Uchaguzi 2020 NEC wanavyoajiri Wasaidizi wa Uchaguzi wanatambuaje wanayemuajiri sio mshabiki wa chama cha siasa?

OLS

JF-Expert Member
Oct 12, 2019
419
669
Waungwana katika kupambana tunajua zikitokea fursa huwa tunazichangamkia kwa nguvu sana. Kila mwaka wa uchaguzi Tume ya Taifa ya Uchaguzi huwa inatoa nafasi za kazi za muda mfupi ili kusaidia shughuli za uchaguzi.

Ni wazi kuwa kwa miaka mingi kazi hizi zimekuwa zikiwa njia sahihi ya walimu kuomba na mara nyingi wamekuwa wakipata, lakini hiki sio kigezo pekee kwa kigezo cha msingi ni mtu kutokuwa na chama cha siasa.

Ni wazi kuwa hatuna mfumo wa moja kwa moja wa mtu kujulikana bila mashaka kwamba ana kadi au hana kadi ya chama fulani, kutokana na ufinyu wa matumizi ya teknolojia.

Swali langu linakuja kuwa ni kwa njia zipi NEC wanahakikisha kuwa wanayemchagua kusaidia shughuli za uchaguzi hana ushabiki na chama cha siasa.

Kwa kuwa kuandika barua kuwa mtu hana chama haimaanishi hana chama, lakini kama kungekuwa na mfumo centralized labda ingekuwa rahisi.

Nauliza hivi kwa sababu zisizo za kisiasa:
  • Inawezekana wasio na vyama wakaachwa kwa kuwa hakuna mfumo wa kumjua asiye na chama
  • Nafasi hizi zinaweza kuwa ni sehemu ya kuwapa posho waalimu tu huku wengi wasio na ajira wakikosa walau neema kwa kipindi hiki

Signed

OEDIPUS
 
Waungwana katika kupambana tunajua zikitokea fursa huwa tunazichangamkia kwa nguvu sana. Kila mwaka wa uchaguzi Tume ya Taifa ya Uchaguzi huwa inatoa nafasi za kazi za muda mfupi ili kusaidia shughuli za uchaguzi.

Ni wazi kuwa kwa miaka mingi kazi hizi zimekuwa zikiwa njia sahihi ya walimu kuomba na mara nyingi wamekuwa wakipata, lakini hiki sio kigezo pekee kwa kigezo cha msingi ni mtu kutokuwa na chama cha siasa.

Ni wazi kuwa hatuna mfumo wa moja kwa moja wa mtu kujulikana bila mashaka kwamba ana kadi au hana kadi ya chama fulani, kutokana na ufinyu wa matumizi ya teknolojia.

Swali langu linakuja kuwa ni kwa njia zipi NEC wanahakikisha kuwa wanayemchagua kusaidia shughuli za uchaguzi hana ushabiki na chama cha siasa.

Kwa kuwa kuandika barua kuwa mtu hana chama haimaanishi hana chama, lakini kama kungekuwa na mfumo centralized labda ingekuwa rahisi.

Nauliza hivi kwa sababu zisizo za kisiasa:
  • Inawezekana wasio na vyama wakaachwa kwa kuwa hakuna mfumo wa kumjua asiye na chama
  • Nafasi hizi zinaweza kuwa ni sehemu ya kuwapa posho waalimu tu huku wengi wasio na ajira wakikosa walau neema kwa kipindi hiki

Signed

OEDIPUS

Usiongopee watu ndugu, wanaoajiriwa katika kipindi hiki kusaidia shughuli za uchaguzi sio waalimu pekee ,wanaajiri mtu yeyote mwenye sifa zilizoainishwa kwenye tangazo la ajira husika.
pili,wale wanao ajiriwa kusaidia shughuli za uchaguzi huwa wanakula kiapo mbele ya hakimu bila ya kujali alikuwa chama gani
 
Back
Top Bottom