Uchaguzi 2020 NEC: Kuna Majimbo 4 hayajafanya Uchaguzi wa Madiwani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,496
9,278
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage amesema kuna majimbo manne ambayo uchaguzi wa madiwani haujafanyika.

Majimbo matatu Wagombea wamefariki na jimbo moja la Kibosho Kati karatasi za kura zimekosewa hivyo tume itapanga tarehe husika ya uchaguzi.

Akizungumzia hali ya uchaguzi mapema jioni hii, Jaji Kaijage amesema tume hiyo haijapokea taarifa za uwepo wa kura feki katika majimbo ya Kawe, Pangani na Kigoma.

Amewataka wananchi kuendelea kujitokeza kupiga kura katika muda huu mchache uliobaki.

Aidha, aliwataka wapiga kura kufanikisha upigaji kura wa amani na kuwataka wananchi ambao hawakujitokeza kupiga kufanya hivyo zikiwa zimebaki dakika chache kabla ya zoezi la kupiga kura kumalizika.
 
Yaani maandalizi ya uchaguzi yamefanyika kwa miaka mitano, mpaka jana jioni tume ya uchaguzi ilikuwa inasema kila kitu kiko sawa sawa kwa 100% kwa nchi nzima.

Ghafla leo watu wanafika kupiga kura, wanakuta kasoro nyingi za msingi ikiwemo hilo lililosemwa na tume usiku huu. Huu kama sio uwendawazimu ni nini?

Kosa la nani?
Nani atawajibika?
Nani atafidia hizo gharama?
 
Yaani maandalizi ya uchaguzi yamefanyika kwa miaka mitano, mpaka jana jioni tume ya uchaguzi ilikuwa inasema kila kitu kiko sawa sawa kwa 100% kwa nchi nzima.

Ghafla leo watu wanafika kupiga kura, wanakuta kasoro nyingi za msingi ikiwemo hilo lililosemwa na tume usiku huu. Huu kama sio uwendawazimu ni nini?

Kosa la nani?
Nani atawajibika?
Nani atafidia hizo gharama?

Kumbuka, hii ni general election. Kazi ya kuratibu general election katika nchi kubwa kama Tanzania sio kazi ya kitoto. While it’s possible to minimize logistical issue occurrences, it’s impossible to eliminate them.

Hakuna nchi duniani inayoweza kuratibu na kuendesha a perfect general election!
 
Chuki hii kwa Ndugu Pascal Mayalla inatoka wapi....? kwani akipewa cheo tatizo ni nini....? Mimi Nadhani ya kuwa ikitokea JF member ametunukiwa cheo it will be so proud to all JF Members...... Baadala yake watu wamejipa kazi ya Kukaanga Sumu huku nyuso zao wameelekeza Pembeni...... Ni ajabu na aibu....
 
NEC NI WAPUUZI
Yaani maandalizi ya uchaguzi yamefanyika kwa miaka mitano, mpaka jana jioni tume ya uchaguzi ilikuwa inasema kila kitu kiko sawa sawa kwa 100% kwa nchi nzima.

Ghafla leo watu wanafika kupiga kura, wanakuta kasoro nyingi za msingi ikiwemo hilo lililosemwa na tume usiku huu. Huu kama sio uwendawazimu ni nini?

Kosa la nani?
Nani atawajibika?
Nani atafidia hizo gharama?
 
Kumbuka, hii ni general election. Kazi ya kuratibu general election katika nchi kubwa kama Tanzania sio kazi ya kitoto. While it’s possible to minimize logistical issue occurrences, it’s impossible to eliminate them.

Hakuna nchi duniani inayoweza kuratibu na kuendesha a perfect general election!
Acha akili za kitoto.
Tume ya taifa ya uchaguzi ndio inaandaa, kuratibu na kusimamia shughuli zote za uchaguzi. Na siku zote tume imekuwa ikisema swala la kuandaa karatasi za wagombea hukamilika at least wiki tatu kabla ya uchaguzi ili kujipa nafasi ya kupitia, kurekebisha, kusafirisha na kukabidhi vifaa kwenye maeneo husika kabla ya siku ya kupiga kura.

Sasa jiulize tu, ni vipi leo jioni baada ya zoezi la kura kupigwa tume ndio inakuja na hizo blah blah za kusema karatasi kukosewa wakati uchapaji wake ulikamilika wiki tatu zilizopita?

Wewe unadhani hilo ni kosa la bahati mbaya au mpango mkakati?

Nani anawajibishwa?
 
Back
Top Bottom