Elections 2010 NEC: Uchaguzi umeahirishwa majimbo yafuatayo...

Let be serious jamani, vifaa vyenyewe vifaa gani vya kukosekana vituoni na kupelekea kuhairisha/kuchelewesha matokeao ya uchaguzi huu muhimu kwa Nchi yetu TANZANIA..vifaa ninavyoviona kwenye vituo vya kupigia kura ni Plastic Containers za Mchina. Hivi vifaa sio vile highly advanced electronic voting machine ambazo tunaweza sema kama zimekosekana/hazipo basi ni tatizo.
 
Hii haikubariki, kiravu na makame wanapaswa kuwajibika kwa uzembe huu, na hii inaonyesha ni jinsi gani the so called president asivyokuwa makini hata katika kuteua watendaji wake. Kwa mfano huu mdogo tu peke yake, inatupa picha gani ya serikali yake if we vote for him?......to hell let them go
 
bi mkora hiyo inawezekana, nadhani wakiangalia jumla ya kura zilizopigwa na matokeo yake basi wanaweza kuchukulia Adv'ge ya kuvunja uchaguzi

Kabisa mimi nadhani ndio itakavyokuwa.... watachecki na wakiona mambo si mambo watataka kusubiri majimbo haya kwanza na ikiwezekana ku ahirisha kutoa matokeo na pengine uchaguzi kabisa.... I REALLY SMELL A ROTTEN FISH ON THIS!!!!!!
 
amaekuwa akisema kila mara kuwa vifaa vyote vipo,na vimeshafika kwa wakati,
kwa nini kuwe na mabadiliko ndani ya masaa?
hizi ni mbinu chafu tu
Mbwewe zote zile ooh matokeo ya uraisi ndani ya siku moja, mara ooh! ITC iatatumika vilivyo kuhakikisha speedy reporting zimeishia wapi???????? Yaani kumbe ni uchuro tu!
 
Mpanda Mjini, Mpanda Vijijini na Nkenge.
Pia uchaguzi wa madiwani katika kata takribani 20 hautafanyika kutokana na kupungua kwa vifaa

Siyo kwa Waziri Mkuu Mizengwe Pinda huko? Au kaona mambo yamemkalia vibaya anahitaji muda aingie chumba cha ndani kurekebisha?
 
Nachoshauri ni kuwa, Tanzania tunatakiwa tulenge mbali zaidi ktk kujua hatma ya haki ya Watz, kama lazima ipatikane nje ya mfumo wa sheria wa tanzania, inabidi haki itafutwe kwa njia hiyo.
 
Jana usiku NEC wametangaza kuahirisha uchaguzi katika majimbo matatu na kata nyingi tu mpaka tarehe nyingine itakayopangwa na kutangazwa hapo baadaye.

Sababu ya kuahirisha ni ukosefu wa vifaa.

My take:


Kwa nini NEC hawajifunzi kutoka NECTA kusambaza vifaa?


Naomba Watu wa sheria wafafanue hili, kama Uchaguzi katika majimbo hayo hayatafanyia je Matokeo ya Urais yatasubiri mpaka na Ndugu zetu wengine wapige Kura?

Ufafanuzi Tafadhali
 
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

YAH: KUAHIRISHA BAADHI YA CHAGUZI MBALIMBALI

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuwatangazia wananchi wote kuwa katika kikao chake cha tarehe 30/10/2010 imefanya maamuzi ya kuahirisha Uchaguzi katika baadhi ya Majimbo na Kata kutokana na upungufu uliojitokeza hususan katika karatasi za kura.

Kata na Majimbo ambayo Chaguzi zake zimeahirishwa ni kama ifuatavyo:-



1. Uchaguzi wa Wabunge katika majimbo ya Nkenge, Mpanda Mjini na Mpanda vijijini.Kwa upande wa anzibar (Unguja) Majimbo ya Mwanakwerekwe,Mtoni na Magogoni,na Wete (Pemba)
2. Uchaguzi wa Madiwani katika kata zifuatazo:-

Na.
HALMASHAURI
KATA
1
Newala DC
Mtonya
2
Mbulu DC
Endegikot
3
Manyoni DC
Kitaraka
4
Same DC
Kisiwani
5
Kibaha DC
Janga
6
Rufiji
(a) Kibiti
(b) Chemchem
(c) Ngorongo
(d) Kipugira
(e) Mjawa
7
Uyui DC
(a)KIgwa
(b)Ibelamilundi
8
Sikonge
Kisanga
9
Njombe
Mji Mwema

10
Ulanga DC
Msogezi
11
Karagwe DC
(a) Kimuli
(b) Kamuli
12
Kasulu
Kitagata
13
Chato DC
Buseresere
14
Mwanza (Jiji)
(a) Mkuyuni
(b) Mirongo

wa.

Vile vile, katika Kata ambazo Uchaguzi wa Madiwani umeahirishwa, Uchaguzi wa Rais na Wabunge utaendelea kufanyika kama ilivyopangwa.

