Uchaguzi 2020 NEC lindeni heshima kidogo ya Tanzania iliyobaki. Kwa sasa zingatieni mambo makubwa mawili

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Mada inahusika.

Tukiwa katikati ya mchakato wa kuelekea uchaguzi Mkuu, Tanzania iko katika mstari mwembamba sana wa kutunza historia yake ya utulivu, amani na umoja kwenye ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Baada ya uchaguzi wa 2015, yaliyotokea hapo katikati hadi 2020 kwa upande wa umoja wetu, ustawi wa kisiasa , demokrasia na haki basi ukilanganisha na miaka ya nyuma tulitetereka sana.

Watawala hawawezi kukwepa lawama za kushambuliwa watu, kupotezwa watu na wasiojulikana, kumimnywa uhuru wa habari na kujieleza na kumimnywa haki hasa kwa upinzani. Zile chaguzi za marudio na za Mitaa haziwezi kusahaulika kwenye historia.

Pengine ni majaaliwa tu, lakini kutegemea amani katika mazingira yale ilikuwa ni " ku-risk" Tanzania na watanzania na kama kuna somo la kujifunza basi watawala na vyombo vyetu vya Dola ilibidi wajifunze na waseme basi imetosha.

Tumeona na huu mchakato wa kupata wagombea ulivyokwenda na hadi sasa kuna wabunge na Madiwani wa CCM eti wamepita bila kupingwa laKINI BILA KIFICHO WALIPATIKANA KWA HILA . UMINYAJI HAKI NA UONEVU ULIOKUBUHU.

NEC haikwepi lawama hadi sasa, Propaganda huwa hazidumu NA SIO "GUARANTEE" kusaidia Tanzania kuwa na AMANI YA KUDUMU KILA SIKU.

NEC imecheza mdundo wa CCM na watawala kwa kukubali kuhenyeshwa wakurugenzi na wasimamizi wa uchaguzi kuingia katika mtego. Likiharibika basi NEC hawawezi kukwepa lawama.

MAMBO MAWILI YA KUZINGATIWA KWA SASA
Tanzania inaninginia baina ya muda wa RUFAA ZA MAPINGAMIZI YA OVYO na baina ya UPIGAJI KURA NA KUTENDA HAKI HAPO TARAHE 28 Oktoba, 2020.

Huo ndio muda ambao Busara za NEC na ueledi utaivusha Tanzania yetu.

Tunajuwa namna NEC inavyopata masindikizo ya kutokubali hoja za rufaa huko, tunajuwa namna wanavyopata "pressure" ya wadau wa demokrasia na tunajuwa namna wanavyokosa msimamo wa pamoja kutokana na kuchanganywa taaluma za sheria na wanasiasa huko NEC wenyewe.

NEC haipaswi "ku-risk" amani ya Tanzania kwa kutaka kuwafurahisha watawala waovu wasioitakia mema Tanzania kwa kisingizio cha Madaraka yao.

Mtihani wa kwanza kwa sasa ni RUFAA ZA MAPINGAMIZI baada ya NEC kukubali kucheza mdundo wa CCM

Mtihani wa Pili ni haki na Uchaguzi siku ya tarehe 28 Oktoba ikiwa NEC itafanikiwa kuruka kiunzi cha kwanza cha rufaa kama nilivyoeleza

NEC inapaswa kujuwa ukubwa wa dhamana waliyopewa kwamba inavuka mipaka ya Tanzania yetu. Dunia inawatazama kwa karibu na kila tukio na hatua zinarikodiwa vyema.

Mazoea ya NEC kuwadekeza CCM hasa hii miaka mitano 2015 - 2020 ya CCM kufanya watakavyo kwa kuwatumia wakurugenzi makada na watiifu kwa CCM haiwezi ikawa kinga kwao. Mwenyekiti na Mkurungenzi wake Mkuu watabeba lawama zote.

USHAURI KWA NEC
Simamieni HAKI na SHERIA bila upendeleo na msiwe sehemu ya hila dhidi ya wengine.

