa Tume tena wasiwe makada wa Chama chochote cha siasa ili uchaguzi uwe huru, haki na wa kuaminika.
Imetolewa na
Salim A. Bimani,
Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma,
ACT Wazalendo.
01 Septemba, 2021.
Utaratibu huu ni tofauti na utaratibu wa awali ambapo Wasimamizi wa Uchaguzi wa Majimbo kwa Zanzibar walikuwa wakiteuliwa moja kwa moja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi na wengi wao wakiwa Makada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) au wafanyakazi katika vyombo vya ulinzi na usalama.
Kwa kuzingatia kuwa Chama chetu kiliiandikia Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuhakikisha kuwa waliohujumu Uchaguzi wa marudio wa Jimbo la Konde hawarejeshwi kusimamia uchaguzi ujao, tunaunga mkono hatua hii.
Hata hivyo, hatua hii itakuwa na maana iwapo NEC itahakikisha kuwa wanaoteuliwa siyo Makada wa CCM, Watumishi wa Vyombo vya ulinzi na usalama au watumishi ambao rekodi zao za upendeleo wa kisiasa zinafahamika. Chama chetu kinafuatilia kwa karibu mchakato huo kuhakikisha haki inatendeka.
Hatua hii ilipaswa pia kuwagusa Wasimamizi wa Vituo vya Kupigia Kura ambao ndio wamekuwa ni waharibifu wakubwa wa uchaguzi.
Pia, Chama chetu kinatoa rai kwa NEC kutangaza nafasi kwa Msimamizi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Ushetu na kuachana na Wakurugenzi wa Halmashauri ambao wengi wao ni Makada wa Chama Cha Mapinduzi.
Katika kuhitimisha, tunaendeleza wito wetu kuwa Katiba na Sheria za Uchaguzi ziandikwe upya ili Tume ya Taifa ya Uchaguzi ifanye shughuli zake kwa uhuru. Tunatoa rai kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa mchakato huo uanze sasa.
Ni lazima Tume ya Taifa ya Uchaguzi iwe na watumishi wake wanaowajibika kwa Tume tena wasiwe makada wa Chama chochote cha siasa ili uchaguzi uwe huru, haki na wa kuaminika.
Imetolewa na
Salim A. Bimani,
Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma,
ACT Wazalendo.
01 Septemba, 2021.