Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage, Agosti 21 akiwasilisha ripoti ya Uchaguzi Mkuu 2020 kwa Rais Samia alitoa mapendekezo saba ya kufanyiwa kazi, likiwemo la kuanzishwa kwa Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo itawapa meno zaidi.
Mapendekezo ya NEC ya kutaka ianzishwe sheria inayowatambua na kuwapa mamlaka zaidi imetoa tafsiri kuwa wanataka wajiendeshe kwa uhuru na ufanisi zaidi pasi hofu ya kuingiliwa na viongozi, yanaipa nguvu hoja ya wanaotaka tume huru ya uchaguzi.
Licha ya NEC na viongozi wa Serikali mara kwa mara kupinga kutoa au kupokea maelekezo ya uendeshaji wa uchaguzi, lakini ukweli unabaki kuwa kuna mkanganyiko wa kisheria na tume hiyo haiko huru.
Baadhi ya mapendekezo yanaonyesha wanalenga kuboresha utendaji, kuongeza kuaminika kwa wadau na kupata uhuru zaidi.
Kama pendekezo hili litapitishwa kutakuwa na mabadiliko makubwa katika uchaguzi mkuu utakaofanyika 2025, ingawa inaonekana gharama ndizo zitakuwa kikwazo cha utekelezwaji wake kama alivyodokeza Rais Samia.
Pendekezo jingine ni kuunganishwa sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura namba 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, sura ya 292 ili kurahisisha utekelezaji wa sheria hizo.
Vilevile, NEC inapendekeza uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu usimamiwe na mamlaka moja.
Kimsingi mapendekezo ya NEC yanaonyesha taasisi hiyo inavyofanya kazi katika mazingira magumu ambayo pia yanawafanya wasipate uungwaji mkono wa baadhi ya wadau pindi wanapotangaza matokeo ya kuendesha uchaguzi.
Chanzo: Mwananchi
Mapendekezo ya NEC ya kutaka ianzishwe sheria inayowatambua na kuwapa mamlaka zaidi imetoa tafsiri kuwa wanataka wajiendeshe kwa uhuru na ufanisi zaidi pasi hofu ya kuingiliwa na viongozi, yanaipa nguvu hoja ya wanaotaka tume huru ya uchaguzi.
Licha ya NEC na viongozi wa Serikali mara kwa mara kupinga kutoa au kupokea maelekezo ya uendeshaji wa uchaguzi, lakini ukweli unabaki kuwa kuna mkanganyiko wa kisheria na tume hiyo haiko huru.
Baadhi ya mapendekezo yanaonyesha wanalenga kuboresha utendaji, kuongeza kuaminika kwa wadau na kupata uhuru zaidi.
Kama pendekezo hili litapitishwa kutakuwa na mabadiliko makubwa katika uchaguzi mkuu utakaofanyika 2025, ingawa inaonekana gharama ndizo zitakuwa kikwazo cha utekelezwaji wake kama alivyodokeza Rais Samia.
Pendekezo jingine ni kuunganishwa sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura namba 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, sura ya 292 ili kurahisisha utekelezaji wa sheria hizo.
Vilevile, NEC inapendekeza uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu usimamiwe na mamlaka moja.
Kimsingi mapendekezo ya NEC yanaonyesha taasisi hiyo inavyofanya kazi katika mazingira magumu ambayo pia yanawafanya wasipate uungwaji mkono wa baadhi ya wadau pindi wanapotangaza matokeo ya kuendesha uchaguzi.
Chanzo: Mwananchi