Kwa mifano yenu ya kuwaenguwa UPINZANI tu kote BARA NA ZANZIBAR tayari mmeshafanya KOSA la awali na endelevu ambalo kujisafisha kwenu kutakuwa kugumu na kuanzia hapo mna wakati mgumu kujisafisha hilo eleweni.

NEC mnao muda wa kurekebisha mkitaka, hizo pressure za CCM zisiwatishe kumbukeni maisha baada ya uchaguzi.

Kumbukeni "timing" ya wapinzani si ya kubahatisha waliwasoma wakawaelewa watawala , NEC, vyombo vya haki, vyombo vya Dola na taasisi za kidini zinazotumika na KWA KWELI WALIWAELEWA VILIVYO. Mstirajie WAPINZANI watapotenza hii fursa nakuambieni.

MWISHO
Tunachukuwa hii fursa kutimiza wajibu wetu kama raia wa nchi hii kuwaomba NEC kusimamia haki na usawa walau kwa hii fursa ndogo ya kuitunza amani ya Tanzania iliyobaki.

Yaliyofanyika ndani ya miaka hii mitano hayapaswi kujirejea kwenye uchaguzi huu ambao ndio fursa ya mwisho kwa wapinzani, wanamageuzi , wapenda haki na wanademokrasia kote ZANZIBAR na BARA na dalili zote zinaonesha hatari iliyoko mbele.

Shime NEC tendeni haki na msimamie haki kwa dhati.


Kishada.
 
NEC ni tawi la mti kuna mzizi uliojichimbia chini zaidi huu ndyo wenye Shida. Huu mzizi umejaa miba na hii ndyo inaipa kibri NEC...uchaguzi wa serikali za MiTAA uliumiza mioyo ya wapenda haki nchini na duniani, safari hii NEC isikubali maji na chakula inachopewa na mzizi wenye miba mana kuna dalili mzizi unaweza kukatika miba yake!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
NEC wanafanya kazi kwa mashinikizo makubwa!! Tuwaonee huruma. Hata hayo mapingamizi yanayaangalia tu hawana mamlaka wanasubiri maelekezo.
Huu ni wakati wa kujiamini zaidi kwa wale waliopewa dhamana. Kama kuna wakati somo la sheria na confidence za ujaji zinatakiwa kutumika kwa maslahi ya Taifa ni sasa.

Umma unashuhudia. Mazoea hayapaswi kufanywa sheria. NEC itabeba na kuvuna ilichopanda.
 
NEC ni tawi la mti kuna mzizi uliojichimbia chini zaidi huu ndyo wenye Shida. Huu mzizi umejaa miba na hii ndyo inaipa kibri NEC...uchaguzi wa serikali za MiTAA uliumiza mioyo ya wapenda haki nchini na duniani..safari hii NEC isikubali maji na chakula inachopewa na mzizi wenye miba mana kuna dalili mzizi unaweza kukatika miba yake!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Siku mbili zitaamua ama ubwege wa Watanzania na Upinzani kwa ujumla au ubabe wa CCM na NEC.

Siku hizo ni SIKU YA KUTOA MAJIBU YA RUFAA ZA WAGOMBEA na SIKU YA UCHAGUZI .

Yetu macho.
 
Mada inahusika.

Tukiwa katikati ya mchakato wa kuelekea uchaguzi Mkuu, Tanzania iko katika mstari mwembamba sana wa kutunza historia yake ya utulivu, amani na umoja kwenye ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Baada ya uchaguzi wa 2015, yaliyotokea hapo katikati hadi 2020 kwa upande wa umoja wetu, ustawi wa kisiasa , demokrasia na haki basi ukilanganisha na miaka ya nyuma tulitetereka sana.

Watawala hawawezi kukwepa lawama za kushambuliwa watu, kupotezwa watu na wasiojulikana, kumimnywa uhuru wa habari na kujieleza na kumimnywa haki hasa kwa upinzani. Zile chaguzi za marudio na za Mitaa haziwezi kusahaulika kwenye historia.

