NEC lazima mjue Wasabato wana haki ya kupiga na kupigiwa kura

Paulo anaendelea kusema kwamba “huduma ya kifo” iliyoandikwa kwenye jiwe ilikuwa na aina ya utukufu katika ule muda ambao Musa alipewa. Lakini Paulo anaelezea kwamba ‘utukufu wa Roho Mtakatifu” – ambao Paulo sasa anauita “huduma ya haki” – ni mkubwa zaidi kuliko “utukufu wa andiko”, ambao Paulo sasa anauita “huduma ya hukumu”. Anatufundisha kwamba utukufu wa Roho (kwenye Agano Jipya) ni mkubwa kuliko wa utukufu wa amri ulioandikwa kwenye vibao vya mawe, ni kama vile utukufu wa amri ulioandikwa kwenye mawe hauna utukufu sasa (mstari wa 10). Kiuhalisia anatuambia kwamba utukufu wa huduma ya Roho na wa haki ni mkubwa sana kiasi kwamba Mungu ameacha utukufu wa huduma ya maandishi ya kwenye vibao iliyoandikwa kwenye jiwe (mstari wa 11). Waadiventista hawaelewi neno la Mungu katika sura hii, na katika mafundisho yao wanafufua au wanarudisha ‘huduma ya andiko iliyoandikwa kwenye vibao vya mawe’ ambayo inawafanya watu waendelee kubaki katika kifo cha kiroho na hukumu. Wanaitukuza huduma hii kinyume na Agano Jipya la Mungu ambalo linaweka sheria zake ndani ya mioyo yetu kwa Roho wake. Waadventista wanafuata haki, ila katika kutilia mkazo katika sheria ya Musa, wanasababisha kifo na hukumu. Na ni haki ambayo Waadventista wanasema wanaishi kwayo, ambayo kabisa wanakosa na kushindwa kuipata kwa mafundisho yao kuhusu sheria. (Warumi 10:2,3).

Naelezea zaidi kuhusu hili katika makala yangu nyingine (Je, Tukusanyike Siku Gani Kati ya Jumamosi na Jumapili?), ila acha nioneshe hapa kwamba wale wanaohubiri kutunza/kufuata sheria ya Musa wapo kinyume na huduma ya Roho, wala hawajui huduma ya Roho katika maisha yao inayozaa matunda ya haki. Kwa kupitia huduma ya Roho tu ndio tunapata ubatizo katika Roho anayetupa uzima, uzima wa Yesu ndani yetu ambao kwa huo tunaishi maisha ya kitakatifu na kuzaa matunda ya haki. Kwa kutilia mkazo katika kufuata amri kumi, Waadventista wanazuia neema ya Kristo (Wagal. 1:6) na kujaribu utakatifu uliokamilika “katika mwili” badala ya katika imani na katika Roho ya Kristo (Gal 3:2,3). Waadventista hawaelewi nguvu ya Injili kama ilivyotangazwa katika Warumi 8:1-4. Kwa mantiki hii wale wanaofuata mafundisho ya Waadventista wamewekwa nje katika kujua nguvu ya ukombozi wa Kristo katika kuwafanya wenye haki na watakatifu, na katika mantiki hii, Uadventista sio Ukristo; zaidi ya hili, kiuhalisia, unapinga Injili kama Paulo alivyoweka wazi katika barua yake yote kwa Wagalatia.

Katika maono yake, tunaona kwamba Ellen White na Waadventista kwa kupitia upotefu huu wamebadilisha sehemu sahihi ambayo Mungu amempa Kristo Yesu, na badala yake, Sheria, na hasa sheria ya Sabato! Wanataka wawapeleke watu kwenye Agano la Kale na waishi huko! Ni udanganyifu gani huu, hii ni kuinua sheria juu ya Yesu Kristo!

