Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Ndugu zangu wana Jamvi
Zimebaki siku chache watanzania wenye Umri kuanzia miaka 18 na kuendelea kulijongelea Sanduku la Kupiga kura ili Wafanye Maamuzi yatakaamua Hatma ya Maisha yao kwa kipindi kingine cha miaka 5 yaani kutoka 2010 mpaka 2015.
Siku zinapokaribia joto la Uchaguzi linapanda si tu kwa Wagombea wa nafasi mbali mbali bali hata kwa Wapiga kura ambao wengi mwaka huu wameonesha hamasa kubwa sana ya Kushiriki huu uchaguzi
Wiki kama moja iliyopita Tume ya Uchaguzi iliwataka Wananchi wote wakahakikishe majina yao katika vituo walivyojiandiskisaha kupigia Kura.
Tayari kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya wananchi kwamba hawajaona majina yao katika vituo walivyojiandikisha kupiga kura na hisia zimeanza kutawala na kulihisisha tukio hili na Kitendo kilichokuwa kikifanywa na Chama kimojawapo cha kuorodhesha namba za Shahada za kupigia kura
Sipendi kuchukua nafasi hii kumtafuta Mchawi, bali ningependa Kiravu, Makame na NEC kwa Ujumla watoe Muongozo ya nini kinapaswa kufanywa pale mtu anapokwenda kwenye kituo na kukuta Jina lake halipo kwenye Orodha iliyochapishwa
NEC Isipofanya hivyo itatufanya hata sisi wengine Kuamini kwamba NEC walipelekewa majina (nazungumzia yale yaliyokuwa yanaorodheshwa na Chama fulani) ili wayaondoe katika Orodha na kuwanyima wale waliodhaniwa ni Wapinzani wa Serikali Fursa ya Kupiga Kura
Naomba NEC wafanye yafuatayo
1: Kiravu na makame tunaomba mtueleze sisi ambao majina yetu hayachapishwa katika vituo tulipojiandikisha kupiga kura nini Tufanyeje
2: NEC ituambie ni kwa nini mtu amebadilisha kituo cha kupiga Kura lakini jina lake halikufutwa katika kituo cha mwanzo? Na huyu mtu ana kadi mbili kwa maana alipofanya marekebisho hamkuichukua ile ya kwanza na hamkumfuta katika kituo chake cha mwanzo, Je hili limefanywa Makusudi ili mtu huyu akipiga Kura Asubuhi TEMEKE aweze kuwahi kwenda kupiga kura kwenye kituo chake cha zamani cha Ubungo?
Asanteni sana
Zimebaki siku chache watanzania wenye Umri kuanzia miaka 18 na kuendelea kulijongelea Sanduku la Kupiga kura ili Wafanye Maamuzi yatakaamua Hatma ya Maisha yao kwa kipindi kingine cha miaka 5 yaani kutoka 2010 mpaka 2015.
Siku zinapokaribia joto la Uchaguzi linapanda si tu kwa Wagombea wa nafasi mbali mbali bali hata kwa Wapiga kura ambao wengi mwaka huu wameonesha hamasa kubwa sana ya Kushiriki huu uchaguzi
Wiki kama moja iliyopita Tume ya Uchaguzi iliwataka Wananchi wote wakahakikishe majina yao katika vituo walivyojiandiskisaha kupigia Kura.
Tayari kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya wananchi kwamba hawajaona majina yao katika vituo walivyojiandikisha kupiga kura na hisia zimeanza kutawala na kulihisisha tukio hili na Kitendo kilichokuwa kikifanywa na Chama kimojawapo cha kuorodhesha namba za Shahada za kupigia kura
Sipendi kuchukua nafasi hii kumtafuta Mchawi, bali ningependa Kiravu, Makame na NEC kwa Ujumla watoe Muongozo ya nini kinapaswa kufanywa pale mtu anapokwenda kwenye kituo na kukuta Jina lake halipo kwenye Orodha iliyochapishwa
NEC Isipofanya hivyo itatufanya hata sisi wengine Kuamini kwamba NEC walipelekewa majina (nazungumzia yale yaliyokuwa yanaorodheshwa na Chama fulani) ili wayaondoe katika Orodha na kuwanyima wale waliodhaniwa ni Wapinzani wa Serikali Fursa ya Kupiga Kura
Naomba NEC wafanye yafuatayo
1: Kiravu na makame tunaomba mtueleze sisi ambao majina yetu hayachapishwa katika vituo tulipojiandikisha kupiga kura nini Tufanyeje
2: NEC ituambie ni kwa nini mtu amebadilisha kituo cha kupiga Kura lakini jina lake halikufutwa katika kituo cha mwanzo? Na huyu mtu ana kadi mbili kwa maana alipofanya marekebisho hamkuichukua ile ya kwanza na hamkumfuta katika kituo chake cha mwanzo, Je hili limefanywa Makusudi ili mtu huyu akipiga Kura Asubuhi TEMEKE aweze kuwahi kwenda kupiga kura kwenye kituo chake cha zamani cha Ubungo?
Asanteni sana