Uchaguzi 2020 NEC yaonya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu watekeleze wajibu wao kwa mujibu wa mwongozo na Sheria iliyowateua

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imewataka watazamaji wa uchaguzi wa ndani na wa kimataifa, waliopewa idhini na tume hiyo kuangalia uchaguzi mkuu, watekeleze wajibu wao kwa mujibu wa mwongozo na sheria iliyowateua.

Tume hiyo imewaonya waangalizi hao, kuepuka kuingilia au kuvuruga mwenendo wa uchaguzi na kwamba watakaokiuka watachukuliwa hatua za kisheria.

Aidha, tume hiyo imesema kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi, imeteua maofisa 329,864 kutoka maeneo mbalimbali kuwa sehemu ya timu ya watu watakaoshiriki kusimamia uchaguzi mkuu Oktoba 28.

Akizungumza na waangalizi wa uchaguzi wa ndani na kutoka nje ya nchi, Dar es Salaam jana, Mjumbe wa NEC, Balozi Omar Mapuri alisema maandalizi ya uchaguzi huo yanaenda vizuri na vifaa vyote muhimu vingi vimeshafika majimboni na kwasasa vinasubiri kupelekwa kwenye vituo vya kupigia kura.

Alisema NEC imetoa idhini kwa taasisi za kimataifa 17 kuwa watazamaji wa uchaguzi mkuu. Alisema taasisi za ndani zilizoidhinishwa ni 97 na wakalimani wa lugha wako 28.

Aliwataka waangalizi hao kuzingatia sheria, Katiba ya nchi na miongozo inayowaongoza kufanya wajibu wao wa utazamaji katika uchaguzi huo na kuhakikisha hawaingilii mwenendo wa uchaguzi au kusababisha vurugu.

“Cha msingi hapa kwa watazamaji wa ndani na wa nje kuzingatia sheria, Katiba ya nchi na miongozo iliyowapa kibali cha kutekeleza wajibu wenu huo, msiingilie au kuvuruga mwenendo wa uchaguzi, watakaokiuka sheria itachukua mkondo wake,’’ alisema Balozi Mapuri.

Alisema awali waangalizi hao, walipeleka maombi NEC ya kuteuliwa na jumla ya maombi 14,575 yalikubaliwa na kupewa idhini.

Kila mmoja alipewa vitu vyote muhimu ikiwapo miongozo iliyoandaliwa kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza, taratibu, majukumu yao, mipaka yao na kutakiwa kuisoma na kuielewa.
 
Tanzania ni Nchi huru

Asije akatokea mtu akaanza kutufundisha sisi demokrasia
 
Ndugu usichojua Nchi inayoongoza kwa kukopa duniani ni marekani na ndio inadaiwa zaidi

Kukopa si ajabu, km unakopa kwa tija huo ni uzalendo

Tanzania imetoka mbali hakuna wa kuimbisha
Nchi huru unakopa bilion 115 kupambana na korona ambazo ni pesa za unaowaita mabeberu.

Uku ukidanganya watu unakusanya trion 1.3 kwa mwezi.

Kama hauna funza kichwani una Nini?
 
Hao waangalizi kama walikuwa hawajui watu wasiokubalika wanavyopora ushindi basi watajionea wenyewe safari hii ili wakaandae vikwazo kihaki.

Vituo vingine vya kupigia kura havitakuwa na mawakala wa vyama vya upinzani baada ya wakurugenzi kuamurishwa kutokuwaapisha kisha Magufuli na wapambe wake watakuja "kushangilia ushindi wa kishindo".
 
Ndugu usichojua Nchi inayoongoza kwa kukopa duniani ni marekani na ndio inadaiwa zaidi

Kukopa si ajabu, km unakopa kwa tija huo ni uzalendo

Tanzania imetoka mbali hakuna wa kuimbisha
Unakopa Sana ukiwa na wigo mpana wa kulipa .

Ila usikope halafu wanaokukopesha unawatukana na kuwaita Mabeberu
 
Tanzania ni Nchi huru

Asije akatokea mtu akaanza kutufunfindisha sisi demokrasia
Hakumlienda kufanya nn Sasa jaman na nyie ni watu huru
 

Attachments

  • images.jpeg.jpg
    images.jpeg.jpg
    41.4 KB · Views: 1
Hizi kauli za Tume zinaleta ukakasi!
Kongamano hili lilitakiwa kujwa la kuwakumbusha wajibu wao lakini si kuwaonya eti wasiingilie wala kuvuruga uchaguzi, hivi ni lini waangalizi waliwahi kuvuruga uchaguzi hapa Tanzania?
Ni lini waliwahi kuingilia uchaguzi hapa Tanzania??? Maana ya kuwa mwangalizi ni kuangalia namna misingi ya HAKI ilivyofuatwa!
Na kwa mujibu wa kiapo chao wao wanapaswa kuueleza ulimwengu ukweli wa kile walichokiona na kukishuhudia bila kupindisha wa kuficha! Sasa kuanza kuwarushia kauli za kuwaogofya ni kama kuwatia hofu wasitimize wajibu wao ipasavyo! Tanzania imeshauhakikishia ulimwengu mara kadhaa kuwa uchaguzi wa mwaka huu, utakuwa huru na wa haki, hivyo figisu kama hizi tena ni za nini?
Waacheni waangalizi wakatimize wajibu wao uliowaleta, kama ni wizi wa kura acheni wauseme!
 
Back
Top Bottom