Pengine ni majaaliwa tu, lakini kutegemea amani katika mazingira yale ilikuwa ni " ku-risk" Tanzania na watanzania na kama kuna somo la kujifunza basi watawala na vyombo vyetu vya Dola ilibidi wajifunze na waseme basi imetosha.

Tumeona na huu mchakato wa kupata wagombea ulivyokwenda na hadi sasa kuna wabunge na Madiwani wa CCM eti wamepita bila kupingwa laKINI BILA KIFICHO WALIPATIKANA KWA HILA . UMINYAJI HAKI NA UONEVU ULIOKUBUHU.

NEC haikwepi lawama hadi sasa, Propaganda huwa hazidumu NA SIO "GUARANTEE" kusaidia Tanzania kuwa na AMANI YA KUDUMU KILA SIKU.

NEC imecheza mdundo wa CCM na watawala kwa kukubali kuhenyeshwa wakurugenzi na wasimamizi wa uchaguzi kuingia katika mtego. Likiharibika basi NEC hawawezi kukwepa lawama.

MAMBO MAWILI YA KUZINGATIWA KWA SASA
Tanzania inaninginia baina ya muda wa RUFAA ZA MAPINGAMIZI YA OVYO na baina ya UPIGAJI KURA NA KUTENDA HAKI HAPO TARAHE 28 Oktoba, 2020.

Huo ndio muda ambao Busara za NEC na ueledi utaivusha Tanzania yetu.

Tunajuwa namna NEC inavyopata masindikizo ya kutokubali hoja za rufaa huko, tunajuwa namna wanavyopata "pressure" ya wadau wa demokrasia na tunajuwa namna wanavyokosa msimamo wa pamoja kutokana na kuchanganywa taaluma za sheria na wanasiasa huko NEC wenyewe.

NEC haipaswi "ku-risk" amani ya Tanzania kwa kutaka kuwafurahisha watawala waovu wasioitakia mema Tanzania kwa kisingizio cha Madaraka yao.

Mtihani wa kwanza kwa sasa ni RUFAA ZA MAPINGAMIZI baada ya NEC kukubali kucheza mdundo wa CCM

Mtihani wa Pili ni haki na Uchaguzi siku ya tarehe 28 Oktoba ikiwa NEC itafanikiwa kuruka kiunzi cha kwanza cha rufaa kama nilivyoeleza.

NEC inapaswa kujuwa ukubwa wa dhamana waliyopewa kwamba inavuka mipaka ya Tanzania yetu. Dunia inawatazama kwa karibu na kila tukio na hatua zinarikodiwa vyema.

Mazoea ya NEC kuwadekeza CCM hasa hii miaka mitano 2015 - 2020 ya CCM kufanya watakavyo kwa kuwatumia wakurugenzi makada na watiifu kwa CCM haiwezi ikawa kinga kwao. Mwenyekiti na Mkurungenzi wake Mkuu watabeba lawama zote.

USHAURI KWA NEC.

Simamieni HAKI na SHERIA bila upendeleo na msiwe sehemu ya hila dhidi ya wengine.

Kwa mifano yenu ya kuwaenguwa UPINZANI tu kote BARA NA ZANZIBAR tayari mmeshafanya KOSA la awali na endelevu ambalo kujisafisha kwenu kutakuwa kugumu na kuanzia hapo mna wakati mgumu kujisafisha hilo eleweni.

NEC mnao muda wa kurekebisha mkitaka, hizo pressure za CCM zisiwatishe kumbukeni maisha baada ya uchaguzi.

Kumbukeni "timing" ya wapinzani si ya kubahatisha waliwasoma wakawaelewa watawala , NEC, vyombo vya haki, vyombo vya Dola na taasisi za kidini zinazotumika na KWA KWELI WALIWAELEWA VILIVYO.
Mstirajie WAPINZANI watapotenza hii fursa nakuambieni.

