Chillah
JF-Expert Member
- Oct 12, 2016
- 8,287
- 8,828
Paulo anaendelea kusema kwamba “huduma ya kifo” iliyoandikwa kwenye jiwe ilikuwa na aina ya utukufu katika ule muda ambao Musa alipewa. Lakini Paulo anaelezea kwamba ‘utukufu wa Roho Mtakatifu” – ambao Paulo sasa anauita “huduma ya haki” – ni mkubwa zaidi kuliko “utukufu wa andiko”, ambao Paulo sasa anauita “huduma ya hukumu”. Anatufundisha kwamba utukufu wa Roho (kwenye Agano Jipya) ni mkubwa kuliko wa utukufu wa amri ulioandikwa kwenye vibao vya mawe, ni kama vile utukufu wa amri ulioandikwa kwenye mawe hauna utukufu sasa (mstari wa 10). Kiuhalisia anatuambia kwamba utukufu wa huduma ya Roho na wa haki ni mkubwa sana kiasi kwamba Mungu ameacha utukufu wa huduma ya maandishi ya kwenye vibao iliyoandikwa kwenye jiwe (mstari wa 11). Waadiventista hawaelewi neno la Mungu katika sura hii, na katika mafundisho yao wanafufua au wanarudisha ‘huduma ya andiko iliyoandikwa kwenye vibao vya mawe’ ambayo inawafanya watu waendelee kubaki katika kifo cha kiroho na hukumu. Wanaitukuza huduma hii kinyume na Agano Jipya la Mungu ambalo linaweka sheria zake ndani ya mioyo yetu kwa Roho wake. Waadventista wanafuata haki, ila katika kutilia mkazo katika sheria ya Musa, wanasababisha kifo na hukumu. Na ni haki ambayo Waadventista wanasema wanaishi kwayo, ambayo kabisa wanakosa na kushindwa kuipata kwa mafundisho yao kuhusu sheria. (Warumi 10:2,3).
Naelezea zaidi kuhusu hili katika makala yangu nyingine (Je, Tukusanyike Siku Gani Kati ya Jumamosi na Jumapili?), ila acha nioneshe hapa kwamba wale wanaohubiri kutunza/kufuata sheria ya Musa wapo kinyume na huduma ya Roho, wala hawajui huduma ya Roho katika maisha yao inayozaa matunda ya haki. Kwa kupitia huduma ya Roho tu ndio tunapata ubatizo katika Roho anayetupa uzima, uzima wa Yesu ndani yetu ambao kwa huo tunaishi maisha ya kitakatifu na kuzaa matunda ya haki. Kwa kutilia mkazo katika kufuata amri kumi, Waadventista wanazuia neema ya Kristo (Wagal. 1:6) na kujaribu utakatifu uliokamilika “katika mwili” badala ya katika imani na katika Roho ya Kristo (Gal 3:2,3). Waadventista hawaelewi nguvu ya Injili kama ilivyotangazwa katika Warumi 8:1-4. Kwa mantiki hii wale wanaofuata mafundisho ya Waadventista wamewekwa nje katika kujua nguvu ya ukombozi wa Kristo katika kuwafanya wenye haki na watakatifu, na katika mantiki hii, Uadventista sio Ukristo; zaidi ya hili, kiuhalisia, unapinga Injili kama Paulo alivyoweka wazi katika barua yake yote kwa Wagalatia.
Katika maono yake, tunaona kwamba Ellen White na Waadventista kwa kupitia upotefu huu wamebadilisha sehemu sahihi ambayo Mungu amempa Kristo Yesu, na badala yake, Sheria, na hasa sheria ya Sabato! Wanataka wawapeleke watu kwenye Agano la Kale na waishi huko! Ni udanganyifu gani huu, hii ni kuinua sheria juu ya Yesu Kristo!