Aidha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuwajulisha wananchi wote kuwa tarehe za kufanyika kwa chaguzi hizo itatangazwa hapo baadaye.


(Rajabu R. Kiravu)
Mkurugenzi Tume ya Taifa ya Uchaguzi
 
CCM wana hila wanataka kuarishwa ili wajizatiti kwa kuhonga

CCM ni WAHUNI. Nilijua tu watafanya mizengwe kama hii makusudi ili UCHAGUZI UAHIRISHWE KWENYE MAJIMBO AMBAYO WAPINZANI WANA NGUVU ili baada ya UCHAGUZI MKUU waweze kujipanga upya kuyakomboa hayo majimbo. Huo ndio mkakati ambao kwa mtu mwenye akili anaweza kubaini. Hapa BWANA HAKUNA CHA UCHAGUZI HURU NA HAKI. Ni ubabaishaji mtupu na wizi mtupu.
 
Rais atawezaje kuapishwa kama majimbo hayo hayatafanya uchaguzi wao?
Nafikiri hii ni mbinu ya kuahirisha uchaguzi nchi nzima au kumhalalisha JK kuendelea kushika uongozi.
Hayo majimbo nayo yana haki ya kumchagua kiongozi wa juu wa serikali.
 
Nawashauri wapinzani wakishindwa wapinge matokeo on ground kwamba kulikuwa na mizengwe...........tena ngazi ya kimataifa ah NEC MNABOA YAANI MNABOAAAA
 
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

YAH: KUAHIRISHA BAADHI YA CHAGUZI MBALIMBALI

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuwatangazia wananchi wote kuwa katika kikao chake cha tarehe 30/10/2010 imefanya maamuzi ya kuahirisha Uchaguzi katika baadhi ya Majimbo na Kata kutokana na upungufu uliojitokeza hususan katika karatasi za kura.

Kata na Majimbo ambayo Chaguzi zake zimeahirishwa ni kama ifuatavyo:-



1. Uchaguzi wa Wabunge katika majimbo ya Nkenge, Mpanda Mjini na Mpanda vijijini.Kwa upande wa anzibar (Unguja) Majimbo ya Mwanakwerekwe,Mtoni na Magogoni,na Wete (Pemba)
2. Uchaguzi wa Madiwani katika kata zifuatazo:-



Vile vile, katika Kata ambazo Uchaguzi wa Madiwani umeahirishwa, Uchaguzi wa Rais na Wabunge utaendelea kufanyika kama ilivyopangwa.

Aidha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuwajulisha wananchi wote kuwa tarehe za kufanyika kwa chaguzi hizo itatangazwa hapo baadaye.


(Rajabu R. Kiravu)
Mkurugenzi Tume ya Taifa ya Uchaguzi

Hapo kwa red naona amefafanua kuhusu kata tu, vipi kule ambako ni jimbo zima mbona hajatoa ufafanuzi kama nako uchaguzi wa rais utaendelea? Kama huko uchaguzi wa rais hautafanyika, ni wazi matokeo hayawezi kutangazwa hadi uchaguzi ukamilike majimbo yote. Kumbe walishamdokeza shehe Yahya mambo haya ili atuandae kuona uchaguzi ukiahirishwa?
Au no! Nakumbuka huyu shehe Yahya alitabiri kuwa uchaguzi leo hautakuwepo. Labda huu tulioshiriki leo ni uchaguzi wa kimsukule!
 
Naomba Watu wa sheria wafafanue hili, kama Uchaguzi katika majimbo hayo hayatafanyia je Matokeo ya Urais yatasubiri mpaka na Ndugu zetu wengine wapige Kura?

Ufafanuzi Tafadhali


Wewe vipi? Kura zilizoahirishwa ni kura wabunge au/na madiwani... sasa kura za Rais zinaathirika je?

Ufafanuzi: Uchaguzi wa Rais Unaendelea kama kawaida.

Na majimbo haya ya uchaguzi; Uchaguzi wao utarudiwa.
 
kuna hii paragraph nilikuwa sijaicopy inafafanua katika hayo majimbo matatu

*****************************************

Hata hivyo katika majimbo hayo matatu ambapo Uchaguzi wa Wabunge umeahirishwa, Uchaguzi wa Rais na Madiwani utanaendelea kufanyika leo kama ilivyopangwa.
**********************************************
 
Wewe vipi? Kura zilizoahirishwa ni kura wabunge au/na madiwani... sasa kura za Rais zinaathirika je?

Ufafanuzi: Uchaguzi wa Rais Unaendelea kama kawaida.

Na majimbo haya ya uchaguzi; Uchaguzi wao utarudiwa.


Uchakachuaji tu hakuna msamiati tofauti na huu
 
NEC imeshindwa kazi; wanaharibu uchaguzi. Nashauri wajiuzulu au Tume ivunjwe, wanaweza kutufanyia mambo ya Kivuitu.
 
Back
Top Bottom