Ellen White alisema kwamba amri ya nne iling’aa juu ya zote na kuzungukwa na duara linalong’aa na ilitengwa kutunza heshima ya jina la Mungu! Anaendelea kusema kwamba kama amri ya nne inaweza kuvunjwa basi amri nyngine zote zinaweza kuvunjwa! (Early Writings of Ellen G. White, p.32,35). Labda hii inaweza kukusaidia kuelewa kwa nini Waadventista wengi wanasema kwamba kama tusipotunza sabato ni sawa na kusema tunaweza kufanya dhambi za kuvunja amri nyingine tisa! Hawaelewi kabisa Agano Jipya wanaposema “kama tunaweza kuvunja sabato ni sawa na kusema tunaweza kuzini!” (Haishangazi Waadventista hawawezi kusikia au kuelewa tunayosema wakati akili zao zimepofushwa na roho hii ya udanganyifu). Akili za Waadventista yamepotoshwa na mafundisho haya, na matokeo kwamba kushika sheria ni sehemu muhimu ya dini yao na ni aina hii ya dini ambayo Paulo alihubiri dhidi yake katika barua yake kwa Wagalatia. Tunaona kuwa mafundisho ya Wasabato juu ya siku ya saba hayatokani na maandiko bali yanatokana moja kwa moja na maono ya Ellen White ambayo yaliipa sheria nafasi ya kwanza badala ya Yesu Kristo. Nao Waadventista walitafsiri maandiko kufuatana na maono yake, na kwa kufanya hivyo wanapotosha maandiko yote!
 
Waadventista wana orodha ya imani 28 za msingi (unaweza kusoma mwenyewe kwenye tovuti yao ya rasmi). Namba 20 inahusu sabato, na inasema, “amri ya nne ya sheria ya Mungu isiyobadilika inahitaji kushikwa kwa siku hii ya saba ya sabato…. Ni ishara ya ukombozi wetukatika Kristo, ishara ya utakaso wetu, ishara ya utii wetu.” (“The fourth commandment of God’s unchangeable law requires the observance of this seventh-day Sabbath… It is a symbol of our redemption in Christ, a sign of our sanctification, a token of our allegiance.”) Kwa hiyo wanasema kwamba kushika sabato ni ishara ya ukombozi wako na utakaso! Watu hawa wamezua dini mpya lakini hakika sio Ukristo! Sisi tunakombolewa kwa damu ya Yesu Kristo; sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa damu yake na kwa Roho wa Mungu. Hili limeshatimizwa kwa ajili yetu na Yesu Kristo, na utakaso wetu umeonyeshwa kwa kupitia maisha yaliyobadilishwa kwa imani katika Kristo na si kwa utunzaji wa sheria ya sabato!

Namba 19 ya sheria ya msingi ya imani ya Waadventista (inayoitwa “Sheria ya Mungu”) inasema, “Kanuni kuu za sheria ya Mungu ni ilivyo katika amri kumi, na imeonyeshwa kwa mfano katika maisha ya Kristo. Maagizo haya ni msingi wa Agano la Mungu na watu wake na kiwango katika hukumu ya Mungu.” (“The great principles of God’s law are embodied in the Ten Commandments and exemplified in the life of Christ… These precepts are the basis of God’s covenant with His people and the standard in God’s judgment.”)

Ni wazi kuwa kwa sentensi hizi Waadventista wamekataa ukweli wa Injili na hawana uelewa wa Agano Jipya. Msingi wa Agano Jipya la Mungu na watu wake ni damu ya mwanae Yesu Kristo – sio amri kumi! (Luka 22:20, Waebrania 9;14-20;12:24; 13:20). Ukamilifu wa Mungu umewekwa katika Yesu Kristo – na sio katika amri 10! (Wakolosai 2:9). Mungu sio maandiko yaliyoandikwa kwenye vibao vya mawe; Yeye ni uzima wenyewe, na kutimiza haki ya sheria tunahitaji maisha yake ndani yetu na kuishi kwa imani ndani yake. Yesu Kristo alisema yeye ni njia ya ukweli na uzima! Kristo anayeishi ndani yetu ni njia ya kutimiza haki – na sio kutunza sheria (warumi 8:2-4). Msingi wa Agano la Mungu na sisi ni kifo na ufufuo wa mwanawe! Kama mafarisayo, ndivyo wasabato hao wanashika kwa makini sheria. Wanaabudu maadhimisho ya mambo ya sheria na kukataa njia ya Mungu katika uzima na haki kwa njia ya imani katika mwana wake Yesu Kristo. Kupitia bidii yao katika sheria wanakosa kabisa haki ya sheria; wanashindwa kutimiza haki kwa mujibu wa sheria hata kama inasemwa katika Warumi 10:2-4. Je, hawajasoma, “hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria.” (Warumi 3:20)? Kiwango katika hukumu ya Mungu siyo amri kumi kama Wasabato wanadai katika udanganyifu wao, bali ni Yesu Kristo mwenyewe,

“Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na Injili yangu, kwa Kristo Yesu.” (Warumi 2:16).
 
