Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,498
- 51,092
Ukisoma sheria za uchaguzi mkuu ya mwaka 2015 na mabadiliko yake yote na sheria ya matumizi kwenye uchaguzi kuna mambo yafuatayo:
1. NEC imepewa mamlaka ya kisheria kutangaza Tarehe ya Uchaguzi lakini Sheria haikuipa NEC mamlaka ya kutangaza tarehe rasmi ya kuanza kampeni! Je, mamlaka ya kutangaza tarehe rasmi ya wanasiasa kuanza kampeni NEC imeyatoa wapi?
2. Pili Sheria inataka NEC itoe kwenye Gazzette majina ya wateuliwa kugombea katika nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi miezi isiyopungua miwili na isiyozidi mitatu baada ya kuwa nominated, Kwa nini NEC mpaka hivi sasa haijatimiza sharti hili, maana imebaki miezi miwili tufanye uchaguzi lakini NEC mpaka sasa hivi haijapitisha majina ya wagombea wa uraisi au ubunge!
3. Sheria waziwazi imempa msajili wa vyama vya siasa uwezo wa kumuwekea pingamizi mgombea yeyote huko NEC kutokana na kuvunja sheria ya matumizi ya fedha kwenye uchaguzi na makosa mengine ya uchaguzi,Je ni mtu gani tena mwingine tena kwa mujibu wa sheria za uchaguzi tulizo nazo anaweza kumuwekea pingamizi mgombea na kwa vifungu vipi?
Naambatanisha hapa sheria ya uchaguzi ya mwaka 2015 na sheria ya makosa ya matumizi ya fedha kwenye uchaguzi.
1. NEC imepewa mamlaka ya kisheria kutangaza Tarehe ya Uchaguzi lakini Sheria haikuipa NEC mamlaka ya kutangaza tarehe rasmi ya kuanza kampeni! Je, mamlaka ya kutangaza tarehe rasmi ya wanasiasa kuanza kampeni NEC imeyatoa wapi?
2. Pili Sheria inataka NEC itoe kwenye Gazzette majina ya wateuliwa kugombea katika nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi miezi isiyopungua miwili na isiyozidi mitatu baada ya kuwa nominated, Kwa nini NEC mpaka hivi sasa haijatimiza sharti hili, maana imebaki miezi miwili tufanye uchaguzi lakini NEC mpaka sasa hivi haijapitisha majina ya wagombea wa uraisi au ubunge!
3. Sheria waziwazi imempa msajili wa vyama vya siasa uwezo wa kumuwekea pingamizi mgombea yeyote huko NEC kutokana na kuvunja sheria ya matumizi ya fedha kwenye uchaguzi na makosa mengine ya uchaguzi,Je ni mtu gani tena mwingine tena kwa mujibu wa sheria za uchaguzi tulizo nazo anaweza kumuwekea pingamizi mgombea na kwa vifungu vipi?
Naambatanisha hapa sheria ya uchaguzi ya mwaka 2015 na sheria ya makosa ya matumizi ya fedha kwenye uchaguzi.