MWISHO
Tunachukuwa hii fursa kutimiza wajibu wetu kama raia wa nchi hii kuwaomba NEC kusimamia haki na usawa walau kwa hii fursa ndogo ya kuitunza amani ya Tanzania iliyobaki.

Yaliyofanyika ndani ya miaka hii mitano hayapaswi kujirejea kwenye uchaguzi huu ambao ndio fursa ya mwisho kwa wapinzani, wanamageuzi , wapenda haki na wanademokrasia kote ZANZIBAR na BARA na dalili zote zinaonesha hatari iliyoko mbele.

Shime NEC tendeni haki na msimamie haki kwa dhati.


Kishada.
Kwa kuwa mgombea wao anakubalika na amefanya mambo mengi mazuri hivyo hana hofu ya kugaragazwa na NEC itatenda haki uchaguzi uwe huru na wagombea wote watarudi.
 
Simamieni HAKI na SHERIA bila upendeleo na msiwe sehemu ya hila dhidi ya wengine.

Kwa mifano yenu ya kuwaenguwa UPINZANI tu kote BARA NA ZANZIBAR tayari mmeshafanya KOSA la awali na endelevu ambalo kujisafisha kwenu kutakuwa kugumu na kuanzia hapo mna wakati mgumu kujisafisha hilo eleweni.
haya wanayafanya kwa maagizo toka juu! kumbukeni ccm bila hila, uongo, gilba, ubinafsi, uhujumu na wizi hakiwezi kamwe kuwepo ktk uso wa dunia.
 
Mazoea ya NEC kuwadekeza CCM hasa hii miaka mitano 2015 - 2020 ya CCM kufanya watakavyo kwa kuwatumia wakurugenzi makada na watiifu kwa CCM haiwezi ikawa kinga kwao.
Ninaamini baadhi ya wakurugenzi kwa sasa wameanza kushtuka. Wapo baadhi ambao kiuhalisia mazingira yatawasukuma kutangaza wapinzani. Na ikitokea wakapindua meza, watapata majibu yao papo hapo. Namuonea huruma sana mkurugenzi wa jiji fulani. Ni suala la wakati tu. Tutaona
 
Ukitaka kuamini kama sisi waafrika tuna shida , tazama vijisheria vya uchaguzi vya kubumba vilivyotungwa namna vinavyojizonga. eti Msajili, Tume na wagombea wote wanaweza kuweka Pingamizi.

Yaani hata Mutungi kwa chuki zake dhidi ya Maalim Seif kwa Mfano anapewa nafasi ya kutumia ghilba kuweka Pingamizi.

Walikusudia nini kama sio kukwaza mchakato.

Hadi leo tarehe 8 Septemba 2020 wiki mbili baada ya kuanza kampeni za Ubunge , udiwani na Rais eti kuna majimbo, vyama na wagombea wake hawajui kama ni ndege au ni popo.

Katikati ya Kampeni wengine hawajijui wako wapi. Hii ni mifano ya uchafu wetu sisi Waafrika.
 
NEC kazeni hivohivo sie tunataka kuwaona makeyboard warriors barabarani
Kumbuka kwamba wakati NEC wanakaza hivyo hivyo kwa mujibu wa kauli yako, basi Dada na ndugu zako nao wanakazwa kweli kweli. Siku likiharibika usije ukajificha uje hapa hapa uwasifu tume kwa kuvuruga amani yetu.

Sisi wengine uwezo wetu ni kutumia Bando na muda wetu kutahadharisha, ndio uwezo wetu.
 
Unapoteza muda tu mkuu jamaa hawashauriki, siyo makosa yao.
Nimetimiza wajibu wangu Mkuu.

Uwezo wangu ni kutumia bando, kujificha nyuma ya keyboard, kutumia muda wangu na nguvu chache za akili ili kuonya na kushauri.

NEC wasije kulaumu kwamba watanzania hawakupaza sauti kuwasaidia dhidi ya masindikizo ya CCM.
 
Back
Top Bottom