Wasabato wapo wachache sana lakini wanapenda kuinekana wananguv kuliko wote

Sisi tukisema jumapili siku ya sala sijui itakwaje
Nieleweke kuwa siongelei ukubwa au ubora wa dini yoyote hapa, ninaongelea uwezekano wa wasabato kutopiga kura siku ya Jumamosi basi na si vinginevyo haya mengine mnayaleta nyinyi na wala hizo dini zingine hazijalalamika!
 
Wasabato sio wachache kama mnavyodhani, ni moja ya dini yenye wafuasi wengi tu hapa Tanzania hasa mikoa ya kanda ya ziwa, kuna baadhi ya vijiji katika mikoa hiyo pengine unaweza kupata robo tu ya wakazi wakaenda kupiga kura, muulize Kangi Lugo la, Ester Bulaya, Chenge, hata Rais Magufuli mwenyewe hawezi kubali huo ujinga anajua atapoteza kura kiasi ambacho si cha kupuuza, kwa makadirio ya chini wana kura zisizopungua 500,000. Hakuna chama kitakuwa tayari kupoteza hizo kura, wala hakuna nchi ya watu makini inaweza kutupa kura kiasi hicho kisa SIKU, kuhusu wakristo wengine wanaosali Jumapili hawajawahi lalamika dini na imani zao zinaruhusu kufanya shughuli zingine baada ya kusali na hii imefanyika kwa zaidi ya miaka hamsini ni nini leo kinalazimisha tuba dili siku ili tuanze mgogoro usio kuwa na maana.
Idadi ya washiriki wa kanisa la Waadventista Wa Sabato nchini Tanzania imeonekana kuwa na idadi ndogo iliyoongezeka katika kipindi cha miezi 10 iliyopita.
Takwimu zilizotolewa mwaka huu na makao makuu ya kanisa hilo katika maeneo yake mawili ya kiutendaji hapa Tanzania yaani Unioni Konferensi ya Kaskazini na Unioni ya Kusini zinaonesha kuwa Unioni ya Kaskazini yenye konferensi nne mpaka kufikia mwishoni mwa robo ya pili ya mwaka 2014 ilikuwa na washiriki 336,305 na ile ya kusini yenye konferensi mbili ina washiriki 104,348.
Hii inamaanisha kwamba kuna washiriki wa kanisa hilo kwa sasa wapatao 440,653 kati ya watanzania zaidi ya milioni 40 kwa mujibu wa takwimu hizo ambalo ni ongezeko la washiriki 29,362 katika kipindi cha miezi 10 toka disemba mwaka jana.
Takwimu zilizotolewa na Uongozi wa Kanisa hilo Disemba mwaka jana zinaonesha kulikuwa na washiriki wa kanisa hilo wapatao 322,351 katika Unioni Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania na washiriki 88,940 katika Unioni ya kusini mwa Tanzania hii ni kwa mujibu wa Takwimu zilizotolewa na uongozi wa kanisa hilo nchini.
Hata hivyo utafiti unaonesha kuwa makanisa mahalia yamekuwa yakishindwa kutoa malezi ya kiroho na kuratibu idadi kubwa ya washiriki wapya wanaoongezeka kutokana na mikutano mbalimbali ya injili inayofanyika nchini ambapo jumla ya watu 35,657 walibatizwa katika kanisa hilo katika kipindi cha mwezi Januari hadi Septemba mwaka jana na hivi karibuni huko jijini mwanza walibatizwa watu 3000
Kanisa la Waadventista Wa Sabato duniani lina waumini milioni 18 katika nchi 215 zilizopo kwenye divisheni 13 za kanisa hilo.

NB:
Tuna jaribu kuonesha kuwa Wasabato ni wapotoshaji... na wewe umejaribu kupotosha takwimu... eti kanda ya ziwa ni wasabato laki tano walio piga kura au kujiandikisha, taarifa ambazo zina kinzana na chombo chenye mamlaka nchini tena cha kisabato...
 
kuingiliwa huko ni kuwa namna gani unapo sema hivyo...? na zao zina weza ingilia serikali...? Mf. kufanya siasa badala ya Dini kama usajili wake ulivyo... nani hapa ana haki juu ya mwingine? Ndio maana mna taadhalishwa ktk vitabu vyenu vya dini.... heshimuni mamlaka zenu ambazo pia ni mamlaka za Mungu...!
Ungekuwa umesoma na kuelewa wala usingenijibu kwa majibu mepesi ya namna hiyo!
 