Ellen White alisema kwamba amri ya nne iling’aa juu ya zote na kuzungukwa na duara linalong’aa na ilitengwa kutunza heshima ya jina la Mungu! Anaendelea kusema kwamba kama amri ya nne inaweza kuvunjwa basi amri nyngine zote zinaweza kuvunjwa! (Early Writings of Ellen G. White, p.32,35). Labda hii inaweza kukusaidia kuelewa kwa nini Waadventista wengi wanasema kwamba kama tusipotunza sabato ni sawa na kusema tunaweza kufanya dhambi za kuvunja amri nyingine tisa! Hawaelewi kabisa Agano Jipya wanaposema “kama tunaweza kuvunja sabato ni sawa na kusema tunaweza kuzini!” (Haishangazi Waadventista hawawezi kusikia au kuelewa tunayosema wakati akili zao zimepofushwa na roho hii ya udanganyifu). Akili za Waadventista yamepotoshwa na mafundisho haya, na matokeo kwamba kushika sheria ni sehemu muhimu ya dini yao na ni aina hii ya dini ambayo Paulo alihubiri dhidi yake katika barua yake kwa Wagalatia. Tunaona kuwa mafundisho ya Wasabato juu ya siku ya saba hayatokani na maandiko bali yanatokana moja kwa moja na maono ya Ellen White ambayo yaliipa sheria nafasi ya kwanza badala ya Yesu Kristo. Nao Waadventista walitafsiri maandiko kufuatana na maono yake, na kwa kufanya hivyo wanapotosha maandiko yote!
Naelezea zaidi kuhusu hili katika makala yangu nyingine (Je, Tukusanyike Siku Gani Kati ya Jumamosi na Jumapili?), ila acha nioneshe hapa kwamba wale wanaohubiri kutunza/kufuata sheria ya Musa wapo kinyume na huduma ya Roho, wala hawajui huduma ya Roho katika maisha yao inayozaa matunda ya haki. Kwa kupitia huduma ya Roho tu ndio tunapata ubatizo katika Roho anayetupa uzima, uzima wa Yesu ndani yetu ambao kwa huo tunaishi maisha ya kitakatifu na kuzaa matunda ya haki. Kwa kutilia mkazo katika kufuata amri kumi, Waadventista wanazuia neema ya Kristo (Wagal. 1:6) na kujaribu utakatifu uliokamilika “katika mwili” badala ya katika imani na katika Roho ya Kristo (Gal 3:2,3). Waadventista hawaelewi nguvu ya Injili kama ilivyotangazwa katika Warumi 8:1-4. Kwa mantiki hii wale wanaofuata mafundisho ya Waadventista wamewekwa nje katika kujua nguvu ya ukombozi wa Kristo katika kuwafanya wenye haki na watakatifu, na katika mantiki hii, Uadventista sio Ukristo; zaidi ya hili, kiuhalisia, unapinga Injili kama Paulo alivyoweka wazi katika barua yake yote kwa Wagalatia.
Katika maono yake, tunaona kwamba Ellen White na Waadventista kwa kupitia upotefu huu wamebadilisha sehemu sahihi ambayo Mungu amempa Kristo Yesu, na badala yake, Sheria, na hasa sheria ya Sabato! Wanataka wawapeleke watu kwenye Agano la Kale na waishi huko! Ni udanganyifu gani huu, hii ni kuinua sheria juu ya Yesu Kristo!
Ellen White alisema kwamba amri ya nne iling’aa juu ya zote na kuzungukwa na duara linalong’aa na ilitengwa kutunza heshima ya jina la Mungu! Anaendelea kusema kwamba kama amri ya nne inaweza kuvunjwa basi amri nyngine zote zinaweza kuvunjwa! (Early Writings of Ellen G. White, p.32,35). Labda hii inaweza kukusaidia kuelewa kwa nini Waadventista wengi wanasema kwamba kama tusipotunza sabato ni sawa na kusema tunaweza kufanya dhambi za kuvunja amri nyingine tisa! Hawaelewi kabisa Agano Jipya wanaposema “kama tunaweza kuvunja sabato ni sawa na kusema tunaweza kuzini!” (Haishangazi Waadventista hawawezi kusikia au kuelewa tunayosema wakati akili zao zimepofushwa na roho hii ya udanganyifu). Akili za Waadventista yamepotoshwa na mafundisho haya, na matokeo kwamba kushika sheria ni sehemu muhimu ya dini yao na ni aina hii ya dini ambayo Paulo alihubiri dhidi yake katika barua yake kwa Wagalatia. Tunaona kuwa mafundisho ya Wasabato juu ya siku ya saba hayatokani na maandiko bali yanatokana moja kwa moja na maono ya Ellen White ambayo yaliipa sheria nafasi ya kwanza badala ya Yesu Kristo. Nao Waadventista walitafsiri maandiko kufuatana na maono yake, na kwa kufanya hivyo wanapotosha maandiko yote!