Naona hapa mtoa maada anakumbusha kwamba katiba inatoa haki kwa mtanzania yoyote kuwa na uhuru wa kuabudu kwahiyo usiingiliwe kwa kuweka kupiga kura( Chaguzi mbalimbali)
 
Waadventista wana orodha ya imani 28 za msingi (unaweza kusoma mwenyewe kwenye tovuti yao ya rasmi). Namba 20 inahusu sabato, na inasema, “amri ya nne ya sheria ya Mungu isiyobadilika inahitaji kushikwa kwa siku hii ya saba ya sabato…. Ni ishara ya ukombozi wetukatika Kristo, ishara ya utakaso wetu, ishara ya utii wetu.” (“The fourth commandment of God’s unchangeable law requires the observance of this seventh-day Sabbath… It is a symbol of our redemption in Christ, a sign of our sanctification, a token of our allegiance.”) Kwa hiyo wanasema kwamba kushika sabato ni ishara ya ukombozi wako na utakaso! Watu hawa wamezua dini mpya lakini hakika sio Ukristo! Sisi tunakombolewa kwa damu ya Yesu Kristo; sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa damu yake na kwa Roho wa Mungu. Hili limeshatimizwa kwa ajili yetu na Yesu Kristo, na utakaso wetu umeonyeshwa kwa kupitia maisha yaliyobadilishwa kwa imani katika Kristo na si kwa utunzaji wa sheria ya sabato!

Namba 19 ya sheria ya msingi ya imani ya Waadventista (inayoitwa “Sheria ya Mungu”) inasema, “Kanuni kuu za sheria ya Mungu ni ilivyo katika amri kumi, na imeonyeshwa kwa mfano katika maisha ya Kristo. Maagizo haya ni msingi wa Agano la Mungu na watu wake na kiwango katika hukumu ya Mungu.” (“The great principles of God’s law are embodied in the Ten Commandments and exemplified in the life of Christ… These precepts are the basis of God’s covenant with His people and the standard in God’s judgment.”)

Ni wazi kuwa kwa sentensi hizi Waadventista wamekataa ukweli wa Injili na hawana uelewa wa Agano Jipya. Msingi wa Agano Jipya la Mungu na watu wake ni damu ya mwanae Yesu Kristo – sio amri kumi! (Luka 22:20, Waebrania 9;14-20;12:24; 13:20). Ukamilifu wa Mungu umewekwa katika Yesu Kristo – na sio katika amri 10! (Wakolosai 2:9). Mungu sio maandiko yaliyoandikwa kwenye vibao vya mawe; Yeye ni uzima wenyewe, na kutimiza haki ya sheria tunahitaji maisha yake ndani yetu na kuishi kwa imani ndani yake. Yesu Kristo alisema yeye ni njia ya ukweli na uzima! Kristo anayeishi ndani yetu ni njia ya kutimiza haki – na sio kutunza sheria (warumi 8:2-4). Msingi wa Agano la Mungu na sisi ni kifo na ufufuo wa mwanawe! Kama mafarisayo, ndivyo wasabato hao wanashika kwa makini sheria. Wanaabudu maadhimisho ya mambo ya sheria na kukataa njia ya Mungu katika uzima na haki kwa njia ya imani katika mwana wake Yesu Kristo. Kupitia bidii yao katika sheria wanakosa kabisa haki ya sheria; wanashindwa kutimiza haki kwa mujibu wa sheria hata kama inasemwa katika Warumi 10:2-4. Je, hawajasoma, “hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria.” (Warumi 3:20)? Kiwango katika hukumu ya Mungu siyo amri kumi kama Wasabato wanadai katika udanganyifu wao, bali ni Yesu Kristo mwenyewe,

“Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na Injili yangu, kwa Kristo Yesu.” (Warumi 2:16).
Nina swali dogo tu kwako,
Mungu ana kigeugeu?

Ni sehemu ipi ya torati la manabii iliondolewa na Yesu Kristo?

Kuna amri yoyote ile iliruhusiwa kuvunjwa baada ya kifo cha Kristo.
Kwa nini Kristo alisema hakuja kuvunja torati na kwamba hakuna kitakachopungua hadi utimilifu alikuwa anawaambia kizazi gani, je sisi hayatuhusu?
Hata hivyo katafakari wala sihitaji majibu sio msingi wa mada
 
takwimu zina jieleza vizuri tu... na wasabato sio dini yenye nguvu... maana kama ingekuwa ina nguvu wasinge lalama hivi wange chukua hatua...

wakatoliki na madhehebu mengine yanayo fanya ibada J2 waliambiwa wakitoka kwenye ibada wakapige kura na viongozi wa dini wali wasisitiza waumini wao wafanye hivyo... na zoezi lilienda vizuri bila shida...

hawa kwakuwa ni dini inayo jieleza kutoka kwa muasisi wake na madhumuni yao yapo wazi kabisa... Jmosi ni siku ya shetani ina itwa hivyo kwa mujibu wa mhasisi wa dini hiyo mama ellen...

na shetani siku zote hawezi shindana na mungu na akashinda ndio maana ameweza wateka wachache na wengi wame poneka toka kwa shetani... wapo Millioni 17 mpaka 18 kwa makisio Duniani kote... wakati waislamu kwa tanzania ni million 13 kwa makadilio... hapa utaona tu kuwa mungu hashindwi na chochote hasa muovu shetani.... kwa kutumia jina lake na uruma yake kuuadaa ulimwengu... kama vle shetani alivyo taka kumuadaa Yesu...
 
Nadhani hujanielewa nimesema kwa mujibu wa imani ya Wasabato siku hiyo ni kwaajili ya kuabudu tu na si vinginevyo huwa hawafanyi kazi nyingine yoyote.
Kwa mujibu wao wenyewe,na si kwa mujibu wa NEC
 
Naona hapa mtoa maada anakumbusha kwamba katiba inatoa haki kwa mtanzania yoyote kuwa na uhuru wa kuabudu kwahiyo usiingiliwe kwa kuweka kupiga kura( Chaguzi mbalimbali)
kama una uhuru wa kuabudu nenda kaabudu... fata imani yake mengine ya kaisali muachie kaisali... tofauti na hapo una zidi kutuonesha jinsi unavyo lega lega kiimani... ya Mungu una yataka na Ya kaisali pia...
 
Nina swali dogo tu kwako,
Mungu ana kigeugeu?

Ni sehemu ipi ya torati la manabii iliondolewa na Yesu Kristo?

Kuna amri yoyote ile iliruhusiwa kuvunjwa baada ya kifo cha Kristo.
Kwa nini Kristo alisema hakuja kuvunja torati na kwamba hakuna kitakachopungua hadi utimilifu alikuwa anawaambia kizazi gani, je sisi hayatuhusu?
Hata hivyo katafakari wala sihitaji majibu sio msingi wa mada
naona imekuingia sasa....! kutoka kuwa sio lengo la Uzi na kuanza kuhoji kilicho andikwa...

ngoja nikupe vingine ili ukombolewe na damu ya kristu na sio sabato...
 
“Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda… Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama Yeye alivyo mtakatifu… Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.” (1 Yoh. 2:6; 3:2,3; 4:17.)

Ingawa mengi zaidi yanaweza kuongelewa kuhusu sheria na imani, nimeandika kikamilifu kuhusu hili katika makala nyingine inayoitwa “Tukusanyike siku gani kati ya jumamosi na jumapili?” Kwa hiyo tafadhali soma makala hiyo ambapo nimeenda katika maandiko mengi ambayo yanahusiana na tofauti kati ya kuishi kwa imani na kuwa chini ya sheria.

Maria alikuwa mama wa Yesu duniani, lakini wale wakatoliki wanaoomba kwake hufanya ibada ya sanamu. Mungu alitoa sheria kupitia Musa, lakini katika Agano Jipya Mungu ametupa Yesu Kristo ili tupate kutimiza haki kwa njia ya “imani ndani yake” – si kwa “kushika sheria ya Musa”. Kwa mafundisho yao Waadventista hufanya ibada ya sanamu na kuinua sheria juu ya Yesu Kristo. Kwa kuitukuza sheria, hasa ya amri ya nne, wamepotoshwa kuhusu maana ya Agano Jipya na wametolewa nje ya wokovu kutoka kwa Mwana wa Mungu.

Ibada hii ya sanamu inajionyesha yenyewe katika udanganyifu zaidi na Ellen White katika habari za siku ya sabato. Yeye hufundisha kwamba utunzaji wa sabato utakuwa upimaji mkubwawa uaminifu miongoni mwa Waristo – itawatofautisha kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia! Alisema wale waumini wanaokutana jumapili huonesha ‘uhaini’ wao kwa Mungu kwa kuiinamia “sheria ya nchi”, na katika nyakati za mwisho wao ndio watakaokuwa na chapa ya Mnyama! ‘Waumini’ wanaotunza sabato wanaonyesha uaminifu kwa mamlaka ya Mungu na wao atawapa “muhuri ya Mungu” uliotajwa katika kitabu cha Ufunuo. Wengine wote (pamoja na wale wanaokiri Kristo) watapokea chapa ya Mnyama! Waadventista mara nyingi huwaita Wakristo wasiotunza sabato na sheria ya Musa “kanisa potofu” , “makanisa yaliyoanguka” au “babeli”. Na wanafanya hivyo pia kwa Wakristo wasiokubaliana nao kwenye vikao kama vile vikundi vya facebook. Hiki ndo ambacho Ellen White aliandika,
 
“Niliona kwamba sabato ni, na itakuwa, ukuta utakaotenganisha Waisraeli wa kweli wa Mungu (yaani, wale wanaoshika siku ya sabato) na wasioamini (yaani, wote wasioshika siku ya sabato).” Early writings p.32,33.

“Alama au muhuri ya Mungu ni sabato yake, na muhuri au alama ya Mnyama na kupinga sabato.” (The Great Controversy page 691, 1888 edition.)

“Niliona kwamba Mungu ana wana waaminifu miongoni mwa makanisa yalioanguka na kabla mapatilizo hayajaachiwa, wahubiri na watu wataitwa kutoka katika makanisa haya na kwa furaha watapokea ile kweli… Wote walio waaminifu wataondoka katika makanisa yaliyoanguka, na kusimama na masalia.” (Early Writings p.261.)

Hivyo fundisho hili linafikia kiwango cha uongo kamili. Linasema kuwa, si tu kwamba tunatakiwa kutunza sheria ya Musa kwa ujumla wake, lakini iwapo hatutatunza hii sabato ya nje tutakuwa ni sehemu ya haya makanisa yaliyoanguka (au Babeli) na tutakuwa ni sehemu ya wale wanaopokea chapa ya mnyama! Je, hapo unaweza kuona kanisa la Wasabato linavyotuingiza kwenye mtego wa kanisa la vifungo na hofu?

Kanisa la Wasabato lina mfumo wa kuamini ambao sio tu kwamba unawaweka nje ya Injili ya kikiristo, bali hata katika upinzani dhidi ya injili! Katika maana hii kanisa la Sabato ni kama kanisa la Mormons na kanisa la Mashahidi wa Jehova. Joseph Smith, aliyeanzisha kanisa la Mormons alidai kuwa aliona maono na kusema kuwa malaika alimsaidia kutafsiri kwa Kiingereza kitabu cha sahani za dhahabu. Vivyo hivo usabato hutegemea kwa wingi maono na mafundisho ya Ellen White kwa ajili ya kuelewa na tafsiri ya maandiko. Kanisa la Sabato hujitahidi sana kukataa dhana hii, wakisema kuwa Biblia iko juu zaidi katika mafundisho na matendo. Na kwa wazi kabisa husema,
 
“Hatuamini kuwa maandiko ya Ellen White yanaweza kutumika kama msingi wa mafundisho… Hatuamini kuwa Biblia inaweza tu kueleweka kupitia maandiko ya Ellen White” (“We do not believe that the writings of Ellen White may be used as the basis of doctrine… We do not believe that Scripture can be understood only through the writings of Ellen White.”)

Hii sio kweli; hebu angalia matumizi ya neno “tu” katika sentensi iliyotangulia! Wanachomaanisha ni kuwa tafsiri yao ni inafanana na ya Ellen White na hivyo hawamtegemei yeye (lakini ni tafsiri inayofanana na ya kwake kwa sababu waliathiriwa na yeye!). Hii ni hoja inaendelea katika mzunguko! Tunakaribia ukweli halisi tunapoangalia kauli nyingine wanazotoa kuhusu maandiko ya Ellen White:

Hatuamini kuwa ubora au kiwango cha uvuvio (inspiration) katika maandiko ya Ellen White ni tofauti na maadiko ya biblia… Tunaamini kuwa Ellen White alivuviwa na Roho Mtakatifu na kuwa maandiko yake, yatokanayo na uvuvio huo, yanahusu na yana mamlaka, na hasa kwa Waadventista Wasabato” (“We do not believe that the quality or degree of inspiration in the writings of Ellen White is different from that of scripture… We believe that Ellen White was inspired by the Holy Spirit and that her writings, the product of that inspiration, are applicable and authoritative, especially to Seventh-day Adventists.” The Adventist Review, December 23, 1982, The Inspiration and Authority of the Ellen G. White Writings, Ten Affirmations and Ten Denials on Ellen White’s Authority).

Hivyo hapa wanaeleza kwa uwazi kabisa kuwa ubora au kiwango cha uvuvio cha Ellen White ni sawa na cha Biblia (hata kama siku hizi wanajaribu kuzikana), na kuwa maandiko yake yanaendana na yana mamlaka. Wasabato wanaamini kuwa maono na mafundisho ya Ellen White nilioorodhesha hapo juu yamevuviwa na Mungu! Hii inaonesha jinsi kanisa zima la Wasababto lilivyodanganyika. Hakuna kanisa la kikristo linaloweza kueleza hivi juu ya mwandishi wao yeyote yule, hata kama wanamwamini au kufuata mafudisho yake kiasi kwa gani.
 
Tuliwahi kuwa na semina Morogoro na nilikuwa na majadiliano na muumini wa kanisa la sabato. Baada ya kumwonyesha maandiko toka Wagalatia na Wakolosai hatimaye alikubali kuwa ni makosa kuwaeleza watu kuwa wanatakiwa kukusanyika siku ya sabato. Shauku yangu ni kuwa watu wasizuiwe kupata wokovu kamili ambao upo katika Yesu Kristo na ndio sababu nimeandika makala haya. Ni kwa ajili ya watu wale ambao hawana uhakika na wanahitaji wa maelezo ya kimaandiko na ufafanuzi, na kwa hao ambao ijapokuwa ni wasabato, hawajaarithiriwa na kupofushwa na mafundisho ya namna hiyo. Mungu huangalia mioyo yetu na ninafikri inawezekana kwamba mtu akisikia kwa mara ya kwanza kupitia kanisa la sabato habari za Yesu kufa kwa ajili ya dhambi zao na kuamini, Mungu aweza kutenda katika maisha yao. Iwapo moyo wa mtu huyu ni wazi na kweli mbele za Mungu, basi kusoma kwake neno la Biblia kutamwongoza kutoka katika uongo huu wa kanisa la Sabato. Na hivyo, makala hii imeandikwa katika matumaini hayo, kwa sehemu, ili kuwafikia watu kama hao. Lakini kwa wale ambao tayari wameshaathriwa kwa kina sana na mafundisho haya Wasabato na ambao wana bidii sana katika Sheria, upofu na uongo ambao hutenda kazi mioyoni mwao hufanya vigumu kwao kukiri ukweli na kuelewa kile ambacho kiko wazi kabisa katika maandiko ya Biblia. Kama mafarisayo watapinga na kupambana na ukweli wa Injili.

Baadhi ya watu hubishana na Wasabato kana kwamba wasabato ni Wakristo ambao hushika mafundisho yaliyo tofauti na Wakristo wengine. Watu wanaofanya hivyo wanakuwa hawawatendei haki Wasabato! Kushindana na Wasabato kana kwamba ni Wakristo wenzao ni kuwadanganya! Iwapo unataka kuwa rafiki wa kweli na iwapo unataka kuwapenda upendo ule wa Injili, inakubidi kuwaasa kuwa wanafundisha “injili nyingine” (Gal 1:8) na kwamba wanajiweka chini ya laana (Wagal. 3:10), kwamba dini yao ni bure (Gal 4:11), kwa Yesu hana faida yoyote kwao na kuwa wameanguka kutoka kwenye neema (Gal 5:4)! Hii sio kuwahukumu; hii sio kuwakashifu wala sio kuwa katili kwao. Bali huu ni uhalisia ambao pendo letu kwa Bwana Yesu na ukweli wake vinatakiwa kutuongoza katika kutangaza.
 
Back
Top Bottom